Flash Back Memories: Matukio ya Boarding School

Daaaah mie nakumbuka siku ya kwanza tu mshua ananiacha skuli baada ya dk5 naibiwa viatu
Pia nakumbuka ule uji tuliokuwa tukinywa sukari tunaipata kwa hisia tu
Siku ya disco tulikiwa tunaenda kijiji cha jirani kunyoa nywele tunaenda lundo kama mtu hamsini hivi
Wizi wa karanga kwa wanakijiji
Kujisaidia kwenye mashamba ya wanakijiji
Nakumbuka siku moja jamaa yetu mmoja alikamatwa anadigi kwenye shamba la mwanakijiji basi alibebeshwa kinyesi chake mpaka assembly
Nakumbuka miaka ile kuoga ilikuwa ni dhambi
Uniform ni nyeupe lakini baada ya wiki kadhaa zinakuwa km sare za magereza
Weekend kuzama mnadani kunywa gongo huko huko tunakutana na walimu wetu lkn hawakufanyi kitu wanasema ya kaisati muachie kaisari...Lakini kiukweli maisha ya boarding yamenibadilisha sana ktk maswala ya kugangamara
 
1.Mkianza ubishi bwenini ni mpaka asubuhi.
2.Jumapili wali,unakutana na raia wana ndoo ya maji ya lita kumi kama mbili hivi.Moja inawekwa wali na ya pili nyama halafu zinapelekwa chemba wakirudi wanakuta ndoo zote hamna.
3.Siku ikakosewa ikapikwa pilau basi ujue hapo lazima ngumi zitazuka
4.Code za kuitanaa usiku mkiwa mmetoroka kwenda kwa kijiji,codes hizo zilikuwa zinatumika mita kadhaa..ukiita ukisikia kimya hicho sio kikosi chako potea haraka saaana.
5.Wizi wa kuruka kitanda kimoja kimoja.Huo ulikuwa hautabiliki
5.Choo kimoja kinatumika na shule nzima,hapo mgomo wa kuzibua vingine.
6.Unaiba kuku wa walimu then wanafungiwa kwenye ndoo usiku saa nane mapishi yanafanyika.Wanaamshwa wale wafuasi tu.
 
hapo makongo na mm nimesoma aise afande miraji alikua ni shida tupu pia kuna babu chacha naye alikua matata sana aise alikua anapenda kuwabusu wanafunzi wa kike
 
Hahaha,

O' Level.

1. Picha linaanza nimefika form one baada ya kukabidhiwa kitanda tuu, nikaibiwa ndoo niliyokuja nayo. Nikaitafuta nikaikuta bweni jingine, kuichukua ile kuifikiaha tuu na kujipindua nikakuta ndala na ndoo vimeibwa tena. Daah, watu form six waliokuwa wamebaki likizo (maana form one tulikuwa tunawahi wiki kabla kabla wengine hawajafungua shule ili tuzoee mazingira) wakaniambia hayo ndo maisha. Na wewe tafuta wa kumuibia.


2. Kuna siku tulikula panya, panya aliingia katika unga, wakati wanamimina unga katika masufuria ya ugali panya yumooo. Aisee tukagoma na shule ilifungwa.


3. Sisahau kwenda kuchunga ng'ombe kuna ng'ombe tulimtegua mguu ili aumwe achinjwe tule nyama.


4. Kuchanja kuni ilikuwa ni shughuli iliyonikera sana.


5. Kuna siku ulipikwa wali tukapiga addition, tukawa na wali kama mabakuli matatu hivi. Sitosahau ule wali tuliula kwa siku 3. Kazi ilikuwa ni kuuanika juani tuu. Hahahaa. Hatukuumwa wala nini.


5. Kupitisha wiki bila kuoga wala kupiga passport ilikuwa ni kawaida sanaa kwa maisha yale.


6. Kuna siku ilikuwa sherehe ya walimu. Zikapikwa nyama roast, wakateua wanafunzi wabebeb wawapelekee walimu. Raia tulitoroka na hotpot moja lililokuwa full nyama. Ila hatukushtukiwa.


7. Jumatatu ilikuwa ni siku ya kusoma barua zilizpletwa. Mimi ilikuwa sijawahi kutumiwa barua. Nikaona isiwe tabu, nikaenda zangu mjini nikajitumia barua kwa stempu ya kufoji ili na mimi nioshe. Hahahahaaa.


8. Bweni zima kunukia perfume moja siku ya sherehe ilikuwa jambo la kawaida maana unakuta bweni zima mwenye perfume ni mmoja.

9. Kulala na uniform ilikuwa ni jambo la kawaida kwangu.

Advance.
1. Baadhi ya vitu niliacha. Nikaongezea vingine. Utoro wa kwenda mitaani kutafuta vyakula, kuangalia mpira na picha za ngono vibandani.

2. Kuvuta likizo mwezi mzima, na kuwahi kuondoka shule mwezi mzima kabla ya tarehe official kufungwa.

3
 
U Ungeenda kula walikwa mama pendo, au mihogo mwisho wa lami
 
Nakumbuka ile siku ya wali basi ikitokea mmepata wali mwingi inakuwa mazoezi kuumaliza! Tulikuwa tunakula sana and then tunapumzika kwa kuruka ruka huku tukituzunguka pale ndani ili ule wali tuliokula upate kujishindilia vizuri ipatikane space tumboni kabla ya kuanza round ya pili!
 
Ni Unaruhusiwa.. sio Unaluhusiwa
 
Dining kuvaa viatu kwangu ilikuwa ilikuwa ngumu sana
Mihogo maghorofani
Jumanne wali nyama mchana, alhamisi mchana ugali nyama,
Jumamosi wali maharage usiku
Jumapili mchana wali nyama na ndizi au machungwa
Nikapata uongozi form 2, km Dom leader walinipa kwa kunikomoa sababu ya utundu wangu,nikajikuta Dom zima wananipa kura,
Asubuh resprection mitundiko haitakiwi dirishani viatu vipangwe vizuri chini ya kitanda space imedekiwa vizuri
Jumamisi ndo balaa usafi was kufa MTU, ploti imefyekwa, space imedekiwa bado zamu zako za mwezi, nilikuwa siipendi hiyo siku. Sintakaa nisahau kuna, kuna mabint walitoroka walienda Moro hotel ( shimoni) kulikuwa na semina kuna TV moja kwenye habari waliwatoa wale mabint walimu waliwaona SAA 3 tukapigiwa kengere woote rokoo, kucheki wadada hawapo ikawa msala kwa viongozi wooote.
 
Dah! Nimecheka sana
 
Ukiskia madoja sasa mm ndio nilkua rais wao.
Doja la kimataifa kukaa assemble mara moja kwa wiki.
Kuingia darasan mpaka niskie kuna paper.
Coz shule yetu ilkua porin karbu na mpaka wa burund, bac mapind yang yote kwa por huku nikijiburudidha na ndiz pamoja na maparachich na bang kwa mbal.
Kumchapa fimbo kiongoz yoyote mnaa kwa maticha.
Alaf walichokua wanashangaa sasa matokeo yakibandikwa ubaon nmewaburuza.
 
Hahaha Orando katutesa sana.... especially wale tuliokuwa wala flight.. pale ukuta wa salvation army
. Sema nn maisha yalikuwa ka mission ivi kila siku.....
 
Daaah ile tabia ya kuibiana kamba za viatu na soksi asubuhi ilikuwa hatari Hahaha haha...
 
1.tulikuwa tunachukua nyanya na viazi nakwenda kwenye poli la shule nakuni kupika Chui
2.wanafunzi wa boarding kuwaibia wale form one peanut butter siagi dawa ya mswaki pocket money navengine kwenye trucker
3.kwasababu tulikuwa karibu na beach tunatoroka kila time yajioni kwenda kuogelea na kula samaki kama unamkwanja sikuhio
4.kupiga kelele usikuu kisha patron akija nafimbo watu Libya
5.kutege prepo na Rafsanjani
6.kusingizia unaumwa ili uende home
 
hapo makongo na mm nimesoma aise afande miraji alikua ni shida tupu pia kuna babu chacha naye alikua matata sana aise alikua anapenda kuwabusu wanafunzi wa kike
Anawafinyanga finyanga usoni kisha anawabusu ahahahaha....usio akukute sehem sio hyo Babu Chacha utakula fimbo zisizo. NA idadi aisee
 
U
Ungeenda kula walikwa mama pendo, au mihogo mwisho wa lami
Ahahaha Mama P...si mpaka uwe NA hela mkuu? Huko mwisho wa Rami tulikuwa tunaenda tafuta totoz usiku baada ya kula,kuna mshikaji wangu mmoja aliopoa Dada mmoja nyt alipokutana naye kesho yake mchana jamaa kamkimbia demu anasema sio mwenyewe maana mademu wa mwisho wa Lami usiku wanan'gaa ila usiombe ukutane nao mchana utajuta kwann ulilala nae usiku walivyokomaa sura
 
ctasahau cku nlipotoroka bwenin nkaenda kulala geto kwa demu, iltakiwa nrud sa 11 alfajir ila ukatokea ujambaz pale kjijin wakakamatwa wakauawa. wenzangu bwenn wakajua huenda na mm nmeuawa kwa bahat mbaya, hof ikatanda na mimi kwa hof ckutoka nje nkashnda mule geto kutwa nzma had sa6 nkarud bwenn vjana wana hof balaa
 
Mkuu kweli tofauti ipo kwa baadhi ya viumbe, wakati wewe unadoji, wengine tulikua tunabundi. Jamaa angu alikua HP, sasa yeye alikua na ofisi yake. Tukaigeuza ofisi yake kama chimbo la kupigia buku. Yaani tunarudi bwenini kulala saa 9, watu wengine washalala. O level hiyo mkuu. Msuli wake haukua wa kitoto.
 

Kuna jamaa siku ya NECTA form 2 alitoboa akaja kulala saa 11 alfajiri, matokeo yake akaja kuamka saa 5 asubuhi baada ya kelele za tuliotoka kwenye pepa kuanza kusikika mitaa ya bwenini. hahahahaaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…