Forever Living imeniachanisha na mke wangu

Forever Living imeniachanisha na mke wangu

yaani wakuu hii kitu inaitwa Forever imeshaua ndoa yangu ila wife hataki kundoka hao forever ni matapeli wamemfilisi bado hajielewi
 
Ila wandugu hawa jamaa siyo wazuri kabisa, kwani ukikutana nao wakaanza kukupa shule utajilaumu kwa nini upo jinsi ulivyo, maana unaona utajiri nje nje, kmesabibisha jamaa yangu wa karibu aache kazi TBL kisa wao!

Sasa inapokuja kwa wenzetu( dadaz) huwa wepesi kushawishika kuingia humo kwa kuina ni kazi rahisi kumbe katika kuitekeleza haina tofauti na umachinga, ofisi kwa ofisi, wateja wakubwa wanaume, na mwanaume hata kama hakupanga kununua ila akishawishiwa tu lazima anunue kwa minajili ya kujitengenezea mazingira ya kupiga mzigo
 
Forever Living Car.jpg
Hii ni Gari aina ya Jeep Grand Cherokee ya Kimarekani yenye thamani ya zaidi ya milioni 90 za Kitanznaia mpya kabisa yaani 0 km iliyonunuliwa na dada Huyu Blandina Njau kama wiki sita zilizopita naye anafanya biashara hii ya Forever Living.

Forever Living House.jpg
Hii ni Nyumba ya Mr and Mrs Mgoyo wakiwa na watoto wao nje ya nyumba yao huko Arusha Tanzania yenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 400 za kitanzania wameijenga kwa fedha wanayolipwa na kampuni ya Forever pia...wamehamia nyumba hii mwaka jana nao wanafanya biashara hii.

Watoto wanapenda asali,watoto hawapendi ukali,watoto wanapenda safari,maisha kufika ni mbali tena kwa msoto mkali.Je na wewe maisha haya unayapenda??siyo uchawi wala utapeli ni ukweli mtupu..kinachotakiwa Kuwa na mtaji wa kianzio wa 800,000(laki nane za kitanzania) ili nawe siku moja ufikie malengo mwakubwa kama hawa watanzania wenye uthubutu.Kama upo tayari na haujafikia ndoto zako tupigie +255784778788 tukuelekeze.

 
Amalinze

Acha kutafuta wateja kijanja wewe bosi weni rick wa rems pale mwalimu house hana hivyo vitu kila mtu auze madawa yenu hayo nani amuuzie mwenzie
 
Last edited by a moderator:
wewe piga kimya jifanye kama haujui chochote...

siku ukichoka na matendo yake mwambie nimekuvumilia vya kutosha....nakupeleka kwenu.
 
Nenda ofisini kwao kawaeleze biashara zao zinavunja mahusiano yako.
 
Acha kulalamika ndugu, hiyo nyumba kaingia mdudu. Fanya maamuzi. Yawe hasi au chanya ila fanya maamuzi.
 
Forever! hili neno! duh watu wanakupa makavu hawatafuni maneno sometime JF raha ila uombe yasikukute
 
Pole sana mkuu.inaonekana kuna jamaa amefanya yake tayari kwa mkeo ndo mana dharau nyingi.piga chini tunza wanao.
 
Mimi kama mwanamke wa kitanzania, na ninayejiita good feminist naona changamoto mbili tu kuhusu dada zangu na kaka zangu wanaozungumzwa hapa

baadhi ya wanawake,tumepata elimu na nafasi na uhuru wa kufanya mambo fulani ambayo mama zetu hawakuyafanya wala wale waliotutangulia....zaidi tukalelewa tukakua tukijua kuwa kuna mfumo dume na kwamba wanaume wamekuwa sehemu ya kutudumaza,kutuonea,kutudharau na kutufanya tuwe nyuma.

(Hili ni complicated kidogo nikitumia mila,misingi ya dini na majukumu ambayo wanawake tumelelewa na kuandaliwa kufanya kwenye familia).
Tumeamua basi sasa basi nasisi tutapigana kama wao,tufanye yale tunayoweza kufanya na wanaume hawakuwa kikwazo....priority hapa ikiwa ni Hela na mafanikio yanayotafsiriwa kwa yale ambayo hela inaweza kutoa.

Kitu nilichojifunza kwangu binafsi kwa wanawake ninaowatazama kwasababu ya mafanikio na heshima waliyojijengea ni kuwa mafanikio,furaha na heshima haviletwi tu na hela....katika vitu vigumu lakini wanawake tunapaswa kujifunza ni ku-balance maisha yetu ya kikazi,kifamilia na kindoa.Binafsi nimejifunza sana kwa Sheryl Sandberg COO wa Facebook na mama yangu ambaye ni mtumishi.

Mafanikio ni nini? kuwa na hela na kulala na wanaume tofauti tofauti,kuwa safarini na kuacha familia yako muda mrefu mikononi mwa watu wengine ukitafuta hela?kumuacha partner wako wa maisha nyumbani amudu majukumu ambayo kimsingi yaliandaliwa kuwa yako),kuwa na kauli za rahisi na nyepesi kama za mafanikio yangu kwanza mengine baadaye wakati ulishaamua kuwa na ndoa?
yabidi kujipanga sana na kuangalia mitazamo gani ya kubeba na ipi siyo ya kubeba.

Kwa wanaume,ukweli ni kuwa maisha yamebadilika. hatutakuwa wanawake ambao mama zetu walikuwa.hata lifestyle tu za sasa hazituruhusu. Ni muhimu kushauriana na mke/mpenzi wako ni kwa namna gani mnaweza kuishi na mapambano ya maisha ambayo sote tunayo na mwisho wa siku kuwe na mafanikio si tu ya kifedha bali pia ya ndoa yenu,watoto wenu,jamii na hata uzee wenu.

Mabadiliko ni magumu sana.kuweni sehemu ya mabadiliko,badala ya vitisho na lawama,tushauriane kwa namna ya kuenenda. ukitishia kumuacha mwanamke ambaye akili yake inaangalia tu kwamba hela ndio kila kitu na pengine alikuoa kwa uwezo wako na sasa anaona uwezekano wa kuwa na zaidi au tayari ana uwezo zaidi ya alivyowahi kuwaza na sio kingine utaumia na wewe na familia pia.

sasa ushauri wangu kwako mi nadhani,usipigishane kelele na mwanamke. Kuwa clear tu,nini unaweza kubaliana nacho na nini huwezi. mpe uhuru wa kuchagua na muda wa kufanya hilo,baada ya hapo waite washauri wenu au hata wazee weka maamuzi yako kama mwanaume na uyasimamie ukiwa umejipanga na majibu hasi na chanya kutegemeana na kile ukitakacho. Forever Living kuna wanawake wanaifanya vizuri na kwa kulinda heshima na ndoa na familia zao,usiichukie.
 
Ndio maisha hayo mpige chini mapema kabla hayajakuja kutokea ya ufosaro.
 
Michelle nimekupenda bure kwa bandiko lako #66 . Laiti wanawake wengi zaidi wangekua na upeo huo... ubarikiwe zaidi
 
Last edited by a moderator:
Michelle nimekupenda bure kwa bandiko lako #66 . Laiti wanawake wengi zaidi wangekua na upeo huo... ubarikiwe zaidi

Amen. Asante sana.

Kuwa na washauri wazuri ni kitu muhimu,watakunyenyekesha unapotaka kutumia hisia,ndoto na matamanio yako kufanya maamuzi magumu,watakusaidia usikosee au wakuache ukosee wakurekebishe mapema kwa kukufundisha. Wanapofanikiwa wajifunze pia kwa waliotangualia kufanikiwa manake wao sio wa kwanza kufanikiwa.
 
Kazi zingine ni kuwaweka wake zenu mitegoni. Hata kama alikua mwadilifu lakini mwanamke ni mdhaifu ni rahisi kushawishika pasipo hata kupenda. Sasa hio forever living kuanza kuzunguka maofisini kwa watu na hata mpaka nyumbani, ndugu kuna jamaa ni smaku eti. Perfume tu anayonukia jamaaa mkeo anahisi yuko switzerland. Anaalikwa lunch ku discuss product kalamanzi.

Sijui unapajua. Lunch ya wawili si chini ya laki. Halafu jamaa hatongozi. Akitoka hapo anachukua mzigo wote anaingia kwa vogue anatambaa. Baada ya siku kadhaa anamwalika tena for lunch na ku discuss possible investments.

Huna kitu hapo tena.Mimi nimepiga marufuku forever, sijui kwenda china na bar. Duka hilo hapo, mzigo china atafwata dada. Hutaki utakaa nyumbani ufuge kuku.
 
Back
Top Bottom