KIGENE
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,551
- 813
Rais wa zamani wa Cuba Fidel Castro amekanusha vikali taarifa zinazosambazwa na vyombo vya habari vya magharibi na kulikandia hasa gazeti la Hspania la ABC pamoja na mitandao ya kijamii, kwa kuutangazia ulimwengu kuwa afya yake imedorola ile mbaya,Castro alitamba kuwa ni muda sasa ajasumbuliwa na ugonjwa wowote hata walau kuumwa na kichwa.
Katika makala inayoonyesha picha zilizopigwa na mwanaye Alex Casrto inamuonyesha Fidel Castro mwenye umri wa miaka 86 akiwa katika bustani ya miti na nyingine akiwa anasoma gazeti la Gramma.
Fidel Castro hajaonekana hadharani tangu Marchi wakati alipokutana na Papa Benedict XVI.
Fidel Castro alingatuka madarakani mwaka 2006 baada ya kuugua kwa muda na kukabidhi mikoba ya kuendesha taifa la Cuba kwa ndugu yake Raul.