Flyover inayofaa Ubungo ni hii hapa

Flyover inayofaa Ubungo ni hii hapa

Vile vituo vya mwendokasi itabidi tuvivunje na tumevijenga juzi tu
 
Mi nadhani kwa sababu rais ni mtaalamu wa haya mambo atajenga tu ila lazima aanze na pale salenda kuelekea coco beach
Nani amekwambia Rais ni mtaalamu wa haya mambo, au kwa sababu amekaa miaka mingi katika wizara ya ujenzi ukadhani ni Engineer? Yeye ni mwalimu wa Chemistry and Maths.
 
Mawazo mazuri sana haya na ingekuwa vizuri wahusika wakayafanyia kazi hasa wakati huu ambapo kuna mipango ya kujenga flyovers.Hongera sana mkuu,haya ndio tunayoyakosa humu JF,zaidi sana matusi ya vijiweni yasiyokuwa na maana wala mwelekeo wa kujenga.
 
Kwa kuongezea tu, tumekua na mazoea kuita ni flyovers, lakini hiyo hapo ni interchange. Flyovers ni simple kuliko interchange. Flyovers zinakua kwenye maeneo simple ambayo kunakua na lengo la kurusha lanes za upande mmoja zipite juu kama cross over au bridge. Lakini kwa Ubungo hapo ni interchange.
 
Huu ndoo ulikuwa kwenye mchakato


pWgFaKW.jpg
Huyu Engineer ina faa afukuzwe kazi!!
Utawekaje Fly over kama tuta la viazi!
Haipambi mji! Wala siyo kivutio!!
Imenyooka tu!! UDSM Product au?
 
Mkuu,

Ngoja nikusaidie kitu muhimu sana katika maisha yako. Kama unataka kuwa Traffic Engineer basi tafadhali kasomee vyuo vikuu na pia uwe na kipaji. Nilisomea hili somo na hasa kwenye kudesign barabara za mwendo kasi.

Hizo barabara zote unazoziona hapo kwenye michoro, hazipo kwa bahati mbaya. Ni kutokana na idadi ya magari yaliyopo siku wana design na kuongeza factor kuwa baada ya miaka kwa mfano 10, idadi itaongezeka na kuwa magari XXX.
Ukishapata idadi ya magari yote yanayopita moja kwa moja, kukata kulia na kukata kushoto hapo ndipo maamuzi ya magari haya yapite wapi yanaanza.

Hili somo kuna watu wa kipaji na hata usome vipi, kama huna kipaji bado unaweza usiwe mzuri. Pamoja na kuwa na kipaji ila badi usomee ili kutumia utaalamu uliousomea na kuuweka kwenye michoro. Wakati mie nasoma, Mkali wa somo hili alikuwa jamaa asiye na Phd ila wenye PhD na hata Maprofesa walikuwa wanakuja kwake kuuliza kama walichokifanya kiko sawa au siyo. Kwa mfano sehemu za taa, aliweza kabisa kuona kwa haraka sana magari yatakavyokutana na hatari ya kuruhusu magari FFF kabla ya magari DDD. Kwa ufupi ni kuwa jamaa alikuwa na kipaji cha kuzaliwa kwenye Traffic Engineering.

Sasa basi tukirudi kwenye Interchange, kwanza huwa kuna Junction za kawaida. Magari yakizidi, kwa mjini unaweza Traffic light na nje ya mji unaweka hiyo round about. Kazi kubwa ya round about (hilo duara) ni kutuliza munkari wa madereva wanaoingia sehemu ya makutano ya barabara. Ni njia rahisi sana kutumia (gharama) ila inakula eneo kubwa. Ndiyo maana inafaa sehemuza pembeni au nje ya mji.

Ubungo ni kama katikati ya mji. Hilo duara litasababisha majengo mengi sana kubomolewa. Ni afadhali kutumia solution nyingine ambazo pia unaweza kuchanganya na taa za barabarani. Faida ya taa za barabarani ni kuwa magari yakishapata green, yanakwenda kasi na kuondoka wakati round about inawataka wapunguze mwendo.

Mfano mzuri wa hizi Interchange ni kama hii hapa. Kama unaona kwenye picha, inachukua eneo dogo sana pembeni ila kuna sehemu imewekwa taa za barabarani. Ogopa sana round about mjini na sehemu za heavy traffic. Ndiyo maana hata pale shule ya uhuru ile round about imeondolewa.

McEwen_01.jpg


KWA MAONI YANGU NADHANI MCHORO HUU UNAFAA UKIJENGWA PALE UBUNGO MATAA , KUMEKUWA NA MICHORO MINGI ISIO ENDANA NA UFINYU WA NAFASI YA PALE UBUNGO NA NI YA GARAMA KUBWA LAKINI HUU KIDOGO UNABANA NAFASI NA NI RAHISI MTU UPANDE WOWOTE KUINGIA NA KUTOKA . NAFIKIRI WENGI WETU MNA JUA ADHA YA KUINGIA UBUNGO TERMINAL UKIWA UMETOKEA MJINI LAKINI KUNGEKUWA NA FLYOVER YA NAMNA HII TUSINGEPATA ADHA YA KUINGIA STAND KUU NA KUELEKEA MJINI,MWENGE NA BUGURUNI NA KIMARA.

ASANTENI.

ANGALIZO .

MSIINGIZE SIASA HILI NI WAZO BINAFSI.

liB3dh9.jpg
 
Magari yanayotoka mjini kuelekea Kimara yatapita chini (mshale wa zambarau )na magari yanayotoka kimara kuelekea ubungo na mjini ya tapita chini(mshale wa njano)


sB9tgWg.jpg
Nzuri sana nimeipenda ila tayari tumeshachelewa huo mradi umeshaanza na uko kwenye maandalizi ya awali ya kuandaa site
 
hivi vitu ni rahisi na vinawezekana na vingeshafanyika miaka mingi tu nyuma,,shida asilimia kumi.. rusha na ubinafsi...kadri tunavokwenda ardhi inapanda na watu wanaongezeka...kama ubungo kwa sasa hapawezekani mpaka fidia itembee sana unles mchoro ubadilishwe ambao utakua gari zaidi
 
Nashukuru mkuu kwa challenge uliyoitoa, nami nakubaliana wewe kuwa eneo lililopo linaweza kuwa dogo kwa huu mchoro. Ahsante


Mkuu, naomba nikuchallenge kidogo...
Ulianza kujua vipimo vya eneo husika ndo ukachora plan au umeanza kuchora kwanza ndo ukaipa jina la mahali?

Na je umefikiria kuhusu ukubwa wa eneo husika?

Kwa haraka inaonekana Songas wahamishe mashine zao zote (200 MW) na upande wa pili Ubungo Main substation ihame....
Bomba la gesi pia linalokatiza hapo?

Gharama ya project?
Vipaumbele?

Mwisho nakupongeza kwa ubunifu mzuri.
 
Flyover inaondoa taa barabarani na njia kuu ya kusaidia kuondoa msongamano barabarani
ingekuwa vyema zaidi kama tungefanya divergence za shughuli zingine miji mingine mfano tu wa delhi na new delhi maana sasa hv kila shughuli ili ikamilike ni lazma twende posta almost
 
Mawazo mazuri sana haya na ingekuwa vizuri wahusika wakayafanyia kazi hasa wakati huu ambapo kuna mipango ya kujenga flyovers.Hongera sana mkuu,haya ndio tunayoyakosa humu JF,zaidi sana matusi ya vijiweni yasiyokuwa na maana wala mwelekeo wa kujenga.
Asante mkuu, na ni kweli naona kuna vitu vinakuwa vya kweli mpaka vinawakosesha raha wakubwa wanaona njia rahisi ni kuwasaka wachangiaji maarufu JF kwa mwendo huu JF watu watakuwa hawachangii sana.
 
Back
Top Bottom