Fingerprint huisha muda wake?

Fingerprint huisha muda wake?

Mbwembwe nyingi halafu unashindwa kuelezea kikamilifu , kwa maelezo yako fingerprint zina expire !!
Kiuhalisia finger print ni forever. Or else criminals wangukuwa kwenye safe zone baada ya records ku expire
ndio watu tuliokocna bongo mkuu. huruma sana
 
Data zinahifadhiwa kidigitali, hivyo hazifutiki. Ni kama picha, video na taarifa nyengine za Digitali.
Ahsante chief mkwawa, manake mfano Mtu aliyejisajili Nida kwa mfumo wa vidole. akienda ku renew I'd yake after ten years akiweka Vidole jina lake lita appear kwenye System?
 
Alama za videlo hazina expire date kwenye mfumo labda zifutwe au mfumo uharibike beyond repair
Sababu ya ku renew ni mabadiliko ya details, sura nk

Si sahihi sana kusema alama za vidole ni kwa ajili ya ku track criminals(ingawaje inarahisisha sana zoezi hilo)......... itoshe tu kusema alama za vidole ni utambulisho bora wa mtu katika karne hii ikiwemo na DNA pamoja na Dental formula

Siku hizi maofisini una sign in and out kwa alama za vidole
Huko mbeleni tutaacha kabisa kutumia cards, itakua ni mwendo wa alama za vidole tu
Yes mkuu umejibu vema,hapo juu wengi wamejibia kuonyesha ni kiasi gani middle class wetu ni shida,finger prints hazina expired date, na zinatakiwa ziwe ndani ya systems ya nchi na sio kwa uhalifu tu kuna faida nyingi mno,ndio maana wenzetu kuomba passport unatakiwa uwe na ID tu,finger prints pia zinasaidia utambuzi na sasa ukienda bank inabidi utumie kidole chako ili account informations zako zitokee kwenye screen ,ID wakuu hii ni LIFE BOOK ,inatakiwa uzaliwe nayo na kufa nayo, haina ukomo, why zetu zina ukomo...ni matokeo ya kuishi in a pithole country
 
Ahsante chief mkwawa, manake mfano Mtu aliyejisajili Nida kwa mfumo wa vidole. akienda ku renew I'd yake after ten years akiweka Vidole jina lake lita appear kwenye System?
Ndio mkuu kama data zilihifadhiwa vizuri litatokea
 
Sifa ya database ni kutunza kumbukumbu kulingana na zilivyohifadhiwa, kwa mantiki hiyo alama za vidole zilizohifadhiwa katika mfumo haziwezi futika labda itokee mfumo umeleta hitilafu, kuna uvamizi wa kimtandao ulioharibu data, kuharibika kwa storage system beyond repair n.k

Alama za vidole zilizo katika vidole vya kila mmoja wetu nazo huwa hazibadiliki isipokuwa kuwe na external factor, mfano mtu anayetumia sana mikono pasipo kufunika ncha ya vidole vyake kuna muda hupoteza patterns za fingerprints, lakini kwa puwa ngozi huwa inajirekebisha basi alama hizo hurudia hali yake baada ya muda...

Kwa mtu ambaye ameungua vidole, kapata matatizo ya kiafya yenye kuharibu ngozi n.k, mtu huyu anaweza kupoteza kwa kiasi kikubwa alama za vidole vyake...
 
Back
Top Bottom