Flight that took off in 2017 landed in 2016

Flight that took off in 2017 landed in 2016

Kutokana na tofauti ya masaa baina ya USA na CHINA,hii ndege ili take off tarehe 1-1-2017 kutoka Shanghai China na kufika San francisco USA tarehe 31-12-2016.View attachment 453618
Non-stop flight kutoka Shanghai kwenda San Francisco ni muda wa saa 11 na dakika 05,wakati Shanghai ipo mbele kwa saa 08 GMT sawa na saa 16 tofauti yake na San Francisco CA.
 
yaani waliondoka kama leo, halafu wakafika jana!
Geographic wonder!
Ndege ilikua inaelekea mbele wakati Kalenda/time ikirudi nyuma!! Wakati wapo angani masaa yalikua yanarudi nyuma badala ya kwenda mbele!!
 
Ndege ilikua inaelekea mbele wakati Kalenda/time ikirudi nyuma!! Wakati wapo angani masaa yalikua yanarudi nyuma badala ya kwenda mbele!!
Mi nilichoelewa ni kwamba, mzunguko wa dunia, una spidi ndogo kuliko ndege, ndiyo maaana ndege iliipita tarehe husika na kufika mahala ambapo siku haijabadilika, bado pana tarwhe ya jana, kwa kule ndege ilikotoka
 
Na watakuwa walifanya makusudi hiyo flight na booking ilifanywa long time before, na mpunga kampuni imepiga kwa tiketi za flight hiyo. Yaani hapo watu walipiga hesabu zao wakaona inawezekana basi wakapanga flight.
Yeah,walifanya kama some sort of "time" adventure!
 
Mi nilichoelewa ni kwamba, mzunguko wa dunia, una spidi ndogo kuliko ndege, ndiyo maaana ndege iliipita tarehe husika na kufika mahala ambapo siku haijabadilika, bado pana tarwhe ya jana, kwa kule ndege ilikotoka
Mkuu kwa hiyo hii inaweza kua uthibitisho kua Dunia inazunguka? Maana kuna watu hua wanapinga kua Dunia haizunguki na sio kweli ni "Spherical" ?
 
masaa 17 + kutoka Dubai hadi Marekani. mwaka gani huo na ilikuwa ndege ya aina gani na jimbo gani ulikwenda. mbona saa nyingi mno.

To proof yourself just Google airlines from Dubai to America takes how long and which lines provide the service.
 
sio sayansi mkuu Kasinde ila ni maajabu ya Mungu,,,, kutenganisha usiku na mchana ni Mungu alifanya na wala has nothing to do with science!......

nataman na mimi nije nioe hicho ulichoshuhudia wewe, looks amazing tho!

Yeah Mungu aliumba hivyo. Siku moja jipe off uzuru ukanda wa Mashariki ya mbali ujionee uumbaji wa Mungu. Utaona utofauti na kukaa mahali pamoja.
 
Kutokana na kuwepo kwa utofauti huo wa masaa hivi hadi Leo bado kuna eneo au nchi ni 2016?
 
Mi nilichoelewa ni kwamba, mzunguko wa dunia, una spidi ndogo kuliko ndege, ndiyo maaana ndege iliipita tarehe husika na kufika mahala ambapo siku haijabadilika, bado pana tarwhe ya jana, kwa kule ndege ilikotoka[/QUOTE

We can't feel Earth's rotation or spin because we're all moving with it, at the same constant speed. Earth spins on its axis once in every 24-hour day. At Earth's equator, the speed of Earth's spin is about 1,000 miles per hour (1,600 kph).
 
Mkuu kwa hiyo hii inaweza kua uthibitisho kua Dunia inazunguka? Maana kuna watu hua wanapinga kua Dunia haizunguki na sio kweli ni "Spherical" ?
inawezekana,
ingawa kwa kigezo hicho tu haitoshi, kwa sababu kuna kitu wanaita mstari wa tarehe, kama dunia inazunguka basi, maana yake ndege iliishinda dunia spidi, na kama jua ndilo linalozunguka vile vile spidi yake ni ndogo kuliko spidi ya hiyo ndege, na ndiyo maana ilifanya overtakeng!
na ili ujue kwamba imeovertake ni huo mstari wa tarehe, ambao kama kinachozunguka ni jua wenyewe upo, na hata kama kinchozunguka ni dunia wenyewe upo vile vile!
 
Kutokana na kuwepo kwa utofauti huo wa masaa hivi hadi Leo bado kuna eneo au nchi ni 2016?

Hapana, nchi zinazochelewa kuingia mwaka mpya ni marekani kule california! Tukiwa tarehe moja mida ya saa tano asubuhi ndo marekani california wanaingia mwaka mpya, kama sio california basi huko alaska ya marekani. Hivyo mpaka leo hamna nchi bado ipo 2016. By midnoon tarehe 1 nchi zote nafikiri zilikuwa 2017. Nchi za mashariki huko japan, uchina ndo huwa za kwanza kuingia mwaka mpya ndo maana hata hiyo flight ilifanikiwa maana ilitoka mwaka unapowahi kuingia kuelekea mwaka inapochelewa kuingia.
 
Pia imeipa umaarufu zaidi hiyo Kampuni ya ndege,ni kama aina fulani ya commercial advertisement,ubunifu mzuri sana,hongera zao,watu wanaona mbali sana aisee!!
Yeah, walikuwa wabunifu sana na waona fursa, hata mie ningekuwa nazo pesa alafu niko huko ningefanya hiyo adventure.
Very interesting!!
 
Mi nilichoelewa ni kwamba, mzunguko wa dunia, una spidi ndogo kuliko ndege, ndiyo maaana ndege iliipita tarehe husika na kufika mahala ambapo siku haijabadilika, bado pana tarwhe ya jana, kwa kule ndege ilikotoka
Daaah, hiyo geography yapi mkuu yani ndege izidi speed ya dunia


hakuna ndege ya abiria inayozidi speed ya dunia inajizungusha kwenye mhimili wake

Na vile vile sidhani kama kuna chombo kimetengenezwa na binadamu ambacho kinazidi speed ya dunia kulizunguka jua ambayo ni zaidi ya kilometa 100,000 kwa saa
 
Back
Top Bottom