Ferooz: Rais Mkapa hakuninunulia gari

Safi sana nadhani kwa maneno yako Ferouz bado mkapa ataendelea kukuona mpumbavu na lofa

Usinisahau kwenye Baraza Jipya.
 
Nyimbo za wasanii wakongwe hazijawahi kukinai kama hizi za akina sheta!

Pini kama mkasa wa boss, barua,wife,mtazamo,nikusadieje,vumilia and the list goes.... Ubora na uthamani wake sio kushuka Leo wala kesho kwa mtu anaeujua muziki.

Muziki zamani, siku hizi ni utani,hakuna hata burudani wala madini, akili zao zote zipo sokoni.

sent from tekno ya shilingi elfu saba na mia tano.
Mkuu umenifanya nikamkumbuka Mfalme Wa Ryhmes Afande Sele kwenye pini lake Mtazamo aliwahi kuuliza "Hivi kwani lazima tuwe wote wasanii...!?"

Kizazi cha sasa hivi kinaharibu sana muziki yaani nyimbo zinatolewa kila uchao zenye ladha ya Big G yaani wimbo unatoka leo kesho umeisha ladha hutamani tena kuuskiliza.

Lakini ikitokea likapigwa pina la Sonia kwa mfano, au Piga makofi au labda Hii Leo, Kikao cha dharura, Msinitenge etc, etc yaani una~enjoy hadi kuhisi msanii husika kautendea haki moyo wako.
 
kama ela ulipiga sana kipindi ile

sent from my iphone 7 nimeinunua SAPNA pale POSTA
 
Mkuu umenifanya nikamkumbuka Mfalme Wa Ryhmes Afande Sele kwenye pini lake Mtazamo aliwahi kuuliza "Hivi kwani lazima tuwe wote wasanii...!?"

Kizazi cha sasa hivi kinaharibu sana muziki yaani nyimbo zinatolewa kila uchao zenye ladha ya Big G yaani wimbo unatoka leo kesho umeisha ladha hutamani tena kuuskiliza.

Lakini ikitokea likapigwa pina la Sonia kwa mfano, au Piga makofi au labda Hii Leo, Kikao cha dharura, Msinitenge etc, etc yaani una~enjoy hadi kuhisi msanii husika kautendea haki moyo wako.

Mkuu nawe pia umenikumbusha mbali sana, kikao cha dharura was one of my most favorite tracks mpaka nilifikia hatua ya kununua redio ya cassette kwa ajiri ya kuiplay. Asante.

sent from tekno ya shilingi elfu saba na mia tano.
 
Shukran kwa kulitolea maelezo Manaake hii taarifa hata kwetu huku ushetu ilisambaa vilivyo yakwamba ulipewa gari na mh.Mkapa

Nawaheshimu sana wasanii wakongwe hapa Tanzania mlikitendea vyema kipindi chenu kwa nyimbo zenu nyingi zilizo na lundo la mafundisho katika Jamii na uhalisia haswa!!


Nyakati zinabadilika,heshima kwenu wakongwe!
Wahenga wetu ao

LOVE ABOVE ALL
 
Kwani, aliyesema kuwa kapewa gari na Mkapa ni nani? Kipindi kile habari zilisambaa sana mitaani kuwa alipewa zawadi, kwa nini hakukataa kipindi kile kile kuwa hakupewa zawadi? Hii habari hata aisngeiandika sababu haina maana kwake! Rais hayupo madarakani, hilo gari alishaliuza miaka kumi iliyopita na sasa itakuwa ni scraper tu. Hii habari sijui mmeileta ile iweje, maana hakuna ujumbe wowote hapo.

Kutoa nyimbo hivi kwa kipindi hiki inabidi ujipange haswa, maana kuna ngoma kali zinaachiwa kila siku. Kama ngoma yako siyo kali, unaweza kuifungia hadi miaka miwili bila kuitoa. Ajipange sana!
 
Kwa hiyo sasa unataka upewe au unataka tufanye nini Bwn. feruzi?
 
mi navyojua hyo gari alipewaga zawadi na taasisi 1 inayojihusisha na mambo ya ukimwi baada ya kutoa ile nyimbo ya starehe,,
 
mi navyojua hyo gari alipewaga zawadi na taasisi 1 inayojihusisha na mambo ya ukimwi baada ya kutoa ile nyimbo ya starehe,,
Amefanya mahojiano na EATV hakusema kama alipewa hiyo gari na Taasisi inayojihusisha na mambo ya Ukimwi. Angalia bandiko linavyosema
 
Back
Top Bottom