For Teamo and Co: Baadhi ya imani potofu kuhusu uzazi na watoto

Halafu kuna hii nyingine (natanguliza samahani kwa wakereketwa wa mambo ya gender),

Kama unaenda safari, mtu wa kwanza kukutana naye akiwa mwanamke (na hasa hasa vile vibibi) bas safari yote imeinga mikosi.

Kwa wale wenye wake wengi, walikuwa na mmoja ambaye analeta bahati nzuri (hana mkosi. Kwa hiyo endapo mtu anasafiri au anaenda kuwinda, basi siku ya kuamkia safari lazima akalale na yule mke mwenye bahati ili mambo yaende mswano. Wakina Shekh Yahaya wanaendeleza haya mambo kupitia nyota. Kwamba kuna wanaume wanasafiria nyota za wapenzi au waume zao. n.k.....

na pia kuna kamtindo nilishawahi kuona kondakta wa basi moja kabla ya kuondoka anarusha vimawe ndani ya basi nikauliza sababu ni nini nikaambiwa eti kuna wanawake wako kwenye siku zao wataleta mkosi barabarani.....kwa kweli huu ni uonevu
 
na pia kuna kamtindo nilishawahi kuona kondakta wa basi moja kabla ya kuondoka anarusha vimawe ndani ya basi nikauliza sababu ni nini nikaambiwa eti kuna wanawake wako kwenye siku zao wataleta mkosi barabarani.....kwa kweli huu ni uonevu

Hii ngoja tusubiri kuiongeza kwa sababu imekaa vibaya sana. Ila kweli, kuna imani kuwa mwanamke akiwa kwenye period chanzo cha mikosi. Nashani kuna makabila ambayo inabidi hata kutengana kitanda na mume wake. Ngoja tusubiri kwanza wadau watupe maoni yao.
 
preta umenikumbusha nyengine

mwanamke akiwa kwenye siku zake asitengeneze mkate wa mayai .....................hauta 'umuka'. yaani utakuwa bumunda! heheh
 
preta umenikumbusha nyengine

mwanamke akiwa kwenye siku zake asitengeneze mkate wa mayai .....................hauta 'umuka'. yaani utakuwa bumunda! heheh

Hii naiongeza moja kwa moja. Unachungulia lakini orodha yetu inavyokua?

Nitamtafuta jamaa yangu (medical anthropologist) ili aangalie uwezekano wa kuyatafit baadhi ya mambo. Na especially maana yake kwa wigo mpana (broad perspective).
 
hii mikwaraq ilikuwa na malengo yake. nitatoa maelezo machache

Kuna mambo mengi yanayoaminika sana katika jamii zetu na huwapa watu mashaka. Nimejaribu kuweka hii list. Naamini wengine wataongezea.

Kuhusu mambo ya uzazi:
1. Wazazi wakifanya tendo la ndoa mtoto anapata madhara (maziwa yanachacha)

kuepusha wazazi wasimalize chakula cha mtoto hasa kwa wale manjemba ambao hawataweza kujizuia kunyonya
au kukamua matiti wakati wa "sega".

2. Mapacha wa kirukwa wanakufa (endapo mzazi mmoja atafanya ngono nje ya ndoa kabla au baada ya kuzaliwa)

kuzuia watu wasitoke nje ya ndoa, hususan ukuzingatia mkwara umeshwekwa kwenye kucheza "sega" wakati mamsap
anakaribia kujifungua

3. Wazazi wakifanya ngono nje ya ndoa wanambemenda mtoto

kutaka watu watunze maadili ya ndoa

4. Baba akimpiga mtoto kichwani na uume wake mtoto anakufa

kuzuia watu wasilale kitanda kimoja na mtoto. ndio maana wamama wengine uhama chumba
wakati wanalea. si unajua ndotoni katika kujigeuza unaweza shtukia rungu lipo kichwani mwa mtoto?


5. Mama akimlaani mtoto wake kwa kumwonyesha sehemu nyeti anakuwa kichaa

kuzuia laana kutolewa kama njugu (urahisi). wamama wangapi wapo tayari kuvua nguo na kuelekeza
nyeti kwa mtoto wake? hiyo hasira itakuwa balaa. aidha huyo mtoto wa kusubiri mpaka mama yake
amvulie na kumuonyesha nyeti utampata wapi si atakuwa kisha kimbia zake? kama akibaki na kukodoa
macho ujue huyo sio mtoto tena bali ni balaa anaweza hata kumbaka mother wake.

6. Ukitembea na ndugu yako wa damu watoto wanaozaliwa wanakuwa mazezeta

kuepusha ndugu wa damu kujamiiana. hata hivyo naamini pia kuna maelezo ya kisayansi yanayoshauri ndugu
wa damu kuepuka kupata mtoto pamoja.

7. Ukifanya tendo la ndoa na mama mja mzito (karibia na kujifungua) mtoto anazaliwa na uchafu kichwani

wazee hawkuwa watundu sana, hivyo mtindo maalumu ulikuwa "kifo cha mende" sasa unaweza fikiria kwa nini waliweka
mkwara kwenye tendo la ndoa wakati wa ujauzito

dah! mengine wengine wanaweza kujazia. hizo ndo busara za wazee wetu
 
preta umenikumbusha nyengine

mwanamke akiwa kwenye siku zake asitengeneze mkate wa mayai .....................hauta 'umuka'. yaani utakuwa bumunda! heheh

my dear wanawake tunanyanyaswa sana....sijawahi kusikia wanaume wao wana mikosi gani ni wanawake tu.....na hii yote ni wao ndio husema
 
Sasa jamani, utamjuaje?

Hii naona imekuja siku hizi (it is contemporary) kwa sababu huko nyuma hao mashetani hawakuwepo.

nakataa hii mkuu

mashoga wamekuja sambamba na lugha ya kiswahili. Kwa hiyo kwenye maeneo ya pwani mashoga wako tokea zamani japo hawakuwa wakijinadi namna hii tunayoiona sasa.
 
Hii naiongeza moja kwa moja. Unachungulia lakini orodha yetu inavyokua?

Nitamtafuta jamaa yangu (medical anthropologist) ili aangalie uwezekano wa kuyatafit baadhi ya mambo. Na especially maana yake kwa wigo mpana (broad perspective).


hiyo list naiyona inavyorefuka! Maisha yetu yamezungukwa na vitu tusivyojua maana :)
 
Godii,

Umenikuna sana kwa maelezo yako.
kuzuia laana kutolewa kama njugu (urahisi). wamama wangapi wapo tayari kuvua nguo na kuelekeza
nyeti kwa mtoto wake? hiyo hasira itakuwa balaa. aidha huyo mtoto wa kusubiri mpaka mama yake
amvulie na kumuonyesha nyeti utampata wapi si atakuwa kisha kimbia zake? kama akibaki na kukodoa
macho ujue huyo sio mtoto tena bali ni balaa anaweza hata kumbaka mother wake.



kuepusha ndugu wa damu kujamiiana. hata hivyo naamini pia kuna maelezo ya kisayansi yanayoshauri ndugu
wa damu kuepuka kupata mtoto pamoja.

Hilo la kuepusha ndugu wa karibu kuona ni kweli kisayansi kwa sababu kuna kitu kinaitwa inbreeding. Yaani watu ndugu au wanyama kuzaa pamoja. Inasababisha kuendeleza magojwa ya kurithisha lakini pia inapunguza kitu kinaitwa "genetic variability" ambayo huaongeza fitness ya viumbe hai. Hata wanyama wa porini wana strategies za kuzuia inbreeding.
 
my dear wanawake tunanyanyaswa sana....sijawahi kusikia wanaume wao wana mikosi gani ni wanawake tu.....na hii yote ni wao ndio husema

Ni kweli kabisa. Ni jambo la kusikitika kwamba myths nyingi zimekaa kimtego mtego kwa ajili ya kuwakandamiza wanawake. Ila kitu kinachokera, wanawake wenyewe wanakuwa media ya kuzieneza. Nadhani tuendelee kujadili labda hawa vijana wetu akina Teamo and Co wengine wanaweza kuambulia moja au mawili ya kuwafaa. Mfano kama hilo la marufuku wakati wa terminal pregnancy!!!

nakataa hii mkuu

mashoga wamekuja sambamba na lugha ya kiswahili. Kwa hiyo kwenye maeneo ya pwani mashoga wako tokea zamani japo hawakuwa wakijinadi namna hii tunayoiona sasa.

Inawezekana. Wenzio tumekuja pwani juzi juzi tu.
 
mwana mwari haruhusiwi kujitia manukato akanukia au atakumbwa na jini
 
mwana mwari haruhusiwi kujitia manukato akanukia au atakumbwa na jini

Which means what?

Kwamba jini linaweza kuwa "popobawa" au?

Nitaiongeza pia ukinipa ufafanuzi kidogo zaidi.
 
nafikiri ni kutaka tu mtoto wa kike ambae hajaolewa asijipambe sana wala kunukia sana kuepusha kuleta vishawishi huko mitaani.

Ndio wakamtisha kwa kumwambia ukifanya hivyo utapata jini ( na utakosa nafasi za kupata binaadamu mwenzio wa kuishi nae)
 
nafikiri ni kutaka tu mtoto wa kike ambae hajaolewa asijipambe sana wala kunukia sana kuepusha kuleta vishawishi huko mitaani.

Ndio wakamtisha kwa kumwambia ukifanya hivyo utapata jini ( na utakosa nafasi za kupata binaadamu mwenzio wa kuishi nae)


Haaaaaaaaa,

Hapo umenikumbusha. Nilishawahi kusikia yule mjinga Shekh Yahaya akisema kuwa majini yanaoa. Kwa hiyo nimekupata. Ngoja niiongeze kwenye list yetu.
 
Haaaaaaaaa,

Hapo umenikumbusha. Nilishawahi kusikia yule mjinga Shekh Yahaya akisema kuwa majini yanaoa. Kwa hiyo nimekupata. Ngoja niiongeze kwenye list yetu.

Mkuu umesahau kale kadesturi ketu ka kuwafunga watoto kabangi mkononi ili kumlinda na wachawi,naona mijini siku hizi kametoweka.Hivi kale kabangi uondolewa mtoto akifikia umri gani.
 
baadhi ya hizi mila ziko across the whole africa, kama mnakumbuka vizuri kwenye kitabu cha things fall apart cha chinua achebe kile cha enzi zile sio hiki kilichoeditiwa, kuna stori za nwoye na wadogo zake kina ezinma wakikatazwa kupiga uluzi usiku kwani wataita wachawi na pia nyoka usiku alikuwa naitwa uzi /kamba kitu ambacho ni the same huku east africa, so naamini hizi mila zilikuwa zinacut across subsaharan africa yote
 
na pia kuna kamtindo nilishawahi kuona kondakta wa basi moja kabla ya kuondoka anarusha vimawe ndani ya basi nikauliza sababu ni nini nikaambiwa eti kuna wanawake wako kwenye siku zao wataleta mkosi barabarani.....kwa kweli huu ni uonevu

Hii pia mimi nimeiona nilimbamba taxi driver mmoja asubuhi akiokota vijiwe saba na kuvitupa ndani ya buti nilipomuuliza akasema ni kinga huwa wanapakia wanawake wakila aina na vijiwe vilivokuwepo kwenye buti kabla vilitupwa na muosha gari kwahiyo anaweka vingine kabla ya kuanza kazi.
 
Mkuu umesahau kale kadesturi ketu ka kuwafunga watoto kabangi mkononi ili kumlinda na wachawi,naona mijini siku hizi kametoweka.Hivi kale kabangi uondolewa mtoto akifikia umri gani.

na wachawi ndo wanaogopa bangi!
 
Back
Top Bottom