Foleni kali sana Ubungo - Kimara

Foleni kali sana Ubungo - Kimara

Swala la bara bara kwa Daslm limetushinda sana sioni kama tatizo litatuliwa karibuni na nilitegemea mikoa inayokua kwa kasi pia wangeweka kipaumbele ni kuwa na bara bara za kutosha na kubwa wao bado wapo kwenye ukarabati tu sioni wakiwaza nje ya hapo..
Kama Mbeya ndio kabisa hawajifunzi
 
Aisee, hii kamba ya leo tarehe 13.08.2025 ni ndefu sio kitoto. Yaani kutoka Ubungo mpaka Kimara umbali wa kilometa 5 tunatumia masaa 2:30. Tatizo nini, ni ujenzi wa barabara au kuna ajali? @Tanroads
Pole mkuu,mimi wakati ule mwanzoni ndio inajengwa hiyo double road na njia za mwendo kasi kipande hicho niliwahi kukaa masaa 4,kilichonipunguzia maumivu enzi zile napiga vyombo nilichepusha gari pembeni nikakaa sehemu mpk saa 6 ndio nikaondoka zangu...
 
Na huo ujenzi hapo Kimara hauishi. Kila siku ndo kwanza wanachimba mashimo. Hopulesi kabisa.

Mwendokasi nadhani lilikuwa wazo zuri japo sikuelewa ni kwa nini tusingeanzisha njia za treni badala ya mabasi. Kila dakika 5 au 10 treni yenye mabehewa 10 hivi inapita na kuzoa kila abiria. Inafika mahali watu hawaoni hata sababu ya kuendesha magari kwenda katikati ya mji.

Lakini kwa vile hakuna tunachoweza kufanya kwa ufanisi hata hizo commuter trains si ajabu tungezitelekeza na kuziharibu kama tulivyofanya kwenye mwendokasi. It is very sad that we can't do shit!
Hata wangeweka train zingeishia kufa kama mwendo kasi tu. Mwanzoni mwendokasi ilipokuwa vizuri watu walikua wanaacha magari yao kimara mwisho pale then wanapanda mwendo kasi, ila kwa sasahivi hilo haliwezekani
 
Aisee, hii kamba ya leo tarehe 13.08.2025 ni ndefu sio kitoto. Yaani kutoka Ubungo mpaka Kimara umbali wa kilometa 5 tunatumia masaa 2:30. Tatizo nini, ni ujenzi wa barabara au kuna ajali? @Tanroads
Kwakweli jana ilikuwa ngumu sana na hata ya kutokea kimara kurudi Ubungo nayo ilikuwa ngumu.
 
Aisee, hii kamba ya leo tarehe 13.08.2025 ni ndefu sio kitoto. Yaani kutoka Ubungo mpaka Kimara umbali wa kilometa 5 tunatumia masaa 2:30. Tatizo nini, ni ujenzi wa barabara au kuna ajali? @Tanroads
Halaf wanashangaa kwanini watu hawaendi Uwanjani; Dar es Salaam ndo mji Mkuu wa hovyo kuliko miji mikuu yote EA
 
Aisee, hii kamba ya leo tarehe 13.08.2025 ni ndefu sio kitoto. Yaani kutoka Ubungo mpaka Kimara umbali wa kilometa 5 tunatumia masaa 2:30. Tatizo nini, ni ujenzi wa barabara au kuna ajali? @Tanroads
Next time nichek , upitie hapa korogwe tule kitimoto na bia
 
Hata wangeweka train zingeishia kufa kama mwendo kasi tu. Mwanzoni mwendokasi ilipokuwa vizuri watu walikua wanaacha magari yao kimara mwisho pale then wanapanda mwendo kasi, ila kwa sasahivi hilo haliwezekani
Management mbovu sana, na hawaamini kabisa kuwa watu kama wewe au mimi tunaweza kuongoza vizuri na kwa ufanisi kabisa hiyo UDART
 
Kama Mbeya ndio kabisa hawajifunzi
Mbeya ni hatari kuliko maeneo mengi sana magari ya Nchi nyingi yanapita pale harafu bara bara ndio ile ya kusubiriana kupita kazi tunayo mlima Mbalizi wa kawaida tu ila eti ni changamoto kuwa na bara bara bora pale..
 
Sijui hata tatizo lilikuwa nini. Asubuhi hii nimetiririka fresh tu kipande hicho kwa dakika 20 tu
Mimi leo nimeamka mapema zaidi maana kuchelewa job nako ni majanga.
 
Tunachoweza ni kuiba kura tu, ili tube mali za umma.
 
Mimi leo nimeamka mapema zaidi maana kuchelewa job nako ni majanga.
Yaani tunalazimishwa kuamka alfajiri sana na kuondoka mjini mapema jioni sana hata saa 8 hivi
 
Aisee, hii kamba ya leo tarehe 13.08.2025 ni ndefu sio kitoto. Yaani kutoka Ubungo mpaka Kimara umbali wa kilometa 5 tunatumia masaa 2:30. Tatizo nini, ni ujenzi wa barabara au kuna ajali? @Tanroads
Jiji hilo limejengwa kizamani sana yani asilimia 80 yawatu wanaelekea katikati ya mji asubuhi na jioni wote wanatoka katikati ya mji kwa staili hii foleni haziwezi kuisha!
 
Back
Top Bottom