Freeman Mbowe na kupanda na kushuka kwa CHADEMA!

Freeman Mbowe na kupanda na kushuka kwa CHADEMA!

Eti kashuka kiwango! Mbowe ni sawa na bondia maarufu ambaye akipanda jukwaani mnamfunga miguu kisha mnatangaza kashuka kiwango mbona anashindwa Ku dance wakati wa pambano.
Mnamzuia kufanya siasa majukwaani kisha mnamtungia kuwa kashuka kiwango? Aliyeshuka kiwango ni kama mzee Malecela ukimlinganisha na PMs waliopita kiasi cha kujipendekeza walao mama arudishwe kazini. Ramli hizi zinegonga ukuta
Unafaa kuwa Greatest thinker kwelikweli
 
Tatizo lako sio kwamba hujui kuandika ila ni aidha umeathiriwa na eneo ulilokulia au huna elimu ya kutosha katika matumizi ya vishazi, uchanganyaji wa irabu na silabi ili kupata uandishi fasaha au muundo sahihi wa sentensi.
Mm namuhamini sana mbowe sana turimujuwa chacha bobu wangwe kupitia mbowe turimujuwa zito kabwe kupitia mbowe turimujuwa john munyika kupitia mbowe arima mdee kupitia mbowe turimujuwa tundu risu kupitia mbowe nashanga unatoa oja kwa kumpinga mbowe unatoka wapi
 
Mkuu Wille Malecela

Hapa Umejenga hoja za msingi sana

Hongera sana kwa hilo

You have brains sometimes..Kudos

Nakubaliana na wewe kuwa Mbowe amefanya kazi kubwa sana CHADEMA lakini hadi sasa amefika mwisho wa uwezo wake....Hawezi kufanya cha zaidi na tofauti

Wasiwasi wangu ni Je....Nani anapaswa kupewa hiyo kazi kubwa ya kukikarabati chama?

Na je Mbowe kutokana na sacrifice aliyoifanya hadi CHADEMA kufika hapo atakuwa tayari kukiacha chama ?

Na je ....Kuna Process zozote zinazoonesha kuna SUCCESSION PLAN ambayo iko Inaishi ndani ya CHADEMA

Again wille...Thanks kwa hoja nzuri

cc Nguruvi3 Mchambuzi Mzee Mwanakijiji
Nakubaliana na wewe kua mbowe kafanya makubwa sana CDM na pia yapo mapungufu mengi pia,ila sikubaliani kua CDM inaelekea kufa,kama uwanja a siasa ungekua sawa pengine ningekubaliana na hoja yako,ila kwa maoni yangu kinachofanya CDM idumu na kuimarika ni ubovu wa ccm,ccm si chama cha siasa kama CDM kile ni chama dola,kinatawala hakiongozi ndio
 
Tatizo lako sio kwamba hujui kuandika ila ni aidha umeathiriwa na eneo ulilokulia au huna elimu ya kutosha katika matumizi ya vishazi ili kupata uandishi fasaha.
But mimi nimemwelewa.
Ujumbe umefika mwaya!!
 
Kumuelewa sio hoja tena hata mimi nimemwelewa kwa sababu lugha ni nasibu...ila ina sarufi zake, hoja iliyoibuka ni athari za kimazingira katika uandishi wake. Na nacho jaribu kumsaidia ili asionekane kichwa maji kutokana na aina ya uandishi.

Fikiria ndio amehitimu kidato cha nne na bado anaundishi huo! Hajui kanuni za uandishi!! Hapa kunatatizo kubwa kuanzia kwa mwalimu wake mpaka jamii ukiwamo na wewe.
But mimi nimemwelewa.
Ujumbe umefika mwaya!!
 
Una tatizo la kuwa incoherent kwenye analysis zako. You are all over the place, umeanza kama unataka kujadili uwezo wa Mbowe kama kiongozi, then unahitimisha kwamba hakuna upinzani serious dhidi ya Chama tawala. Hapohapo tena umefananisha kinachoendelea ndani ya Chadema kwa sasa na Chama cha Democrats cha Marekani. Seriously? Sasa kama unasema Chadema haiwezi kuwa upinzani thabiti dhidi ya CCM unawezaje kuifananisha Chadema na Democratic party ya USA. Hakuna mantiki hapo. Maana inafahamika kwamba, kwanza, Democrats wamepata popular votes almost milioni mbili zaidi ya Republicans walioshinda chaguzi karibu katika kila ngazi ya chaguzi za USA awamu hii.

Sure, Democrats walishindwa kwenye electoral votes, kwa ngazi ya urais, na uwezekano wao kurudi madarakani hivi karibuni bado mkubwa sana tu. Sasa huwezi kuwafananisha na Chadema ambao hawajawahi kushinda majority votes Tanzania kwa ngazi za chaguzi zote tangu wazaliwe kama Chama. Isitoshe, kupotea kimaono kama chama au mtu mmoja mmoja ni kitu cha kawaida sana, na haimaanishi kwamba chama ndo kimepotea forever. Hivi unajua hata CCM walipotea sana kimaono kwa muda mrefu sana tu, mpaka angalau sasa unaona vision ya CCM kupitia Magufuli, ambaye unaweza kumkosoa kwenye tactics anazotumia kufikia vision yake lakini vision yake ipo fairly clear: kusafisha uchafu ulioachwa na watangulizi wake wakiwemo wakina Malecela, Sumaye, Lowassa etc.

- Dmocrats sasa wametangaza wapo kwenye kipindi cha kujitafakari baada ya kushindwa kila ngazi ndio maana nikasema hata Chadema wapo kwenye same state of policitics wameshindwa wanahitaji kujitafakari, wewe naona unaongelea uchaguzi wa USA kwani hapa unahusu mkuu?

le Mutuz
 
Umejitahidi kuwa convince waliokutuma kwamba pesa waliyokupatia has been properly accounted for. One thing you have forgotten is to advise your don to obey the law and govern by using the constitution. Mwambie afanye hivyo muone moto wake. Kwa mfano kutumia bwana yule kujaribu kumdhoofisha maalim hakuwasaidii sana bali huwadhoofisha kwenye macho na ufahamu wa mwenye akili za kawaida tu

- ina maana kuna wanaokulipa pesa pole sana sio wote tupo kama wewe

le Mutuz
 
kwani lemututz nini kigezo cha kushuka CDM Chini ya Mbowe? ninavyo jua ...Kwa ujasiri mbowe amekiongoza chama kwa ujasiri mkubwa sana na mwaka jana wakati wa uchaguzi walifanya maamuzi mazuri kuunganisha nguvu kuunda ukawa. juu ya kuhujumiwa na ccm lakini ni ukweli usio pingika uongozi wake ulifanukisha cdm kupata wabunge wengi zaidi ya chaguzi zilizo pita . kura za mgombea wa ukawa ni zaidi ya 40% sawa na 6 m kura na huku ushindi wa ccm ukiwa ni 8m ...tofauti ya kura 2m tu ..na hizi ukijumlisha za wizi , na zile za vijijini ambako upinzani unashindwa kufikia kutokana na fedha na muda wa kufikia maeneo yote. pia hawa 2m ni wale ambao wako less informed kuhusu siasa za Tz wengi wao bado wanadhani chama ni cha nyerere tu..hata kama kinavurunda.

hivyo ushauri wako sio sawa kwa sababu cdm imepata mafanikio makubwa na imekubalika maeneo yote ya mijini ambako watu ni well informed.
Dar waliichukua chini ya mbowe
Iringa
Mbeya
Moshi
Arusha
Tanga
hata Mwanza juu ukabila ulitumika lakini jiji hilo ni moja katika ngome kubwa ya cdm.
amejitahi na bado ana uwezo mkubwa wa kuongoza, kinachotakiwa sana ni kuona UKAWA unaimarika zaidi , ccm kupigana nayo peke yake ni ngumu ni chama dola na inatumia kila silaha at their disposal hata haram
sasa ushauri kwa mbowe ni kuona ukawa inasimama kwa nguvu zaidi na kufanya tathmini ya uchaguzi kisayansi kuona nini kilipita hata wakakosa baadhi ya majimbo na wapi walikosea hadi kura 2m zikaenda kwa magufuli. huo ndio ushauri wakiufanya kazi na kuja na recomandations basi ni wazi mbowe ataona 2020 ukawa ukiingia madarakani juu ya vitisho watavo kabilina navyo

- Mkuu yote hayo ya mafanikio ya mwaka jana nimeyajumuisha kwenye mafanikio yake na hicho chama ila kwa sasa chama kimekosa muelekeo, ni mtizamo tu na wewe unaweza kuwa na wako tofauti ni sawa

le Mutuz
 
Mm namuhamini sana mbowe sana turimujuwa chacha bobu wangwe kupitia mbowe turimujuwa zito kabwe kupitia mbowe turimujuwa john munyika kupitia mbowe arima mdee kupitia mbowe turimujuwa tundu risu kupitia mbowe nashanga unatoa oja kwa kumpinga mbowe unatoka wapi
mh! kuna wakati hata Kiswahili nacho kinakuwa kigumu aiseeee!!!!!
 
Le Mutz unashangaza sana hivi uliwahi kuona wapi heavy weight akapigana na light weight tena aliyefungwa mkono mmoja na kushinda?? Mwambie ndugu yako JPM aweke ulingo sawa wa siasa kwa vyama vyote alafua aone, sio yeye afanye siasa wengine NO.
 
We saizi yako ni wale wanawake mnaotukanana nao kule Instagram hapa umeingia kwenye kina kirefu nakushauri urusi kule mnakogombana na wanawake kila dakika.
 
Nakubaliana na wewe kuwa Mbowe amefanya kazi kubwa sana CHADEMA lakini hadi sasa amefika mwisho wa uwezo wake....Hawezi kufanya cha zaidi na tofauti

Wasiwasi wangu ni Je....Nani anapaswa kupewa hiyo kazi kubwa ya kukikarabati chama?

Na je Mbowe kutokana na sacrifice aliyoifanya hadi CHADEMA kufika hapo atakuwa tayari kukiacha chama ?

Na je ....Kuna Process zozote zinazoonesha kuna SUCCESSION PLAN ambayo iko Inaishi ndani ya CHADEMA

Again wille...Thanks kwa hoja nzuri
[/USER]
Mkuu nianze na hoja yako ya mwisho. Hili la succession plan

Baada ya uchaguzi tulisema,KUB awe mtu mwingine kama succession plan

Pili, vijana wapewe nafasi ya kutumia talent zao. Hiyo ni succession plan.

Muundo wa kupata viongozi ubadilike. K/mkuu iwe nafasi ya kuomba

Matokeo ya mapungufu haya ni kuwa na katibu mkuu aliyepwaya

Kuhusu sacrifice na kuacha chama, hili ni suala la Demokrasia.

Alikuwepo Mzee Mtei akampa Marehemu Makani na Mbowe hana choice

Anachotakiwa ni kulea viongozi wajao ambalo ni jukumu lake kwa sasa

Kuhusu kukarabati chama, nalo si suala la mtu ni suala la chama kama taasisi

Anapaswa kuongoza ukarabati na siye yeye kuwa mkarabati

Kuhusu kutokuwa na impact, nalo tuliwahi kusema.

Kwamba amefanya mengi na sacrifice hilo halina ubishi.

Na kwamba ni wakati wa kutoa kijiti. Ameongoza kwa muda wa kutosha

Naliona tatizo kwa CDM katika mambo yafuatayo
1. Lazima safu ya uongozi na hasa katibu mkuu isukwe upya

2. Hakuna sababu za uchaguzi mkuu tofauti na uchaguzi wa Mwenyekiti

Hivi unawezaje kutenga safu za uongozi kwa nyakati?

Yaani uongozi mpya na sekretariati iliyochaguliwa wakati tofauti. Haileti maana

3. Hakuna jitihada za 'amalgamation' kati ya waliohamia na zamani.

Hili lina highlight tatizo la ukarabati na linaashiria mzozo muda si mrefu

Ili kuleta harmony lazima kuwe na new leadership.

CDM wana pool of talents kinachokosekana ni leadership

Mwenyekiti kama tulivyosema ametumika and he has nothing new to offer
 
Ccm inashuka sana,vilevile pamoja nakuzuia mikutano bado cdm niwazuri sana.tuendelee kuwekeza vijijini,
 
Back
Top Bottom