Cherenganya
JF-Expert Member
- Jan 21, 2018
- 2,309
- 1,787
- Thread starter
-
- #121
Kaka tunazungumzia situation iliyopo Rais aliyepo madarakani hataki kuishi kwa mazoea mwisho, Sasa njia nyingine ni nguvu ya bunge ambayo obviously haipo, ya pili ni Maandamano ambayo sioni hilo likitokea, na la mwisho ni kwenye sanduku la kura (labda hapa)Uko sahihi kabisa. Lakini nchi siyo mali ya mtu mmoja wala kikundi kidogo cha watu. Ushindani wa kisiasa unayo misingi yake iliyokubalika duniani kote. Tangu nchi hii iingie kwenye mfumo wa vyama vingi imekuwa ikijaribu kuheshimu misingi hiyo na ndiyo maana idadi ya wawakilishi kutoka upinzani imekuwa ikiongezeka kila uchaguzi unapofanyika. Mtu anayekerwa na hali hiyo hafai kuwa kiongozi. Kama kwa bahati mbaya amepata uongozi lazima utafika wakati ataambiwa kuwa huo mchezo wake mbaya ni mauti kwa taifa na haukubaliki. Nadhani uchaguzi wa serikali za mitaa umetufikisha hapo.
Kula tano kakaMiguna miguna yuko Canada alijaribu kurudi Kenya akaishia uwanja wa Ndege kwa kubebwa mzobemzobe.
wakati Odinga akigongeana glass na Kenyata.
Lissu Juzi amejaribu kurudi, baada ya kufika Kenya akaona upepo unasoma vibaya akageuzia huko huko.
Huku Mbowe akifanya maridhiano na Serikali ya CCM.
Kaka tunazungumzia situation iliyopo Rais aliyepo madarakani hataki kuishi kwa mazoea mwisho, Sasa njia nyingine ni nguvu ya bunge ambayo obviously haipo, ya pili ni Maandamano ambayo sioni hilo likitokea, na la mwisho ni kwenye sanduku la kura (labda hapa)
Sent using Jamii Forums mobile app
Niwe mkweli, sioni mwisho mzuri wa Mbowe na Lissu. Sidhani yupo aliyefikiri ipo siku Mbowe ataingia kwenye mgogoro na Dr Slaa lakini Mbowe hajali inapokuja jambo ambalo yeye anaona lina manufaa kwake.
Pona ya Lissu ni awe kama akina Lema na Boni lakini akitaka kutumia akili zake kisawasawa mtaona kitachotokea. Save this post ..[emoji41]
Wakiomba watasamehewa hakuna shida wote ni wa TZ.
Maridhiano juu ya nini? Sema Chadema imenyoosha mikono. Imeushindwa muziki wa Jiwe sasa wanaomba poo kiaina, eti maridhiano. Na vijana wa Chadema mliojana humu mmeshupalia maridhiano, maridhiano! Yapi? Ninyi si mna msemo "mpaka kieleweke"? Vipi sasa kubembeleza maeidhiano!!!?
Mjinga wa siku! Hii ndio falsafa ya wasio na hoja! Yaani mawazo yenu mgando hamtaki wenye akili kubwa kuyakandia! Kwa taarifa yako, huyo ndiye rais wako ajaye 2020! Lamba jivu upooze kiungulia!
Rais aliishasema, anayefikiri atamkwamisha, atakwama yeye. Akina Mbowe na washauri wake wakafikiri anatania. Mara UKUTA, mara Mange Kimambi, mara kususia chaguzi ndogo, mara kususia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Na sasa eti mnaomba maridhiano. Halafu mmeshupaza shingo kweri kweri, maridhiano, maridhiano!Hata kuandika habari za cdm unatetemeka kudadeeeeekiiiii, Njaaaa hiyo sasa huna tena sehemu ya kupeleka hayo majungu yenu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Muda utasema ila nina wasiwasi kuna jambo linaendelea.Yule bwana mkubwa hawezi kufanya maridhiano na wapinzani. Kwasabb makungwi wake (M7 na PK) hawajawahi kukaa meza moja na wapinzani mpk leo. Na hawa ndiyo wamempa mbinu zote za kuukandamiza upinzani.
Mbowe amejaribu kutafuta namna ya kumteka huyu jamaa kwa kujishusha lkn roho na dhamira ya huyu jamaa havimruhusu kufanya maridhiano na wapinzani. PK and M7 will hit him!
Ulichokiongea kama hisia zako ndiyo ukweli wenyewe haujakosea chochot, ila kwa muhtasari wa nchi binafsi naliona hilo ni jambo jema kwa namna yoyote ile.Kwanza sitaki kuamini kuwa Mbowe alishiriki katika lile tukio hivi hivi tu bali kushawishiwa na watu wa sytem na wasaidi wengine wa Bwana mkubwa na pia sitaki kuamini kuwa alikwenda kushirikia bila kushirikisha viongozi wenzake ndani ya chama hivyo kuna uwekano mkubwa Mbowe alitoa kauli ile akijua kinachoendelea ingawa pia inawezekana kaingia katika mtego kwa faida ya Bwana yule asietaka kuonekana kuwa anaweza kushindwa katika misimamo yake(nitaeleza huko mbele).
Kosa alilolifanya Mbowe na chama chake kwa ujumla, ni kushiriki tukio lile bila kushauriana na viongozi wengine wa upinzani ambao naamini wangeshirikishwa,basi aliyoyasema Zitto yasingetokea hata kama wasingefikia muafaka wa pamoja kuwa Mbowe ashiriki.
Nikirudi kwenye mada,nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa Bwana yule alikuwa hajui Mbowe ataongea alichoongea bali alitaka Mbowe ndio aonekana mtafuta suluhu kwanini yeye siku zote hataki kuonekane ameshindwa(hataki kupangiwa).
Na ndio maana baada tu ya Mbowe kuongea,vijana wa Lumumba wakaanza propaganda za kusema Mbowe kaomba suluhu na maneno mengine mengi ili mwisho wa siku wapinzani ndio waonekane wameshindwa katika mapambano ya kudai haki na sasa wanategemea huruma ya Bwana yule kumbe Bwana yule nae anabanwa na pressure ya ndani na nje ya nchi kutokana na aina ya uongozi wake hasa uminyaji wa demokrasia na unyanyasaji kwa wapinzani.
Naamini katika kujisafisha na ili asiendelee kuvurugana na Bwana wakubwa wa hii dunia,Bwana yule ameona kuna umuhimu wa kujirudi japo kidogo, hivyo anaweza kuja kufanyia kazi wazo la Mbowe ingawa anaweza kufanya hivyo kwa kuwazuga tu mabeberu hivyo wawe makini nae.
Ni imani yangu pia, Mbowe kwa upande wake, aliamua kujishusha ili atumie fursa iliojitokeza(akijua kinachoendelea) hivyo akaongea alichoongea ikiwa ni utekelezaji wa kinachoendelea chini ya kapaeti.
Inawezekana kabisa watu wa system hawakumshirikisha Zitto na chama chake hasa kutokana na Zitto kwa sasa kuonekana ni mtu anaemkosoa na kumpinga vibaya sana Bwana yule na pia wakiamini chama cha Zitto hakina wafuasi wengi kama CHADEMA hivyo impact yake haitokuwa kubwa ingawa kwa hili wanaweza kuwa hawakuwaza sawaswa.
Huu ni mtazamo wangu ila muda ndio msema kweli.
Hiyo hekima aitumie kwenye uchaguzi wa mwenyekiti kwa kuwaachia na wengine wagombee bila vitishombowe aliongea kwa hekima sana. hekima hutoka kwa Mungu. tusimbeze Mbowe.
Inawezekana kwa kujua hili,ndio maana hata Mbowe alikubali kushiriki tukio lile.Kalazimishwa na wastaafu alete mshikamano wa kitaifa lasivyo wenye chama wampoke tiketi ya kugombea 2020 so tegemeeni ushirikiano wa kutosha kati yake na wapinzani kuelekea uchaguzi 2020 na baada ya uchaguzi.