Freemasonry Wametushika kila kona

Freemasonry Wametushika kila kona

Kama umeenda shule,nakushauri hiyo kitu achana nayo kabisa

Umenena vyema kwa mtu alieenda shule habari za freemason ni uozo mtupu, wasio na chakufanya ndio wanaentertain haya mambo
 
wanacontrol maisha yako fungua macho

Your life is 100% your responsibility. Kudhani kuna mtu anakucontrol ni kukosa akili kwa kiwango cha juu

Una elimu kiasi gani? Kama umefika hata chuo na bado unaamini huu upuuuzi itakuwa Umesoma TEKU

Watu waliokosa kazi, wasio na elimu au wanaowaza dini muda wote ndio wanaoentertain huu ujinga
 
Tafadhali kama una msimamo mkali wa dini ishia hapa usiendelee kusoma.

Nilikuwa kijiweni muda mfupi uliopita nacheza mchezo wa Draft. Kaja jamaa mmoja baada ya salamu jamaa mungine akauliza muda ili awahi kuondoka, akajibiwa kwamba ni saa moja na robo.
Sasa shida ikaanza kwa yule mgeni wetu, akatuuliza munawajua Freemasons? Nikajibu nawasikia kwamba ni mtandao wa matajiri wakubwa duniani. Jamaa akanicheka akasema umepotea kaka, hao ni waabudu shetani na wametushika kila kona. Nikambishia nikasema si kweli. Ndipo akaja na somo la saa au mfumo wa kusoma saa.

Akaanza kwa kuuliza sasa ni saa ngapi? nikamjibu saa moja. Akaniuliza hapo kwenye saa yako imeandikwa ngapi? Nikamjibu saba. Akasema emheeee hapahapo ndipo wametushika. Akauliza munajua kwa nini saa moja iandikwe saba? Nikajibu sijui. Akauliza munajua 666 alama ya mpinga kristo? Nikamjibu nasikiaga. Ndo sasa akaanza hesabu zake kama ifuatavyo.

1. Saa moja inaandikwa saba: 7-1= 6
2. Saa mbili inaandikwa nane: 8-2= 6
3. Saa tatu „ Tisa: 9-3= 6
4. Saa nne „ kumi: 10-4=6
5. Saa tano „ 11: 11-5 =6
6. Saa sita „ 12: 12-6= 6
7. Saa saba „ 13: 13-7=6
8. Saa nane „ 14: 14-8=6
9. Saa tisa „ 15: 15-9= 6
10. Saa kumi „ 16: 16-10=6
11. Saa kumi na moja „ 17: 17-11=6
12. Saa kumi na mbili „ 18: 18-12=6
Hapo akauliza mumenisoma? Wote tukajibu ndio mzeee.
Akasema kwa masaa 12 mengine Freemason wamefanya kama ifuatavyo.
1. Saa moja inaandikwa 19: 19-1=18=6+6+6
2. Saa mbili „ 20: 20-2=18=6+6+6
3. Saa tatu „ 21: 21-3=18=6+6+6
4. Saa nne „ 22: 22-4= 18=6+6+6
5. Saa tano. „ 23: 23-5= 18=6+6+6
6. Saa sita „ 24: 24-6= 18= 6+6+6
Hivyo kuanzia saa saba usiku inarudia tena kama hapo juu kabisa kuanzia namba 1-6. Hivyo tukabaki kimyaaa. Akasema ndo maana yeye hatumii mfumo wa 24hrs anatumia 12hrs system.

Sasa niwaulize wanajamvi kuna ukweli wowote hapa? Je nikweli Freemasons walivuruga saa makusudi? Je kuna ubaya kutumia 24hrs system?.

tuwe na tabia za kujisomea ili tuepukane na kudanganywa na kila mtu jamani,huyo mgeni wenu hana tofauti na wale waganga wa temeke walokamatwa na ch***pi a.k.a kufuli za dada zetu,huku wakipewa tiba kwa kutumia bomba kubwa,mkuu siku moja nilikaa pale nje kwenye jengo la freemason opposite na BOT kuna kijiwe cha kiwi pale,baada ya muda mfupi nilishuhudia akinamama wengi wakiingia ndani ya lile jengo wakaanza kuvutana na mlinzi kwa muda mrefu sana,Baadae wakaondoka nilipomuuliza yule watchman kulikoni alinijibu kwamba eti wale wakinamama walikuwa wameingizwa mjini na mtu huko street kwamba wampe mkwanja kdg ili awaunganishe na freemason ili wawe matajiri then waende makao makuu wakaanze kukinga mkwanja.....loooh nilipata mstuko mkubwa sn....
 
This is more than stupidity, watu wanakaa na kuwaza ujinga muda wote ndo hawa hawa wakiugua hata mafua husema wamerogwa, mchawi wako ni ujinga wako mwenyewe, ndo kakuloga ndo mana mpaka leo maisha kwako ni magum, kazi kushinda vijiweni,
 
Habari za Wacheza Draft..

Oho! Ebwana usitukoroge ndonya wacheza draft ,utapigwa force king bure!Mtoa mada ni pimbi tu kama pimbi wengine na upimbi wake hauhusiani na mchezo pendwa wa draft.yeye haoni uwepo wa mungu anamwona shetani kila mahala!
 
Kumbe ni kweli nchi hii inaongoza kwa ushirikina!!maana naona watu wengi wamejaa mawazo ya kichawi.Ni aibu sana kuwa na mawazo haya kwenye zama hizi
 
je wale wasioamini ktk hayo madhehebu yaliyoletwa na wakoloni na wafanyabiashara( wazungu na waarabu) inakuwaje au huyo mtu anatulazimisha kuwa waumini wa hao jamaa.
 
tuwe na tabia za kujisomea ili tuepukane na kudanganywa na kila mtu jamani,huyo mgeni wenu hana tofauti na wale waganga wa temeke walokamatwa na ch***pi a.k.a kufuli za dada zetu,huku wakipewa tiba kwa kutumia bomba kubwa,mkuu siku moja nilikaa pale nje kwenye jengo la freemason opposite na BOT kuna kijiwe cha kiwi pale,baada ya muda mfupi nilishuhudia akinamama wengi wakiingia ndani ya lile jengo wakaanza kuvutana na mlinzi kwa muda mrefu sana,Baadae wakaondoka nilipomuuliza yule watchman kulikoni alinijibu kwamba eti wale wakinamama walikuwa wameingizwa mjini na mtu huko street kwamba wampe mkwanja kdg ili awaunganishe na freemason ili wawe matajiri then waende makao makuu wakaanze kukinga mkwanja.....loooh nilipata mstuko mkubwa sn....

Aisee watanzania Sjui Nani katuloga! Hao wamama badala ya kukaanga samaki na mihogo wakidhi mahitaji yao wanaota kuoata hela kirahisirahisi tu!
 
tuwe na tabia za kujisomea ili tuepukane na kudanganywa na kila mtu jamani,huyo mgeni wenu hana tofauti na wale waganga wa temeke walokamatwa na ch***pi a.k.a kufuli za dada zetu,huku wakipewa tiba kwa kutumia bomba kubwa,mkuu siku moja nilikaa pale nje kwenye jengo la freemason opposite na BOT kuna kijiwe cha kiwi pale,baada ya muda mfupi nilishuhudia akinamama wengi wakiingia ndani ya lile jengo wakaanza kuvutana na mlinzi kwa muda mrefu sana,Baadae wakaondoka nilipomuuliza yule watchman kulikoni alinijibu kwamba eti wale wakinamama walikuwa wameingizwa mjini na mtu huko street kwamba wampe mkwanja kdg ili awaunganishe na freemason ili wawe matajiri then waende makao makuu wakaanze kukinga mkwanja.....loooh nilipata mstuko mkubwa sn....

Duh!
Hiyo kali. Sikuhizi kila nguzo ya UMEME imeandikwa namba ya simu kuunganishwa na Freemasons. Hata hao akina mama huwa wanachukua namba za simu kwenye hizo nguzo za umeme wanapiga kisha wanatapeliwa. Kwahiyo tusipokuwa makini mama zetu wanaibiwa sana kwa tamaa ya utajiri wabwerere.
 
Hii Kitu kuna jamaa Mombasa amejirekodi Hata video yake ilishapostiwa humu akitoa mawaidha kuhusu hao Freemason, ila hana ushahidi wowote wa maana zaidi ya kuonesha hajui Historia kuhusiana na mfumo wetu wa kuhesabu ulichanganywa na wauza watumwa waarabu,

kwani sisi pekee ndio tunaoona kuwa saa moja inaanzia pale mshale unapogota kwenye 7am kwa english kwa mswahili ndio kazoeshwa kuwa moja ndicho kitu cha kwanza hatukuzoeshwa kuanza na saba ndio maana hata Jumamosi ilijadiliwa wakaona waiite Mosi yaani Moja hivyo ni wazee wetu tu ndio waliamua kitu cha kwanza kianzwe na 7 au Mosi na hii imetokana sana na Lugha ya kiarabu kwani Al-khamis humaanisha siku ya Tano ya juma,Ijumaa ni Sita na saba ni Sabbath ili kuifuta hiyo saba kwani inahusika sana na Muumba hizi Mbingu ikageuzwa masikioni mwao na ikaitwa Mosi yaani Jumamosi... Huu mfumo ni wetu pekee tuliowekewa na mababu zetu wakilazimishwa na Waarabu... haihusiani kwa namna yeyote ile na Freemason.

Mimi nimeshuhudia sana watu wageni kutoka nchi tofauti hustushwa sana na mfumo wetu wa kuhesabu wengine wakiwemo hao ma member wa Freemason...

Huyu Jamaa ni Muongo sana akidai Mitstubish ni kampuni ya Jackie Chan,Ronadinho ni freemason ,Nembo ya Vodacom ina alama za 666 n.k bul shait...


nimeangalia hiyo video, Nimeamini elimu Muhimu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom