KERO Responded Foleni ya Tunduma mpakani haitatuliwi, kuna Watu wana maslahi Binafsi, inatutesa wengi

KERO Responded Foleni ya Tunduma mpakani haitatuliwi, kuna Watu wana maslahi Binafsi, inatutesa wengi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

DodomaTZ

Senior Member
Joined
May 20, 2022
Posts
161
Reaction score
200
Wazee huku Tunduma ni changamoto kuvuka aisee siku saba foleni haitembei, huu msongamano wa malori katika mpaka wa Tanzania na Zambia upande wa Tunduma ni kero kubwa sana na hali hii inakwamisha Uchumi wa watu wengi na unawafaidisha wachache.

Kuna kiongozi wa masuala ya Usalama (jina ninalihifadhi kwa sasa) amenunua parking anavusha gari zilizolala kwenye parking yake nyie wanyuma hamna kupita mpaka muingie parking yake.


Kibaya zaidi parking yake gharama ya kulipia ni Sh 10,000 kwa siku wakati sehemu ningine zote parking ni Shilingi 5,000, Wazee mbona inakuwa hivi nchi ya wote mbona mifereji ya pesa ni ya wachache?

Hii Dunia ina mwisho hata wakijilimbikizia pesa kama milima hawataondoka nazo, yote kwa yote wanatupa ugumu wa Maisha tu.

Watumishi wamekosa uhadilifu Viongozi wetu wakuu wa nchi wanafanya kazi kubwa lakini Watumishi wasiokuwa waadilifu wanamuangusha mama.

Pia soma:
~
Wadau wadai msongamano wa malori Tunduma unatengenezwa, RC Chongolo aunda kamati kubaini ukweli
~ Foleni ya Tunduma mpakani haitatuliwi, kuna Watu wana maslahi Binafsi, inatutesa wengi
 
Wazee huku Tunduma ni changamoto kuvuka aisee siku saba foleni haitembei, huu msongamano wa malori katika mpaka wa Tanzania na Zambia upande wa Tunduma ni kero kubwa sana na hali hii inakwamisha Uchumi wa watu wengi na unawafaidisha wachache.

Kuna kiongozi wa masuala ya Usalama (jina ninalihifadhi kwa sasa) amenunua parking anavusha gari zilizolala kwenye parking yake nyie wanyuma hamna kupita mpaka muingie parking yake.

Kibaya zaidi parking yake gharama ya kulipia ni Sh elfu 10,000 kwa siku, Wazee mbona inakuwa hivi nchi ya wote mbona mifereji ya pesa ni ya wachache?

Hii Dunia ina mwisho hata wakijilimbikizia pesa kama milima hawataondoka nazo, yote kwa yote wanatupa ugumu wa Maisha tu.

Watumishi wamekosa uhadilifu Viongozi wetu wakuu wa nchi wanafanya kazi kubwa lakini Watumishi wasiokuwa waadilifu wanamuangusha mama.
Wewe unayehifadhi jina, kwa kutumia jina badbia na wewe ni sehemu ya tatizo.
 
Eti "Watumishi wasiokuwa waadilifu wanamuangusha mama."

Nawe ndio yale yale, we sema nchi hii ina mambo ya kisenge, inatosha.. unaanza kuremba remba unadhani ndio foleni itaisha kizembe.

Una kanyota kauchawa.. 🤣😂
 
serikali nashangaa kwanini hawatanui ile barabara wakati ndo lango kuu la mpaka wetu wenye unaingiza mapato mengi.

Yani barabara ya mpaka unaoingiza mapato kwa wingi ila maajabu ni ya njia mbili tu.

maroli yanategemea iyo iyo bajajiji iyo iyo daladala iyo iyo.
 
Tunduma ni balaa, abiria wa kawaida akishuka Mpemba kuitafuta Tunduma ni safari nyingine yenye usumbufu na Kero kubwa ya traffic ya malori…

Barabara ya Tanzam haina tena uwezo wa kuhudumia wingi wa magari….

Tazara cargo freight mpo wapi? Saidieni kuondoa msongamano hapo Tunduma…
 
Back
Top Bottom