Fikiria leo hii Lowassa angekuwa Rais!

Fikiria leo hii Lowassa angekuwa Rais!

Rais hawezi kuwa mgonjwa hataweza kuhimili mikiki mikiki ya kuwaongoza wa Tz wa siku hizi
 
Ningekuwa bado nanunua sukari 2000 badala ya 2300
Bashite asingekuwa anajulikana na Kolomije isingekuwa sehemu maarufu
Wahaya wangekuwa wameshasahau madhara ya tetemeko la ardhi
Hotel ya Mantaray na Kampuni ya Kajima wasingefunga biashara
 
Usimfananishe Lowasa na vitu vya kijingajinga.
 
Angekua ashatoa ajira kwa vijana waliohtimu, angekua na busara na angekubali kukosolewa.
 
777 ingekuwa sehemu ya Ikulu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Na bado mtamkumbuka mpaka yusuf makamba,ndo kwanza mwaka mmoja ikifika mitano akili zitakuwa zimeshakaa sawa.
Riasi ana roho mbaya kama mtoa roho,ye anawaza kukomoa tu.
 
Nilichogundua vijana wengi hapa hasa kwenye mjadala huu, hawaujui utendaji kazi wa Lowassa, inawezekana alipokuwa wazir mkuu wengi walikua secondary tu, ni hivi.........Lowassa ni master plan, kama hamjui ulizeni wakubwa wenu wanaogatilia siasa na utendaji ndo watawaambia who is Lowassa! Anachofanya huyu sijui kutumbua ni kuigiza tu, but wakati Lowassa ni waziri mkuu, ilikuwa ni rahisi zaidi kukutana na Kikwete ukamuelezea ujinga akakuvumilia lakini sio Lowassa hata kukanyaga ofisini kwake tu ilikuwa shughuli...... sio muongeaji ila ni mtendaji, ambao hamumjui siwashangai kuachama hapa ila tunaomjua........tunafahamu kuwa hana uvumilivu na upumbavu wa mtu!!!!!! Kwa miaka miwili tu akiwa waziri mkuu....alibuni course fupi za ualimu kwa form six leavers na kutoa ajira, project ya shule za kata imepunguza gharama kwa wazazi kupeleka watoto shule za mbali,.....hapo akiwa waziri mkuu tu, nini anhefanya angekuwa rais??? Huyu wenu kafanya nini cha maana hadi sasa? Kwa Lowassa tusingesikia kauli za mimi sipangiwi, sishauriwi, sijaribiwi, najiamini, tungeona hayo kwa vitendo kwasababu huwa si muongeaji.......kama hamfahamu, serikali ya JK ilianza kukosolewa na kupuuzwa, kusemwa na kuitwa dhaifu baada ya Lowassa kujiudhuru.....before that watu waliisifia.......may be kosa Lowassa ni kujaribu kuwa popular kuliko boss!!!!!!
Roboti
 
Lowassa angekuwa Rais haya yangetokea
1.Bunge lingeendelea kuwa mubashara
2.Watu wasingekuwa wanashtakiwa kila siku kwa uchochezi
3.Mikopo ya elimu ya juu isingekuwa ni tatizo.
4.Mfumo wote wa ufisadi wa CCM ungeng'olewa mara moja
mkuu Hizo ni nadharia, Rai yangu ni usiweke matarajio makubwa kwenye maisha ya mtu mwingine, hususan viongozi wetu
 
ningepeleka wanangu feza schools,maisha yangekuwa mweremwereeeeee,full baga
 
Lowasa ameibiwa kura.....so Mungu anatoa adhabu kwa wote.
 
mkuu Hizo ni nadharia, Rai yangu ni usiweke matarajio makubwa kwenye maisha ya mtu mwingine, hususan viongozi wetu
Hapana.Nina hakika mambo yangekuwa tofauti.Na ni lazima tuchague viongozi kulingana na mahitaji yetu.
 
post za Jf bana! povu limekutokaje, eti bora lowasaa? ha ha ha ha ha ha watanzania sio wajinga kihivyo, tutampigia kura lowassa endapo tu siku mtatuambia kwa nn mlimuweka kwenye list of shame
Hichi ulichoandika hapa kimetoka ndani ya moyo wako ama ni hisia tu za vidole kuandika utakacho
 
Hapana.Nina hakika mambo yangekuwa tofauti.Na ni lazima tuchague viongozi kulingana na mahitaji yetu.
Ni kweli tuna uhitaji mkubwa wa viongozi ktk maisha yetu, lakini ili tufanikiwe lazima tuweke juhudi kubwa sisi wenyewe, viongozi wawe ziada Tu!
 
Back
Top Bottom