Amina Thomas
JF-Expert Member
- Mar 9, 2008
- 272
- 129
Hawa jamaa wanajiita 'events organisers'. Leo kulikua na siku ya mtoto wa afrika. Shule 4 zilishiriki pale cine club, zikiwemo bahari beach, saint florance, lincoln na saint valentine. Kila mtoto alichajiwa sh. 10,000 ikiwa pamoja na lunch. Kila mzazi alitakiwa kulipa 3,000. Kwanza watoto walikaa na njaa mpaka saa tisa kasoro, tena baada ya wazazi kudai na watoto kuanza kulia, kwani shuhuli ilianza toka saa tano asubuhi! Chakula chenyewe kikawa cha kugombea mpaka kutaka kupigana. Soda moja iligawiwa mara 2 kwenye glasi! Kwa kifupi hakukuwa na entartainment yoyote kwa watoto kwani hata michezo yote iliyokuepo hapo walitakiwa kulipia 1,500. Watoto wengine hawakula mpaka saa 11, tena baada ya kuzuka ugomvi mkubwa! Kwa kweli huu ni utapeli wa wazi!