Fiesta marufuku Mbeya- Sugu

fiesta ndo nini kwanza? si kudumisha ufuska tu mi namuunga mkono sugu
natamani ntukane lakini mmm.m2 mwenye medula inayofanya kaz vyema hawez kushabikia u....e huo wa fiesta wanaenda kuduu tu huko na haina tija yoyote kwa sie vijana ni upumbav kabisa fiesta. namuunga mkono sugu.nyambaf fiesta
 
Hapo Kachemuuuuusha! he needs advices asap! mambo hayafanywi kiholelaholela hivyo! i hope ataligundua haraka hilo kabla hatujapoteza jimbo hili!
 
mWENYE C V KAMILI YA SUGU PLEASE NDIPO TUENDELEE KUJADILI HAYO MENGINE
Ili tuwe wana jf halisi tungejadili hoja yake tuone ina mantiki gani, si kazi (moral) ya ethical jf members kujadili watu bali hoja.
 
Mnaotetea fiesta kwa kupinga hoja ya sugu leteni sababu za kutetea vinginevyo mnapiga majungu tu na kufanya Sugu aonekane yupo sahihi
 
nyie wote mnaomtukana sugu jaribuni kufikilia fiesta inafaida gani kwa wana mbeya kwa sasa? Tofauti na kwenda kufanya upuuzi sugu yuko sawa kwa agizo lake kwa hyo swala la matusi na kejeli siyo nzuri kwa mh mbunge na mimi namuunga mkono kwamba fiesta aina faida kwa wana mbeya bora yangekuwa ni makongamano ya dini hapo sawa kwa sababu watu wangeweza kupokea neno na wakaacha maovu, swala la fiesta linaweza kujenga maadili kwa vijana wa mbeya?
 
hehehe sugu bana.. any way sio official statement ... ni facebook status ambayo ikiwa empty kuna vijimaneno "what do u think right now" ...
 
Huyu!! Atapiga marufuku hata maandamano sasa! Hilo nalo ni tamko lake manake CDM sasa imekuwa ya matamko. Yeye kwenye posho hajatoa tamko ameona ni vyema atoe tamko kwenye FIESTA.
 
Kama ni kule FB na wewe unamkubali, kamgongee like kwenye comment. Otherwise sio kazi yake, make ataanza kusema Mbeya Carnival ifungwe na bar Club Zote kwa sababu haziinui vipaji.

Piga kazi Sugu, acha vijana waburudike.
 
Mbunge wa Mbeya Mr. II amepiga marufuku matamasha yote ya FIESTA mkoani mbeya kwa madai kuwa yanaua vipaji vya wasanii. Source status yake ya FB.

Sugu,

Inakubidi usomeshwe kazi na majukumu ya mbunge kabla kukurupukia vitu vingine.

Sugu, shule muhimu mheshimiwa
 
Hihihihihihi......ana machungu na wandaaji wa Fiesta na lile dili lake la Malaria......
 
Hawa wabunge wengine sijui walitokea wapi? Wakati mwingine huwa sioni umuhimu wa kuwa na Bunge ambalo wabunge 85% na zaidi ni mbumbumbu.

This is too low for him, naamini Jimbo la Mbeya lina changamoto nyingi na muhimu sana kuliko 'kijitamasha' la masaa 8 kwa mwaka.
 
Kwa kweli hapa Mhe. Sugu amechemka, na walio karibu nae basi wajaribu kumshauri asifanye maamuzi ambayo yataonekana kama ni ya kidikteta, issue kama hii itamfanya aonekane yuko out of touch na vijana, ambao akumbuke ndio margin kubwa ya wapiga kura ifikapo 2015.
Tufahamu walengwa wa Fiesta ni vijana na wengi ni wa rika la miaka 15-22 na kwa mtazamo wangu nadhani dhumuni la tamasha kama hili ni kuwaburudisha (entertain) vijana, ni nafasi yao pekee kuwaona ma-Idols wao jukwaa moja kwa kiingilio rahisi.
Vijana wa Mbeya nao wana haki kama vijana wenzao nchini kwetu ya kuwaona wanamuziki wao wanaowapenda na sio sahihi kuwanyima haki yao hii.
Hivi mfano yeye Sugu ndio mmoja wa wasanii kwenye hii Fiesta mfano Mwana FA ama FidQ angejisikia vipi kama wapenzi wake wa Mbeya waliojiandaa kumuona wameshindwa, kisa Mbunge kaleta kauzu?
Naelewa wazazi walio wengi watampa sapoti kwa sababu kwa jicho la mzazi vijana wao bado wako vulnerable katika mikusanyiko kama hii, lakini hii isiwe ndio sababu ya vijana kukosa haki zao kufurahi, la msingi ni kila mzazi kumpa darasa kijana wake, na hawa waandaaji wa matamasha na wasanii wajitahidi kutoa elimu na ujumbe katika hii mikusanyiko.
Zama hizi za utandawazi, vijana wengi wa leo wanawasikiliza zaidi ma-Idols wao kushinda wazee wao. Huo ndio ukweli wa kusikitisha.
Mr. Sugu ajue asilimia kubwa ya wapiga kura 2015 ndio hao anaowakataza wasione Fiesta, anatakiwa ajenge ukaribu nao zaidi na sio kuwapeperusha. Akiendelea na mwendo huu asahau kipindi cha pili.
 
Nilikuwa shabiki namba 1 wa sugu ila sahv ameanza kunitia wasiwasi na upeo wake wa akili,ukataze fiesta kwa sababu/sheria ipi?Halafu ndo huyuhuyu aliyetuambia wanajimbo wake wakija watu fulani tuwapige mawe
 
Back
Top Bottom