Flash Back Memories: Matukio ya Boarding School

Kwenda kuiba ndizi na maparachichi after classes.. Haha...boarding kila Saa unaskia njaa..duka linafunguliwa jmosi tuu..
2.Kuruka dirishani na kuingia lab usiku ili tu kutumia internet...computer yenyewe moja na tulikua watu wanne.

3.Kuagiza chips nje ya shule kwenye matobo ya ukuta...(watu wa vijijini waaminifu unakaa kwenye tobo unaita tu na chips unaletewa.)
Kibosho girls class of 2008
Duuuuuh mlikuwa mna raha kweli kweli
 
I see!!!Class of 2008??!!Kumbe humu tupo na watoto wetu bila kujijua.
Kibosho Girls 2008....A school of my "Step-girl"....Humu tunajadiliana na watoto zetu kabisaaaa...
Hujambo mwanangu lakini?

Hahaha sijambo shkamoo baba
 
na mm kifai modern sec. school class of 2012 nakumbuka nlkuwa naenda kuiba machungwa nyumbani kwa director wa shule! mwenzangu akaenda aiku hyo me sikwenda yeye akang'atwa na nyuki mdomoni!! mdomo ukavimba hatari
 
Hahahaha..hii inanikumbusha ezi za 90s GESECO kuna ticha alikua anaitwa Mahushi noma sana jamaa alikua akiona kisogo tu ameshakumaki kama mlikutana mjin ukamkimbia kesho parade yeye anapita nyuma nyuma kila mstari utasikia anakugusa begani afu anakunong'oneza nimekukamata..hahahaha, Jamaa alikua mnonko hatari,

Kulikua na system ya kutesa manyoya(form one) kunasehemu madogo walikua wanapelekwa humo ndani unakutana na Askari,Mwanasheria na Hakimu hahaha Askari anakukamata,Mwanasheria anakupa taratibu za shule afu Hakimu anakupa hukumu ulete uji kisado kizima kimeungwa na sukari, Crew yenyenguvu yakutisha ilikua inaitwa Nzige yani mtu hata akienda kushtaki Officine amafanyiwa nini ticha akijua huyo jamaa ni wa nzige kesi imeisha, au anakwambia kamuite aje mwenyewe maana yeye mwenyewe anaogopa.
Kuna siku Yule ticha Mnoko Mahushi watu walimvizia yupo officine kwake walika wamekamata nyuki wameweka kwenye mfuko mweusi wakamtupia dirishani afu milango ikafungwa hahaha.

Wanafunzi walikua wamepinda hiyo ilijulikana wilaya nzima kuna siku mkuu wa wilaya alitembelea shuleni akafanya mistake aliacha gari mbele ya shule na Askari akawaambia wabaki kwenye gari kengere ilipopigwa watu wakaenda parade uwanja upo nyuma ya shule wakati anahutubia akachafua hali ya hewa kwa kusema yeye anajiamin yupo vizur ndomaana hata hapo amekuja bila askari ile anamalizia kauli tu jiwe lakwanza likarushwa mara yakaanza kushuka kama mvua maaskari kushtukia mabomu ya machozi yakaanza.

Siku ya Mgomo au Vurugu pakiwa na mpira shule nyingine imekuja wakaanzisha vagi form 1-2 na kazi yao ni kukusanya mawe na kusogeza kwa form 3-4 ndo wanashambulia form 5 walikua wakianzisha wao wanatembeza mkono tu na kuchapa mikanda maana wengi wao walikua wanabeba Nondo
 
shule niliyosoma ilianza 2003 ni ya private mwaka 2004 form two walienda kufanyia necta shule ya jirani kwa kuwa ilikuwa haijasajiliwa mwaka 2005 serikali ikapiga marufuku kufanyia shule ya jirani

Ikatakiwa kusajiliwa shule iko mbali na kijiji siku wanakuja wakaguzi mmiliki akawachelewesha makusudi ili wafike usiku maana shule haikuwa na sifa ya kuwa boarding school
mhasibu wa shule anafika kijijini akawakuta wakaguzi akarudi mbio na baiskeli njiani baiskeli ikaharibika akatupa baiskeli pembeni ya njia akaanza kukimbia kwa miguu akatukuta tupo prepo ilikuwa saa mbili akasema nendeni porini mkajifiche wakaguzi wanakuja kusajili shule inatakiwa isajiliwe kama day school
Tukatoka mbio porini tukaacha daftari darasani mwalimu wa zamu akakusanya daftari zote akaweka ofisini tulikaa porini mpaka saa nane usiku, mhasibu wetu alikuwa na zaidi ya miaka hamsini
 
shule niliyosoma ilianza 2003 ni ya private mwaka 2004 form two walienda kufanyia necta shule ya jirani kwa kuwa ilikuwa haijasajiliwa mwaka 2005 serikali ikapiga marufuku kufanyia shule ya jirani

Ikatakiwa kusajiliwa shule iko mbali na kijiji siku wanakuja wakaguzi mmiliki akawachelewesha makusudi ili wafike usiku maana shule haikuwa na sifa ya kuwa boarding school
mhasibu wa shule anafika kijijini akawakuta wakaguzi akarudi mbio na baiskeli njiani baiskeli ikaharibika akatupa baiskeli pembeni ya njia akaanza kukimbia kwa miguu akatukuta tupo prepo ilikuwa saa mbili akasema nendeni porini mkajifiche wakaguzi wanakuja kusajili shule inatakiwa isajiliwe kama day school
Tukatoka mbio porini tukaacha daftari darasani mwalimu wa zamu akakusanya daftari zote akaweka ofisini tulikaa porini mpaka saa nane usiku, mhasibu wetu alikuwa na zaidi ya miaka hamsini
Daaah hii ya huyu mzee imenigusa, inaelekea alifanya kazi kwa moyo aisee
 
Ilikua kwenye Shule moja huko Moshi
Siku nimechelewa kuamka,kengele ya parade ikalia na mm sikuweza kufika kwa wakati na ukifika kwa kuchelewa ni fimbo za kutosha.

Sasa mimi nikaona njia itakayoniokoa ni kubaki bwenini tu. Sasa pa kujificha ni wapi? Basi,nikajitwika na kutaka kuingia darini! Nilianguka karibia nitenguke kiuno.

Kunyanyuka nikamuona mwalimu wa bweni anakuja. Huyu akikukamata ni hatari sana. Sasa shuleni huruhusiwi kufunga tranka,yote yanaachwa wazi! Nikafikiria fasta,nikachukua tranka moja kubwa na kumwaga vitu Kitandani.
Kisha mwanaume nikajitwika ndani. Nilikua mdogo na nilitoshea. Tatizo hewa sasa,haikua ikitosha. Ticha akafika akaanza kukagua kuanzia uvunguni mpaka darini.

Alipomaliza,akakaa kitandani akaanza kufuta viatu vyake. Kumbe anakanyagia tranka ambalo nipo humo. Alikaa muda mrefu kidogo huku mwenyewe hewa imekua nzito mno na nahema kwa shida. Nikaona hapa Malaika mtoa roho ananichungulia. Nilichofanya nikamuinua mguu na kutoka,aisee alitoka kutoka mbio lakini aliponiona alicheka sana.
Akanipeleka staff,walimu wote walicheka sana mpaka wakashindwa kunichapa. Hahahaha!


KUTUMWA KUPELEKA BARUA KWA DEMU WA Braza.
Kama kawaida,kuwa na mahusiano ya kitoto shuleni. Braza akamuandikia demu barua lakini wanasoma madarasa tofauti. Lile jamaa likaniita likanambia peleka hii barua kwa demu wake. Mimi nikaichukua na kuanza kuipeleka. Ilikua ni usiku muda tunatoka prep. Kumfikishia demu nikamkabidhi alafu nikaanza kumpa maelekezo. Ticha wa zamu huyo katokea. Alinilabua kofi moja hilo sijapata kuliona dunia hii.

KUINGIZWA STAFF NA KUCHAPWA KAMA MBUZI.
Shule yetu ilikua ya Kanisa,kuna kipindi wale wenye mahusiano mnaitwa. Taarifa za uhusiano wenu wanazipata kutoka kwa MaSPY!
Basi,siku hiyo unaitwa na kuambiwa una mahusiano na fulani kisha uwataje wengine ambao unawafahamu wana uhusiano.
Mkishawataja,mnaambiwa kumbatianeni. Kila mtu na mpenzi wake. Walimu wanakaa kila upande,mnachapwa balaa. Mwalimu anakuchapa popote isipokua kichwani. Acha kabisa aisee.




nimecheka hadi machozi yamenitoka!
 
1. Muda wa michezo wenzangu wakiwa viwanjani Mimi nikienda kitaa kula mzigo.
2. Kufungua store ya shule usiku wa manane na kuiba sukari na mchele. Tulikuwa na funguo nyingi sana.
3. Kuiba kuku na Sungura wa mapadri kwakuwa ilikuwa seminari. Na kuwatengeneza supu usiku wa manane.
 
Tulikuwa na HP mmoja mnoko mno, sasa siku moja tukavizia chumbani kwake mida ya class jamaa akanya kitandani kwake sisi wawili tukabaki nje kumuangalizia kama kuna noma. HP alilia vibaya sana siku ile (HP ni wakili mkubwa mjini sasa). Am sure nikimkumbusha hata leo atanikata mbata tu.
 
Back
Top Bottom