First born msichana theory.........

Kwa kweli sijawahi sikia ila ikiwa kweli itakuwa poa sana maana my no.1 is a girl
 
imani ziko nyingi, kabla sijaoa baba yangu aliniambia 'mke ni baraka'! Kwangu mimi hili limekuwa na ukweli kwa kiasi kikubwa.....lakini obviously haliwezi kuhimili tests za kisayansi! Hili la mtoto kwa kweli sijalisikia.
 
mkuu hizo imani na mimi ndiyo kwanza nakusikia wewe na nahisi mtoto wako wa kwanza ni wa kike
 
Mimi nilishasikia imani hiyo kutoka kwa Bosi wangu, maana na mimi nilianza na mtoto wa kike, nilipoenda ofisini na kumwambia Bosi kuwa nimepata mtoto wa kike, aliniambia kuwa nitakuwa na maendeleo kwa sababu mtoto wa kike ana bahati, sikuamini niliona ananitania maana mimi naamini mtoto ni mtoto tu. Kuhusu uzoefu wangu, mimi naona kuna watu wamenza na watoto wa kike lakni mambo yao sio mazuri, wangine watoto wa kiume mambo super, labda ni imani tu. LAKINI LISEMWALO LIPO...., KAMA HALIPO LAJA.
 
Hii imani ni kweli ipo, mimi nilisikia mwaka 2007 kutoka kwa Bosi wangu, nilienda ofisini na kumpa taarifa kuwa mke wangu amejifungu mtoto wa kike, Bosi akaniambia kuwa nitakuwa na maendeleo kwa sababu mtoto wa kike ana bahati. Sikuamini, nilijua ananitania. Sasa kwa kuwa hapa JF napo kuna watu walishasikia, labda kuna ukweli. LISEMWALO LIPO, KAMA HALIPO LAJA. Watu hawawezi kusema kitu ambacho hakipo, ndio maana hatujawahi kusikia kuwa kuna ngombe anayeruka. Lakini, kuna baadhi ya familia naona zilianza na watoto wa kike, mambo ni mabaya, nyingine zilianza wa madume, lakini mambo super. Hii ndio inasababisha nisiamini nadaharia hii.
 
Jamani nimekutana na watu wengi sana sasa wanaoamini kuwa

familia zinazoanza na first born msichana huwa zinapata bahati au baraka zaidi hasa

kwenye kipato......

Katika mazungumzo na watu....nimekuja kugundua kuwa hii imani ipo kwenye baadhi ya

jamii hasa pwani zanzibar,pemba,na jamii za wahindi pia....

Kuna dokta mmoja aliniambia yeye alipozaliwa mtoto wake wa kwanza msichana

akapata scholarship nje.....

Halafu mkewe akajifungua watoto wakiume watatu na hakusafiri tena

mpaka mkewe alipojifungua msichana tena....

Na wengine wanasema ndoa ikianza na mtoto wa kiume ni ishara ya matatizo

kwenye familia wakati wa kike ni ishara ya neema....

Swali hapa je umewahi kukutana imani hiii???????

Unalionaje hili jambo ukilinganisha na watu unaowajua
wenye watoto wa kwanza wasichana na wenye watoto wa kwanza wavulana???????

ITS TRUE "THE BOSS" ANGALIA MATAJIRI WOTE WAKUBWA PLUS MAFISADI FIRST BORN NI GALS, UKITOKA NJE YA NCHI YETU NDO UTAONA NI KWELI, AKINA BILL GATE, CLINTON, SERENA, PLUS MANY:decision:
 
Kimey, mama wangapi?

Kwa kuwa Mkuu wa Kaya ni Muislam, ni ruksa kuwa na wake tarakimu shufwa, sasa wewe angalia kwa mke mkubwa alitanguli baby wa kike au kiume, halafu utajibu swali lako. Ninyi wa Bagamoyo saida upelelezi huo. Lakini mbona Mkuu wa Kaya mambo yake super, ndio maana akaweza kuwa Presidaa. Sasa inawekana hiyo nadharia, ni nul and void!!!!
 
ITS TRUE "THE BOSS" ANGALIA MATAJIRI WOTE WAKUBWA PLUS MAFISADI FIRST BORN NI GALS, UKITOKA NJE YA NCHI YETU NDO UTAONA NI KWELI, AKINA BILL GATE, CLINTON, SERENA, PLUS MANY:decision:

Huenda kuna ukweli, Baraka Obama wale watoto wawili wote ni wa kike!!!!
 
Hapa naona kuna conflict of interest. Wenye 1st born wa kike wanasema ni kweli and vice versa.
 
Back
Top Bottom