Fikra Pevu: Lowassa alipwa mamilioni na Wasomali

Tina

JF-Expert Member
Jul 9, 2007
572
579
WAZIRI Mkuu aliyejiuzulu kwa kutajwa katika kashfa ya mdadi wa umeme uliohusisha kampuni tata ya Richmond Development LLC, Edward Lowassa, amelipwa mamilioni ya fedha na wafanyabiashara wa Kisomali, Fikra Pevu imethibitisha.

Uchunguzi wa muda mrefu wa Fikra Pevu umeonyesha kwamba Wasomali hao kupitia kampuni ya Integrated Properties Investment (T) Limited walimlipa Lowassa Sh milioni 450 kupitia kampuni yake ya Barare Limited. Malipo hayo yalielezwa kuwa ni deni ambalo Lowassa kupitia Barare alikua akiidai kampuni hiyo ya Integrated ambayo kwa Tanzania imekuwa ikijihusisha na uwekezaji katika majengo.

Uchunguzi wa Fikra Pevu umethibitisha kwamba malipo hayo yalifanyika miezi michache kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2010, na Lowassa na mkewe Regina Mumba Lowassa, walikubali malipo hayo kwa kupewa hisa 7,500 zikiwa na thamani ya Sh 60,000 kwa hisa moja.

Kwa nyaraka na habari zaidi: http://www.fikrapevu.com/habari/wasomali-wamlipa-lowassa-milioni-450-2
 
Wale waliokuwa na maswali kuhusu nguvu yake ya hela wasome hati ya malipo kwenye hiyo attachment...kweli kukosekana kwa ajira ni bomu linalotarajiwa kulipuka wakati wowote.....hivi wanajua kweli tunavyoumia kwa kukosa hata hela ya panadol wakati mwingine??
 
bila shaka hii pesa itatumika kuwapa watu bahasha za kaki..watu gani? kuna uzi umeanzishwa na Lunyungu unaeleza kuhusu hawa wapokea bahasha za kaki..
 
Tina na Wana JF,

Duh kwa mwendo huu, tunatakiwa kusema, Mimi sina hela, pesa, mapene na sio Sisi, Watanzania hatuna pesa, hela, mapene.

Nawasilisha
 
And this is the guy tunaaminiswhwa will be the best president ever? Subirini mtasikia mashabikiwake wakiuliza kwani kuna tatizo gani na hilo la kuwa na share. Hoja will be twisted kwa mtindo ule ule two wrongs can make a right na pia nje ya hoja kwamba mwandishi amebagua wasomali.............. stay tuned!
 
kwa mtindo huu tusipotenganisha siasa na biashara basi maisha bora kwa kila mtanzania yatabaki kuwa stori milele
 
wasomali-lowassa.jpg

From Fikra pevu
 
Dhambi iko wapi? Kwani ni makosa kuwa na kampuni ya kukutengenezea pesa za ziada? Naona wengi bado wanaishi Tanzania ya Nyerere.

Unatafuta ilipo dhambi hapo eeh!! subiri iwe too late upate ushahidi !!!!!!!!!!
 
Dhambi iko wapi? Kwani ni makosa kuwa na kampuni ya kukutengenezea pesa za ziada? Naona wengi bado wanaishi Tanzania ya Nyerere.

Spot on. Azimio la Arusha mlilivunja wenyewe mkawaruhusu viongozi kuwa na biashara zao. Sasa cha ajabu ni nini hapo? Kuna viongozi wangapi ambao ni wafanyabiashara? Tafuteni sababu nyingine ya kumchafua EL.
 
Dhambi iko wapi? Kwani ni makosa kuwa na kampuni ya kukutengenezea pesa za ziada? Naona wengi bado wanaishi Tanzania ya Nyerere.

Ibara ya 17 Katiba ya CCM ya mwaka 1977 iliyochakachuliwa mwaka kwa mara ya mwisho mwaka 2007 inasema hivi kuhusu kiongozi.

Pamoja na kutimiza masharti ya uananchama kama yalivyoelezwa katika Katiba. Kiongozi sharti pia awe na sifa sifuatazo:-
  1. Awe ni mtu aliyetosheka na asiwe mtu aliyetawaliwa na tamaa
  2. .........
  3. ......
Wanachojadili watu hapa ni tamaa aliyonayo huyu waziri mkuu mjiuzulu.
 
Jamani i don't see any problem there, kama kuna mtu kaona anionyeshe nini tatizo.
 
WAZIRI Mkuu aliyejiuzulu kwa kutajwa katika kashfa ya mdadi wa umeme uliohusisha kampuni tata ya Richmond Development LLC, Edward Lowassa, amelipwa mamilioni ya fedha na wafanyabiashara wa Kisomali, Fikra Pevu imethibitisha.

Uchunguzi wa muda mrefu wa Fikra Pevu umeonyesha kwamba Wasomali hao kupitia kampuni ya Integrated Properties Investment (T) Limited walimlipa Lowassa Sh milioni 450 kupitia kampuni yake ya Barare Limited. Malipo hayo yalielezwa kuwa ni deni ambalo Lowassa kupitia Barare alikua akiidai kampuni hiyo ya Integrated ambayo kwa Tanzania imekuwa ikijihusisha na uwekezaji katika majengo.

Uchunguzi wa Fikra Pevu umethibitisha kwamba malipo hayo yalifanyika miezi michache kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2010, na Lowassa na mkewe Regina Mumba Lowassa, walikubali malipo hayo kwa kupewa hisa 7,500 zikiwa na thamani ya Sh 60,000 kwa hisa moja.

Kwa nyaraka na habari zaidi: Wasomali wamlipa Lowassa milioni 450, wampa hisa | Fikra Pevu | Kisima cha busara!

Hivi kuna biashara gani ambayo mnadhani Lowassa hafanyi?kwa taarifa yenu mpaka hizi issue za uharamia kwenye pwani ya somalia jamaa ana mkono kwa kushirikiana na hao hao maswahiba wake wa kisomali,nyie hii ndio mnaijua leo,mbona hii cha mtoto..
 
Ukiona mtu anaanza matusi ujuwe hana hoja. Ngoja tu report haya matusi, nyie ndio mnayoiharibu JF.

Utumiage akili, najua unazo nyingi, usitukwaze kwa maksudi, we una poa tukiibiwa na lowasa kupitia madaraka yake kwa utumishi wa uma!
 
Tamaa haimaanishi usifunguwe kampuni. Mbona Mbqowe ni kiongozi aw upinzani bungeni na ana makampuni na miradi kedekede, hatujasikia hata siku mkimsema humu. Hata alipowauzia mafuso used kwa bei Saidi ya mapya mlikaa kimya.

Ondoa neno MBONA, jenga hoja inayojitosheleza yenyewe.
 
nadhani nimeelewa nilicho kisoma.Nadhani hakuna ubaya mtu au kampuni kulipya fedha yoyote ile ili mradi iwe ni malipo halali kwa kazi au huduma halali.

AZIMIO LA ZANZIBAR LINA WARUHUSU WATANZANIA KUWA WAKURUGENZI WA MAKAMPUNI,maana yake ni kwamba watatengeneza faida na watapata fedha nyingi provided wako makini ktk investment zao.

KINACHOTAKIWA KUCHUNGUZWA NIKUONA HAYA MALIPO YANATOKANA NA KAZI HALALI??????UKIMCHUKIA MTANZANIA KWASABABU TU ANA FEDHA NYINGI NI DHAMBI.

TO ME I THINK THREAD HII INAHITAJI KUFANYA UCHUNGZI ZAIDI ILI KUONA NI MALIPO HALALI KWA KAZI AU HUDUMA HALALI.
 
[h=3]Hii ina uhusiano wowote na hii?

Taarifa ya Lowassa kuchunguzwa balaa[/h]
-Raia Mwema lapata msukosuko
-Nakala 10,000 zaharibiwa zisisomwe

HABARI iliyoihusisha familia ya Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, imeibua utata mkubwa baada ya kuibuka kwa vitisho vilivyosababisha kuzuiwa kuchapwa kwa gazeti la Raia Mwema toleo lililopita Namba 161 katika mazingira ya kutatanisha; huku habari hiyo ikikanushwa kwenye gazeti jingine hata kabla haijatoka.

Utata huo ulisababisha uongozi wa Imprint iliyopo chini ya kampuni ya Jamana Printers kusitisha ghafla kuendelea kuchapwa kwa gazeti la Raia Mwema ikiwa tayari limeshachapwa nakala 10,000 katika mazingira yaliyoonyesha kuwapo shinikizo zito kutoka kwa kigogo mmoja aliye karibu na mwanasiasa huyo la kutaka habari inayomhusu Lowassa iondolewe ndipo gazeti lichapwe.

Raia Mwema ambalo lina makubaliano maalumu na wachapaji hao lilishtushwa na uamuzi huo wa ghafla wa wachapaji hao hasa baada ya uamuzi huo kuambatana na hali ya woga mkubwa uliotawala wafanyakazi wa kiwanda hicho usiku wa Jumanne ya wiki iliyopita.

Taarifa ya Meneja Usambazaji wa Raia Mwema, Omari Mwendapole, ambaye alikuwapo usiku huo, inaeleza kwamba hali ya uchapaji iliendelea katika hali ya kawaida kuanzia saa 11 jioni kabla ya kubadilika ghafla saa 1:30 usiku, ilipotolewa amri ya kusitisha uchapaji wakati zikiwa zimekwishachapwa nakala 10,000.

"Tulifika kiwandani mapema saa 11:00 na hakukua tatizo lolote baada ya wahusika kukagua gazeti letu na kuridhika nalo na wakaanza taratibu zote ikiwa ni pamoja na kuchoma plate saa 11:15 na saa 12:00 kazi ya uchapaji ilianza taratibu hadi saa 12:30 mashine zilipoanza kuchanganya na kutoa gazeti zuri.

"Lakini baada ya muda kidogo, msimamizi wa uchapaji wa Imprint akaitwa na mlinzi kwenda kusikiliza simu na aliporejea akawaagiza mafundi wazime mashine kabla ya kuamua kuzima mwenyewe baada ya kuona wanachelewa kufanya hivyo.

"Baadaye niliitwa kwa bosi wao na kuambiwa natakiwa kwenda kwa Meneja Mkuu, aitwaye Shaber, ambako nilijulishwa kwamba ni lazima habari kuu (inayomhusu Lowassa) iondolewe vinginevyo gazeti halitochapwa kabisa," anasema Mwendapole.

Kutokana na amri hiyo ya wachapaji, wafanyakazi wote wa Raia Mwema na watu wengine wote waliokuwamo kiwandani wakati huo waliamriwa kutoka eneo la uchapaji na kupekuliwa kuhakikisha hawabebi hata nakala moja ya gazeti hilo.

Habari zinasema kuwa nakala 10,000 ambazo tayari zilishachapwa ziliharibiwa chini ya uangalizi mkali wa maofisa wa kiwanda hicho ili kuhakikisha kuwa haziingii kwenye soko, na hivyo habari hiyo kusomwa na wananchi.

Hata hivyo, wakati uongozi wa Raia Mwema ukihangaika kutafuta mahali pengine pa kuchapa, ilibainika kwamba kigogo huyo pamoja na mbunge mmoja walikuwa tayari na nakala ya gazeti hilo na ilidhihirika siku iliyofuata baada ya gazeti la Mtanzania lenye uhusiano wa karibu na kigogo huyo kuchapisha habari iliyokanusha habari hizo kabla hata ya habari husika kuchapishwa.

Katika habari hiyo, gazeti hilo lilielezea kwamba kuna taarifa "zilizochapwa katika magazeti" huku zikimnukuu Frederick Lowassa, ambaye ndiye aliyekuwa mhusika mkuu katika habari ya Raia Mwema, akijitetea kwa kudai kwamba hakuwahi kusafirisha fedha nyingine Uingereza kama ilivyoandikwa na ‘magazeti hayo.'

Katika tukio hilo la aina yake katika tasnia ya habari, Frederick Lowassa, alisema;

"Jamani mimi nashangaa sana. Watu hawa wanasahau kuwa mimi ni mfanyabiashara kwa zaidi ya miaka kumi sasa. Na katika kufanya biashara ni lazima nisafirishe fedha nje ya nchi kwa nia ya kununua material (bidhaa). Nasafirisha fedha sehemu mbalimbali duniani, na sijui wameliokota wapi hilo.

"Hakuna wakati nimewahi kusafirisha paundi 495,000 nje ya nchi kwa mara moja, ila nasafirisha fedha nje ya nchi kununua bidhaa mara nyingi tu. Hili wanalozungumza la Uingereza ni kweli kati ya Machi na Aprili nilisafirisha kama Paundi chini ya 200,000 hivi, kwa ajili ya biashara kama kawaida. Benki kama kawaida walijiridhisha fedha hizo zilikotoka, tukawasiliana likaisha.

"Sasa nashangaa watu hawa hili wamelitoa wapi? Na ifahamike kuwa mimi nafanya biashara nyingi tu, na moja ya biashara zangu ni kampuni ya Alphatel. Sisi ni mawakala wa Vodacom. Tunover (mzunguko wa fedha) yetu kwa mwezi ni zaidi ya Sh bilioni 8.0. Hizi ni fedha zinazotumiwa kama sehemu ya mtaji na faida kwa kununua bidhaa na kuuza. Sasa walitarajia mfanyabiashara kama mimi nishindwe kutumia kiasi hicho nje ya nchi? Nanunua vitu kutoka Uingereza, China, Falme za Kiarabu (Dubai), Afrika Kusini, Italia na sehemu nyingine. Watu wa ajabu kweli hawa.

"Nasikitika jinsi wanavyoendelea kumchafua mzee wangu. Na ndio maana nimeelewa barua hiyo ya mwaka jana imeletwa leo wiki hii. Tayari nimewasiliana na mwanasheria wangu katika hili na nitatoa vielelezo vyote, hakuna cha kuficha…. Jamani siasa zao wazibakize huko, kazi waliyofanya kumchafua mzee wangu (Lowassa) hawajaridhika kweli? Katika hili nasema hapana."

Habari hiyo ilifuatiwa na habari nyingine ambayo iliyomnukuu Lowassa mwenyewe akionyesha kwamba Lowassa anaandamwa na katika toleo hilo aligusia tena kuhusu mwanae Fredrick kuchukua hatua za kisheria kuhuhusiana na habari inayohusiana na usafirishaji fedha Uingereza. Habari hiyo imenukuliwa tena katika gazeti lingine jana.

Uongozi wa Raia Mwema tayari umeiandikia barua kampuni hiyo ya uchapaji ukilalamikia tukio hilo la kuzuia gazeti lisichapwe na kuharibu nakala ambazo tayari zilishachapwa, na pia kutoa usiku huo huo baadhi ya nakala za toleo hilo kwa watu wa nje bila idhini ya wamiliki wa gazeti. Pia unataka ulipwe fidia kwa hasara iliyopatikana kwani ililazimu gazeti kuchapwa kwingineko alfajiri, na hivyo kuchelewa kuingia sokoni.

Katika habari yake ya wiki iliyopita iliyoibua mambo yote hayo, Raia Mwema liliripoti kwamba Frederick Lowassa anachunguzwa na Kitengo Maalumu cha Polisi wa Kimataifa wa Uingereza wanaofuatilia utata wa uhamishaji fedha kutoka Tanzania.

Fedha hizo zinahusishwa na ununuzi wa nyumba yenye thamani ya pauni za Uingereza 475,000 (takriban Shilingi bilioni moja) katikati ya Jiji la London.

Hata hivyo, watu walio karibu na Frederick wameelezea kwamba kijana huyo hakuwahi kununua nyumba; bali aliwahi kutaka kupanga kwa ajili ya kuishi akiwa masomoni nchini Uingereza na fedha nyingine alizituma kwa ndugu yake aishie nchini humo.

Nyumba ambayo inatajwa katika maelezo ya awali iko mtaa wa Leinster Gardens, jijini London.

Hata hivyo, hakuna ofisa yeyote wa Serikali ya Tanzania aliyekuwa tayari kuzungumzia suala hilo, pamoja na kuwapo taarifa kwamba tayari vyombo vya dola vya Tanzania vimekwisha kuhusishwa katika uchunguzi huo.

Maofisa wa Polisi wa Idara ya Upelelezi wa Jinai (CID) wanaohusika na uchunguzi wa fedha haramu, wamekwepa kuzungumzia suala hilo na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Robert Manumba, hakuweza kupatikana, na alielezwa kuwa nje ya nchi kikazi.

Ofisa wa CID aliyeelezwa kuongoza kitengo kinachochunguza makosa ya uhalifu wa fedha na nyaraka, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Samson Kasala, alikanusha kufahamu chochote kuhusiana na suala hilo, kabla ya kukata simu alipohojiwa na Raia Mwema kuhusu taarifa hizo.

Taarifa zinaeleza kwamba Kitengo cha Ufuatiliaji wa Fedha Haramu (Financial Intelligence Unit-FIU) kilichopo chini ya Wizara ya Fedha nchini, kilipokea taarifa kutoka Polisi wa Kimataifa wa London, Uingereza, wakitaka taarifa muhimu kuhusiana na Frederick, kabla ya kitengo hicho kuomba msaada wa polisi.

Hata hivyo, Kamishna wa FIU, Herman Kessy, hakutoa ushirikiano na Raia Mwema, kuhusiana na sakata hilo.

FIU imeanzishwa chini ya Sheria ya Udhibiti wa Fedha Haramu ya mwaka 2006 (Anti-Money Laundering Act-2006) kwa kuundiwa kanuni mwaka 2007, lakini hadi sasa kitengo hicho kimekuwa kikiendeshwa na maofisa watano tu, Kamishna Kessy, mchambuzi mmoja, mtaalamu wa mawasiliano na wasaidizi wawili wasio wataalamu, kitengo kilichopaswa kuendeshwa na watu wengi zaidi kutokana na unyeti wake.

Habari zinaeleza kwamba hata ofisa wa Polisi aliyewahi kuhamishiwa FIU kwa kazi maalumu alijikuta akitengwa na kutopangiwa kazi na maofisa hao ambao wengi wanatoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), baada ya kuwa ‘wameaminiwa' sana na uongozi wa juu wa serikali.

Kwa mujibu wa taarifa hizo ambazo bado zinafanyiwa kazi, Frederick ambaye baba yake alijiuzulu Waziri Mkuu kwa kuhusishwa na kashfa ya ununuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme iliyokabidhiwa kwa kampuni tata ya Richmond Development LLC, anadaiwa kufanya mawasiliano kupitia kampuni ya uwakala iliyotajwa kwa jina la ‘Mishcon'.

Nyaraka alizowasilisha, zilidai kuwapo ubia kati ya mtuhumiwa huyo na kampuni tatu ikiwamo Integrated Property Investment(T) Ltd na Barare Ltd Company.

Mkataba huo unaonyesha kuwa Frederick Lowassa ana hisa kwenye kampuni hizo, na kwamba fedha za ununuzi wa nyumba hizo zinatokana na fedha za malipo ya hisa anazopata kutokana na kampuni hizo.

Hata hivyo, mkataba huo unaonyesha kusainiwa Machi 25 mwaka 2009 siku moja baada ya Frederick Lowassa kusaini mkataba kati yake na kampuni ya Mishcon kama wakala wake katika ununuzi wa jengo hilo.

Pia aliwasilisha nyaraka zinazoihusisha kampuni ya Alphatel kama moja ya kampuni ambayo pia yeye ni mkurugenzi wake ambayo pia ni chanzo chake kingine cha fedha anazotumia kununua jengo hilo.

Taarifa zimedokeza kuwa ununuzi huo ulikwama baada ya kushindwa kutoa malipo hayo kwa mujibu wa mkataba kati yake na wakala wa ununuzi wa nyumba hiyo (kampuni ya Mishcon) ambao ulimtaka awe amekamilisha kulipa fedha hizo kabla ya Aprili 14, mwaka 2009.

Hata hivyo, siku chache baadaye ndani ya mwezi huo wa Aprili, Frederick aliipelekea Mishcon kiasi cha pauni za Uingereza 199,940 zikitokea kwenye kampuni ya ununuzi fedha ya Wall Street Exchange.

Aidha kiasi cha pauni 100,000 kiliingizwa kwenye akaunti ya kampuni hiyo hiyo ya Mishcon kwa fedha taslimu katika mikupuo 12 tofauti zikitokea kwenye matawi tofauti ya benki ya NatWest Bank plc iliyoko Kaskazini mwa Jiji la London.

Raia Mwema limeelezwa kuwa mazingira ya kuingizwa fedha hizo kwenye akaunti ya wakala huyo ( Mishcon) ndiyo yameifanya Taasisi ya SCD 6 Economics and Specialist Proceeds of Corruption Unit ya Uingereza inayosimamia uchunguzi wa sakata hilo kuwa na mashaka makubwa kuhusu uhalali wa fedha hizo.

Kutokana na mazingira hayo, SCD 6 Economic and Specialist Crime Proceeds of Corruption Unit yenye ofisi zake Victoria Block, New Scotland Yard, London, ililazimika kuwasiliana na FIU ikitaka maelezo ya awali kuwezesha kufanyika kwa uchunguzi kuhusu fedha hizo.

Raia Mwema iliwasiliana na Fred ambaye alikana kununua nyumba Uingereza lakini alikiri kuwahi kutuma fedha huko. Aliliambia Raia Mwema pia kwamba hajawahi kuhojiwa na yeyote kuhusu suala hilo, na pia kwamba hana taarifa kuwa polisi wa Uingereza wanampeleleza.

Hata hivyo kwa upande mwingine, gazeti hili limebaini kuwa, maelezo ya awali ambayo yalitakiwa kutoka Tanzania na makachero hao wa Uingereza, ni pamoja na kutaka kufahamu kama kweli Frederick Edward Lowassa amezaliwa Agosti 26, 1977, Mwanza Tanzania na anamiliki hati ya kusafiria yenye namba AB 109402 iliyotolewa Tanzania na kwamba anwani yake nchini Uingereza ni 71 Hendrix Drive, Milton Keynes, MK8 0DY.

Pia makachero hao waliitaka Serikali ya Tanzania kutoa ufafanuzi wakitaka kujua kama Frederick Lowassa ni mbia katika kampuni za Alphatel Partnership (Tanzania) Barare Ltd na Intergrated Tanzania Limited, kampuni ambazo zimefahamika kumilikiwa na familia ya Lowassa.

Asasi hiyo ya Uingereza pia imeomba kujua kama FIU wana taarifa zozote za uhalifu dhidi ya Frederick Lowassa na kama baba yake Edward Lowassa anachunguzwa kwa tuhuma yoyote ya rushwa na mamlaka za uchunguzi wa rushwa nchini Tanzania kuhusu fedha haramu.

Uchunguzi wa awali uliofanywa na vyombo vya dola, ulielezwa na taarifa hizo kwamba Frederick Lowassa si mbia katika kampuni hizo na kwamba Barare Ltd wenye hisa ni Edward Ngoyai Lowassa mwenye hisa 500 na Regina Mumba Lowassa mwenye hisa 500 huku wakurugenzi wakiwa ni hao hao.

Ofisa wa Uingereza anayesimamia uchunguzi huo, George Simpson, ameliambia Raia Mwema kupitia barua pepe kwamba kanuni za uchunguzi kuhusiana na kesi zenye mguso wa kisiasa huwazuia kukanusha au kuthibitisha kuhusu uchunguzi unaoendelea hadi pale wanapofikia hatua ya kukamata mtuhumiwa ama anapofikishwa mahakamani.

Taarifa ambazo gazeti hili limezipata mwanzoni mwa wiki hii kutoka vyanzo vyake zinasema kwamba uchunguzi wa suala hilo bado unaendelea, na kwamba watendaji wamepewa maelekezo ya kuendelea nao.

Rudisha Rasilimali kwa Wananchi: Taarifa ya Lowassa kuchunguzwa balaa
 
DAR ES SALAAM | Dar Tower

The Dar Tower is to be constructed on 1-acre plot located next to Movenpick Hotel, a well known five-star hotel. It is a corner plot bordered by two main roads on two sides and an exclusive golf course club, Gym Khana, on the other. A number high rise towers are currently built in the proximity of the site. For example, another 25-floor building is now constructed on the former Red Cross site across the road while a similar tower to be known as Uhuru tower is being built just 250 meters away. The more established towers in the area include Barlcays House, the head office of Barclays Bank, the PPF tower owned by the Parastatal Pension Fund but used by number of banks and international organizations. A number of other high-profile companies and government agencies are located nearby, which explains why the demand for commercial and residential accommodation in the area is very high.

The proposed Dar Tower is a 25-floor mixed-use development with one level underground parking. The ground floor and mezzanine will be used for retail purposes. This will be followed by 10 floors of office space and 10 floors of residential. There will be gym with a swimming pools and coffees shops as wells. The Dar Tower is designed to serve the business community who would like to take apartments and office in the same place. The residents of Dar es Salaam can understand the importance of having all these amenities in one place at the city centre. Traffic congestion and heat are major problems in Dar, therefore having all your working and an amenity in one air-conditioned place is a major advantage for the business community. With a five-star hotel and a golf course next door, and all other banking, commercial and government offices within a walking distance, the Dar Tower is designed to provide an idyllic atmosphere to work, live and entertain. This plot is highly sought-after by companies and wealthy individuals who all competed with IPIT to own it.

The plot is acquired by IPIT through a negotiated joint venture with Nyumba Sanaa, arts and culture trust, which previously owned it. IPIT's share in the joint venture is 75% and will have full responsibility to construct and manage the building. Nyumba Sanaa share is 25% to represent the value of their land and other services they are providing. There is no time limit to the joint venture, which means IPIT will not be obliged to surrender the property to Nyumba after certain period as the case is with Build Operate and Transfer (BOT) ventures.

http://www.ipiltd.com/services/city-towe-morabaha-offer


IPI Ltd is Integrated Properties Limited


Project Overview | IPI Ltd

IPITL has acquired land measuring 200 acres in the Bahari Beach Area of Ununio in Dar es Salaam for development of the self sustained, independent state of the art satellite city comprising of the following:-

  • Executive villas, townhouses and apartments
  • Five Star Hotel
  • Hospital
  • Recreational centre school (nursery & primary school)
  • Nursery and Primary School
  • Service station
  • Shopping Mall not less than 40,000 sqm comprising of banking facilities, night clubs, restaurants, supermarkets, cinema halls and many other facilities required in a big mall.
  • Ferry service that will link the rich, sandy Bahari Beach to the main Dar es salaam port on the one hand, and the exotic Zanzibar islands on the others.
Bahari Beach Town is designed to become a self contained satellite city providing family – friendly environment for potential resident populations of 10,000 people, while its commercial units could serve additional 1,000,000 people within easy connecting area.
Location
The Project is located approximately 30km from the city centre and covering of about 200 acres within the beautiful Bahari Beach Area. The area is well connected to the electricity and water supply from the mains. It is easily accessible from the city centre and other places of interest via the New Bagamoyo road.


[h=1]Board of Directors[/h] Chairman of the Board: Mr. Omar A. Ali
Managing Director: Mr. Suleiman A. Dualeh

[h=2]Management Team[/h] Finance Director: Mr. Abduhakim Hersi
Syndicated Investment Director: Mr. Mohamed H. Suleiman



SomaliNet Forums • View topic - Somali run property project in Tanzania

[h=3]Somali run property project in Tanzania[/h] by Executive » Tue Sep 27, 2011 10:13 am
Very impressive, if we had peace and stability in our country and I think we would be able to rebuild in a short time. Its a $627.6 million housing project in Dar Es Salaam.

IPI Ltd | Bahari Beach | Property Investments Specialists

The Chairman and Managing Director
biz+index+pix.jpg

Board of Directors

Chairman of the Board: Mr. Omar A. Ali
Managing Director: Mr. Suleiman A. Dualeh
Finance Director: Mr. Abduhakim Hersi
Syndicated Investment Director: Mr. Mohamed H. Suleiman


bahari-beach-project.jpg


IPITL has acquired land measuring 200 acres in the Bahari Beach Area of Ununio in Dar es Salaam for development of the self sustained, independent state of the art satellite city comprising of the following:-

* Executive villas, townhouses and apartments
* Five Star Hotel
* Hospital
* Recreational centre school (nursery & primary school)
* Nursery and Primary School
* Service station

Shopping Mall
Not less than 40,000 sqm comprising of banking facilities, night clubs, restaurants, supermarkets, cinema halls and many other facilities required in a big mall.

Ferry service
that will link the rich, sandy Bahari Beach to the main Dar es salaam port on the one hand, and the exotic Zanzibar islands on the others.

Bahari Beach Town is designed to become a self contained satellite city providing family – friendly environment for potential resident populations of 10,000 people, while its commercial units could serve additional 1,000,000 people within easy connecting area.
Location
The Project is located approximately 30km from the city centre and covering of about 200 acres within the beautiful Bahari Beach Area. The area is well connected to the electricity and water supply from the mains. It is easily accessible from the city centre and other places of interest via the New Bagamoyo road.


swimming20pool20and20garden.jpg

several20villas20at20finishing20sta.jpg

master20bedroom.jpg

lounge.jpg

garden20-20front20view202.jpg

front20entrace20-20a20viewer20arriv.jpg

front20view20-20other20villas.jpg
 
Back
Top Bottom