Duuuuuh mlikuwa mna raha kweli kweliKwenda kuiba ndizi na maparachichi after classes.. Haha...boarding kila Saa unaskia njaa..duka linafunguliwa jmosi tuu..
2.Kuruka dirishani na kuingia lab usiku ili tu kutumia internet...computer yenyewe moja na tulikua watu wanne.
3.Kuagiza chips nje ya shule kwenye matobo ya ukuta...(watu wa vijijini waaminifu unakaa kwenye tobo unaita tu na chips unaletewa.)
Kibosho girls class of 2008
I see!!!Class of 2008??!!Kumbe humu tupo na watoto wetu bila kujijua.
Kibosho Girls 2008....A school of my "Step-girl"....Humu tunajadiliana na watoto zetu kabisaaaa...
Hujambo mwanangu lakini?
Marahabaa Mwanangu....loooh!!Kumbe mwanangu huwa unasoma "upupu" wa mimi mzee wako kule MMU??Loooh...,Hii mitandao hatari sana hiiHahaha sijambo shkamoo baba
kumbe we wa juz tuhehe.. nlikua natoroka usiku kwenda mjini kununua chips mayai sh1500 na kuja kuuza hostel kwa wanafunzi wenzangu kwa sh 2000
nitakua nakujua. Mi nilikua nalala simba bweni alilokua analala JKHaha, Kwanjeka tulikuwa tunaenda usiku siku ya Jumapili
Kucheki "pilau".
nitakua nakujua. Mi nilikua nalala simba bweni alilokua analala JK
2008 A LevelMimi pia nilikuwa nakaa Simba Wingi namba Moja.
Mkuu wewe ulimaliza mwaka gani?
Daaah hii ya huyu mzee imenigusa, inaelekea alifanya kazi kwa moyo aiseeshule niliyosoma ilianza 2003 ni ya private mwaka 2004 form two walienda kufanyia necta shule ya jirani kwa kuwa ilikuwa haijasajiliwa mwaka 2005 serikali ikapiga marufuku kufanyia shule ya jirani
Ikatakiwa kusajiliwa shule iko mbali na kijiji siku wanakuja wakaguzi mmiliki akawachelewesha makusudi ili wafike usiku maana shule haikuwa na sifa ya kuwa boarding school
mhasibu wa shule anafika kijijini akawakuta wakaguzi akarudi mbio na baiskeli njiani baiskeli ikaharibika akatupa baiskeli pembeni ya njia akaanza kukimbia kwa miguu akatukuta tupo prepo ilikuwa saa mbili akasema nendeni porini mkajifiche wakaguzi wanakuja kusajili shule inatakiwa isajiliwe kama day school
Tukatoka mbio porini tukaacha daftari darasani mwalimu wa zamu akakusanya daftari zote akaweka ofisini tulikaa porini mpaka saa nane usiku, mhasibu wetu alikuwa na zaidi ya miaka hamsini
Ilikua kwenye Shule moja huko Moshi
Siku nimechelewa kuamka,kengele ya parade ikalia na mm sikuweza kufika kwa wakati na ukifika kwa kuchelewa ni fimbo za kutosha.
Sasa mimi nikaona njia itakayoniokoa ni kubaki bwenini tu. Sasa pa kujificha ni wapi? Basi,nikajitwika na kutaka kuingia darini! Nilianguka karibia nitenguke kiuno.
Kunyanyuka nikamuona mwalimu wa bweni anakuja. Huyu akikukamata ni hatari sana. Sasa shuleni huruhusiwi kufunga tranka,yote yanaachwa wazi! Nikafikiria fasta,nikachukua tranka moja kubwa na kumwaga vitu Kitandani.
Kisha mwanaume nikajitwika ndani. Nilikua mdogo na nilitoshea. Tatizo hewa sasa,haikua ikitosha. Ticha akafika akaanza kukagua kuanzia uvunguni mpaka darini.
Alipomaliza,akakaa kitandani akaanza kufuta viatu vyake. Kumbe anakanyagia tranka ambalo nipo humo. Alikaa muda mrefu kidogo huku mwenyewe hewa imekua nzito mno na nahema kwa shida. Nikaona hapa Malaika mtoa roho ananichungulia. Nilichofanya nikamuinua mguu na kutoka,aisee alitoka kutoka mbio lakini aliponiona alicheka sana.
Akanipeleka staff,walimu wote walicheka sana mpaka wakashindwa kunichapa. Hahahaha!
KUTUMWA KUPELEKA BARUA KWA DEMU WA Braza.
Kama kawaida,kuwa na mahusiano ya kitoto shuleni. Braza akamuandikia demu barua lakini wanasoma madarasa tofauti. Lile jamaa likaniita likanambia peleka hii barua kwa demu wake. Mimi nikaichukua na kuanza kuipeleka. Ilikua ni usiku muda tunatoka prep. Kumfikishia demu nikamkabidhi alafu nikaanza kumpa maelekezo. Ticha wa zamu huyo katokea. Alinilabua kofi moja hilo sijapata kuliona dunia hii.
KUINGIZWA STAFF NA KUCHAPWA KAMA MBUZI.
Shule yetu ilikua ya Kanisa,kuna kipindi wale wenye mahusiano mnaitwa. Taarifa za uhusiano wenu wanazipata kutoka kwa MaSPY!
Basi,siku hiyo unaitwa na kuambiwa una mahusiano na fulani kisha uwataje wengine ambao unawafahamu wana uhusiano.
Mkishawataja,mnaambiwa kumbatianeni. Kila mtu na mpenzi wake. Walimu wanakaa kila upande,mnachapwa balaa. Mwalimu anakuchapa popote isipokua kichwani. Acha kabisa aisee.
1. Muda wa michezo wenzangu wakiwa viwanjani Mimi nikienda kitaa kula mzigo.
2. Kufungua store ya shule usiku wa manane na kuiba sukari na mchele. Tulikuwa na funguo nyingi sana.
3. Kuiba kuku na Sungura wa mapadri kwakuwa ilikuwa seminari. Na kuwatengeneza supu usiku wa manane.
Mkuu acha kabisa. Ilikua hatari aisee! Kuanzia siku hiyo nilikua naamka asubuhi na mapema sana.nimecheka hadi machozi yamenitoka!