Freeman Mbowe - Afanya maajabu Houston TX

Freeman Mbowe - Afanya maajabu Houston TX

Mkwawa

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2011
Posts
1,334
Reaction score
1,466
DSC00467.JPG DSC00462.JPG Wengi wajiunga Chadema, Mkusanyiko ulikuwa ni mkubwa sana kwa historia ya mwana siasa yeyote aliyewahi kutokea Houston TX .

Mbowe awabadili Wana CCM na kuwa Chadema.

Mbowe afanya Houston kuwa base ya CHADEMA na wanachadema watoa Pikipiki 126
 
Mungu aendelee kuwalinda hadi wa maono yenu wana wa ukombozi wa nchi hii.
 
Weka picha wacha porojo, za Kinana tumeona DC.

Ukute ni afadhali ya Lema pale bar ya Wakenya, London.
 
Hivi siku hizi mambo yote ni kwa diaspora? Hivi ni kweli wanaenda kufungua matawi au wanasukumwa na posho na kutembea ughaibuni? Mipango ya diaspora kupiga kura ikoje ifikapo 2015 manake isiwe kufungua tu matawi lakini mwisho wa siku hao wanachama wanakuwa hawana maamuzi siku ya kupiga kura!
 
Hivi siku hizi mambo yote ni kwa diaspora? Hivi ni kweli wanaenda kufungua matawi au wanasukumwa na posho na kutembea ughaibuni? Mipango ya diaspora kupiga kura ikoje ifikapo 2015 manake isiwe kufungua tu matawi lakini mwisho wa siku hao wanachama wanakuwa hawana maamuzi siku ya kupiga kura!

Mimi wananikera sana.
 
mkwawaaaa
acha hizo,
ukweli wa mambo hayo daima huthibitishwa na reliable source na evidence au habari liliyoshiba.
unataka udhaniwe hukujiandaa kuanzisha uzi huu?
weka picha kama ulihudhuria, ongeza taarifa zaidi kama ulishudia au hata kama umehadisiwa
laa! hauna usiwe unaanzisha uzi kwa style hii!

guess how sensitive is the story?
 
Hivi siku hizi mambo yote ni kwa diaspora? Hivi ni kweli wanaenda kufungua matawi au wanasukumwa na posho na kutembea ughaibuni? Mipango ya diaspora kupiga kura ikoje ifikapo 2015 manake isiwe kufungua tu matawi lakini mwisho wa siku hao wanachama wanakuwa hawana maamuzi siku ya kupiga kura!
Kuna wanachama wanaojiandaa kwenda ground,sioni shida waki organize.Adui ni ccm.
 
Hivi siku hizi mambo yote ni kwa diaspora? Hivi ni kweli wanaenda kufungua matawi au wanasukumwa na posho na kutembea ughaibuni? Mipango ya diaspora kupiga kura ikoje ifikapo 2015 manake isiwe kufungua tu matawi lakini mwisho wa siku hao wanachama wanakuwa hawana maamuzi siku ya kupiga kura!

wewe inaelekea umejifungia kwenye kibox kidogo au tayari umeshalewa falsafa za magamba kwamba kila anayetoka nje ya Tanzania ni kwa ajili ya posho au mambo binafsi! Kwanza uelewe lazima chama kijimbanue ndani na nje ya nchi na pia kuna mchakato mzima wa katiba na hili la watu walio ughaibuni kuruhusiwa kupiga kura kwenye balozi zetu au kwa njia ya mtandao litaingizwa so kamanda mbowe yupo kueleza itikadi na falsafa za chama nje ya Tanzania na kutafuta marafiki pia!!na kuhamasisha watanzania walio nje wenye kipato kizuri wawekeze Tanzania na wasaidie pia vuguvugu la M4C ili 2015 mambo yaende sawa!
 
Wengi wajiunga Chadema, Mkusanyiko ulikuwa ni mkubwa sana kwa historia ya mwana siasa yeyote aliyewahi kutokea Houston TX . Mbowe awabadili Wana CCM na kuwa Chadema. Mbowe afanya Houston kuwa base ya CHADEMA na wanachadema watoa Pikipiki 126

Nimeipenda hiyo kwani itawachanganya ccm na Nape akiona Pikipiki hizo 126 atazusha kuwa zimetolewa na wafadhili wa kizungu!
 
Wengi wajiunga Chadema, Mkusanyiko ulikuwa ni mkubwa sana kwa historia ya mwana siasa yeyote aliyewahi kutokea Houston TX . Mbowe awabadili Wana CCM na kuwa Chadema. Mbowe afanya Houston kuwa base ya CHADEMA na wanachadema watoa Pikipiki 126

maajabu yako wapi sasa?unajua maana ya maajabu wewe???
 
watu wengine bwana jimboni kwake hai kuna shida ya kila namna lakini yeye kiguu na njia kutafuta sifa kwa walowezi ambao hata kura huwa hawapigi
 
Mh mbowe amefanya kile kilichowashinda wanasisa wengi wa tanzania walio waliowahi kutembelea houston, ktk mkutano uliofanyika mariot hotel watanzania zaidi ya 100 waliweza kuchua Card za chadema, kabla ya mh mbowe mh Sugu alitoa hotuba fupi akiwaomba wananchi waunganishe nguvu kuutoa utawala mbovu wa ccm, Sugu alienda mbali akisema ccm wanawaogopa wana diaspora, chadema wanawahitaji sana Hawa watu, watasaidia sana kujenga uchumi wa nchi yetu
 

Attachments

  • IMAG0178.jpg
    IMAG0178.jpg
    348.9 KB · Views: 1,291
  • IMAG0180.jpg
    IMAG0180.jpg
    176.9 KB · Views: 518
  • IMAG0181.jpg
    IMAG0181.jpg
    182 KB · Views: 512
Hivi hawa jamaa wa diaspora huwa wanapiga kura kweli hawa?
 
Back
Top Bottom