Freemasonry Wametushika kila kona

Freemasonry Wametushika kila kona

hizi kweli siku za mwisho yaani binadamu wanampa shetani umaarufu kuliko Mungu muumba nchi na dunia na vitu vyote vilivyopo ulimwenguni
haohao ndiyo ndiyo walikuja na habari ya Mungu kwa sasa mpango mzima ni Freemason (Wajenzi Huru)
 
Hivyo vyote hata kama Ni freemasons wamevipata kwa uwezo wa Mungu,it is simple,and I urge you to carry this kwamba,nothing is bad in this universe,only that it depends on how you handle it.Simple❗
 
Tafadhali kama una msimamo mkali wa dini ishia hapa usiendelee kusoma.

Nilikuwa kijiweni muda mfupi uliopita nacheza mchezo wa Draft. Kaja jamaa mmoja baada ya salamu jamaa mungine akauliza muda ili awahi kuondoka, akajibiwa kwamba ni saa moja na robo.
Sasa shida ikaanza kwa yule mgeni wetu, akatuuliza munawajua Freemasons? Nikajibu nawasikia kwamba ni mtandao wa matajiri wakubwa duniani. Jamaa akanicheka akasema umepotea kaka, hao ni waabudu shetani na wametushika kila kona. Nikambishia nikasema si kweli. Ndipo akaja na somo la saa au mfumo wa kusoma saa.

Akaanza kwa kuuliza sasa ni saa ngapi? nikamjibu saa moja. Akaniuliza hapo kwenye saa yako imeandikwa ngapi? Nikamjibu saba. Akasema emheeee hapahapo ndipo wametushika. Akauliza munajua kwa nini saa moja iandikwe saba? Nikajibu sijui. Akauliza munajua 666 alama ya mpinga kristo? Nikamjibu nasikiaga. Ndo sasa akaanza hesabu zake kama ifuatavyo.

1. Saa moja inaandikwa saba: 7-1= 6
2. Saa mbili inaandikwa nane: 8-2= 6
3. Saa tatu „ Tisa: 9-3= 6
4. Saa nne „ kumi: 10-4=6
5. Saa tano „ 11: 11-5 =6
6. Saa sita „ 12: 12-6= 6
7. Saa saba „ 13: 13-7=6
8. Saa nane „ 14: 14-8=6
9. Saa tisa „ 15: 15-9= 6
10. Saa kumi „ 16: 16-10=6
11. Saa kumi na moja „ 17: 17-11=6
12. Saa kumi na mbili „ 18: 18-12=6
Hapo akauliza mumenisoma? Wote tukajibu ndio mzeee.
Akasema kwa masaa 12 mengine Freemason wamefanya kama ifuatavyo.
1. Saa moja inaandikwa 19: 19-1=18=6+6+6
2. Saa mbili „ 20: 20-2=18=6+6+6
3. Saa tatu „ 21: 21-3=18=6+6+6
4. Saa nne „ 22: 22-4= 18=6+6+6
5. Saa tano. „ 23: 23-5= 18=6+6+6
6. Saa sita „ 24: 24-6= 18= 6+6+6
Hivyo kuanzia saa saba usiku inarudia tena kama hapo juu kabisa kuanzia namba 1-6. Hivyo tukabaki kimyaaa. Akasema ndo maana yeye hatumii mfumo wa 24hrs anatumia 12hrs system.

Sasa niwaulize wanajamvi kuna ukweli wowote hapa? Je nikweli Freemasons walivuruga saa makusudi? Je kuna ubaya kutumia 24hrs system?.

Hii Kitu kuna jamaa Mombasa amejirekodi Hata video yake ilishapostiwa humu akitoa mawaidha kuhusu hao Freemason, ila hana ushahidi wowote wa maana zaidi ya kuonesha hajui Historia kuhusiana na mfumo wetu wa kuhesabu ulichanganywa na wauza watumwa waarabu,

kwani sisi pekee ndio tunaoona kuwa saa moja inaanzia pale mshale unapogota kwenye 7am kwa english kwa mswahili ndio kazoeshwa kuwa moja ndicho kitu cha kwanza hatukuzoeshwa kuanza na saba ndio maana hata Jumamosi ilijadiliwa wakaona waiite Mosi yaani Moja hivyo ni wazee wetu tu ndio waliamua kitu cha kwanza kianzwe na 7 au Mosi na hii imetokana sana na Lugha ya kiarabu kwani Al-khamis humaanisha siku ya Tano ya juma,Ijumaa ni Sita na saba ni Sabbath ili kuifuta hiyo saba kwani inahusika sana na Muumba hizi Mbingu ikageuzwa masikioni mwao na ikaitwa Mosi yaani Jumamosi... Huu mfumo ni wetu pekee tuliowekewa na mababu zetu wakilazimishwa na Waarabu... haihusiani kwa namna yeyote ile na Freemason.

Mimi nimeshuhudia sana watu wageni kutoka nchi tofauti hustushwa sana na mfumo wetu wa kuhesabu wengine wakiwemo hao ma member wa Freemason...

Huyu Jamaa ni Muongo sana akidai Mitstubish ni kampuni ya Jackie Chan,Ronadinho ni freemason ,Nembo ya Vodacom ina alama za 666 n.k bul shait...
 
Last edited by a moderator:
Swali langu linamaanisha kwanini 6 (666) na isiwe ni no nyingine kama 7,9 n.k. Yaani ilikuaje ikawa hyo namba mnayoisema??

Wataalam wa Bible wanasema ilianzia kipindi cha mfalme Solomon malkia wa Sheba alipeleka vipande vya dhahabu 666.
 
Mambo ya kwenye draft. Hapa JF kuna Uzi upo kule jamii intelligency kama sikosei umeandikwa: "Freemason inside out" yaani kila kitu kuhusu Freemason, huwa hamuusomi?
 
Wataalam wa Bible wanasema ilianzia kipindi cha mfalme Solomon malkia wa Sheba alipeleka vipande vya dhahabu 666.

Samahani bado kama sijaelewa vizuri do queen of Sheba alivyopeleka hivyo vipande vya dhahabu 666 inahusiana vipi na namba ya mpnga Kristu??
 
Tafadhali kama una msimamo mkali wa dini ishia hapa usiendelee kusoma.

Nilikuwa kijiweni muda mfupi uliopita nacheza mchezo wa Draft. Kaja jamaa mmoja baada ya salamu jamaa mungine akauliza muda ili awahi kuondoka, akajibiwa kwamba ni saa moja na robo.
Sasa shida ikaanza kwa yule mgeni wetu, akatuuliza munawajua Freemasons? Nikajibu nawasikia kwamba ni mtandao wa matajiri wakubwa duniani. Jamaa akanicheka akasema umepotea kaka, hao ni waabudu shetani na wametushika kila kona. Nikambishia nikasema si kweli. Ndipo akaja na somo la saa au mfumo wa kusoma saa.

Akaanza kwa kuuliza sasa ni saa ngapi? nikamjibu saa moja. Akaniuliza hapo kwenye saa yako imeandikwa ngapi? Nikamjibu saba. Akasema emheeee hapahapo ndipo wametushika. Akauliza munajua kwa nini saa moja iandikwe saba? Nikajibu sijui. Akauliza munajua 666 alama ya mpinga kristo? Nikamjibu nasikiaga. Ndo sasa akaanza hesabu zake kama ifuatavyo.

1. Saa moja inaandikwa saba: 7-1= 6
2. Saa mbili inaandikwa nane: 8-2= 6
3. Saa tatu „ Tisa: 9-3= 6
4. Saa nne „ kumi: 10-4=6
5. Saa tano „ 11: 11-5 =6
6. Saa sita „ 12: 12-6= 6
7. Saa saba „ 13: 13-7=6
8. Saa nane „ 14: 14-8=6
9. Saa tisa „ 15: 15-9= 6
10. Saa kumi „ 16: 16-10=6
11. Saa kumi na moja „ 17: 17-11=6
12. Saa kumi na mbili „ 18: 18-12=6
Hapo akauliza mumenisoma? Wote tukajibu ndio mzeee.
Akasema kwa masaa 12 mengine Freemason wamefanya kama ifuatavyo.
1. Saa moja inaandikwa 19: 19-1=18=6+6+6
2. Saa mbili „ 20: 20-2=18=6+6+6
3. Saa tatu „ 21: 21-3=18=6+6+6
4. Saa nne „ 22: 22-4= 18=6+6+6
5. Saa tano. „ 23: 23-5= 18=6+6+6
6. Saa sita „ 24: 24-6= 18= 6+6+6
Hivyo kuanzia saa saba usiku inarudia tena kama hapo juu kabisa kuanzia namba 1-6. Hivyo tukabaki kimyaaa. Akasema ndo maana yeye hatumii mfumo wa 24hrs anatumia 12hrs system.

Sasa niwaulize wanajamvi kuna ukweli wowote hapa? Je nikweli Freemasons walivuruga saa makusudi? Je kuna ubaya kutumia 24hrs system?.
An idle mind is a workshop of the devil.... Huu upuuzi unaweza ukawa umeanzishwa na mtu mmoja anayejiita mkristu, licha ya wajibu wa kujenga ufalme wa Mungu ('ufalme wako ufike') yeye yuko busy kujenga ufalme wa giza..'
 
Haha 7-1=6 na sio 666. Bible imesema 666 lakn mnaleta ujaaaaanja ulchoka sana kwahuu uzi
 
Samahani bado kama sijaelewa vizuri do queen of Sheba alivyopeleka hivyo vipande vya dhahabu 666 inahusiana vipi na namba ya mpnga Kristu??

Hata Mimi sijui lakini naamini kuna watu hapa wanaelimu kubwa watatusaidia. Mimi nimekopi na kupaste kama nilivyodimuliwa sijui chochote.
 
Haha 7-1=6 na sio 666. Bible imesema 666 lakn mnaleta ujaaaaanja ulchoka sana kwahuu uzi

Mkuu hapo jamaa kuna uhuni anafanya na hizo namba anazikorogakoroga anapata hiyo 666. Lengo kutuvuruga tu. Nilijaribu kubishananae lakini alinishinda kwasababu yeye anaongea na data zake na alijipanga wakati mimi nilikuwa sina data na sikujiandaa.
 
Hata Mimi sijui lakini naamini kuna watu hapa wanaelimu kubwa watatusaidia. Mimi nimekopi na kupaste kama nilivyodimuliwa sijui chochote.

Anhaaa!! sawa lakini sidhani kama kuna mtu anahiyo elimu yenye jibu kwanini ni 666 na sio namba nyingine...
 
Sema wewe umeshikwaa ! au usiseme kila mtu ni maskini kwa kuwa huna pesa wewe !
HAO FREMASON; MIMI HAWAWEZI KUNISHIKA !
 
Mbingu na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana. Dunia na wote wakaao ni mali yake. Ukumwamini Mungu wa kweli hitotishwa na hao.
Soma kwenye biblia. Watumishi wa Mungu walipanda mbegu. Usiku adui akaja akapanda magugu. Hayo ya free manson ni magugu ambayo Yesu aliruhusu yamee pamoja na ngano!
 
Back
Top Bottom