Feedback kutoka arabuni...

Feedback kutoka arabuni...

hio tsh 200,000 ni mshahara wa siku moja[8hrs] kwa kazi kama hio UK.

Matumizi ya UK ni bilaha vitu bei ghali ata misosi kwenye mgahawa. Hiyo laki 2 kwa siku wala uwezi kuishi vizuri London
Hapo bado kulipa bills na nyumba etc. Watu wako bize balaha
 
ARABUNI?...kazi za ndani? hahahhaahaaa, USIPELEKE NDUGUYO!
 
waarabu wa hapa Tz tu si waamin sembuse wa hukooo akuu huyo binti mpeleleze vizuri kuna siri kubwa nyuma ya pazia
kweli mdada, hii inatia mashaka..ukiskia tu mtu kaenda mombasa kasheshe
 
Matumizi ya UK ni bilaha vitu bei ghali ata misosi kwenye mgahawa. Hiyo laki 2 kwa siku wala uwezi kuishi vizuri London
Hapo bado kulipa bills na nyumba etc. Watu wako bize balaha

nimeishi UK muda mrefu sana.......kitu chenye gharama kwenye bajeti ni kodi ya nyumba.....vitu kama chakula na mavazi havina bei kabisa....labda utake kula kwenye posh restaurants na kushop designer gears.....prove me wrong weka bei za chakula za mcdonalds,kfc,burger king na za mitaani za wahindi/turkish sizitaji ndio hazina bei kabisa.....btw tusichakachuwe thread....tukubali kutokubaliana.
 
hizi kazi ndizo Mh. wa Temeke huwa anawatafutia wapiga kura wake? ama huwa za professional gani
 
hahaaa! na kalivyo karembo..! mmh! waarabu siwaamini kabisa... watakuwa wamekageuza tende..!

mafanikio ya watu yana mambo mengi nyuma yake, usione watu wanaenda ng'ambo na kurudi ukakurupukia. hebu muhoji vizuri, mwenyewe nataka kwenda huko.
 
Hapana, labda uwe na bahati ya mtende kupata tajiri mzuri. Hawa watu ni wabaguzi na wanawa-treat wafanyakazi wao kama watumwa vile. Nilipata maelezo kutoka kwa dada mmoja wa Kenya aliyelazimika kutoroka kutoka kwa bosi kutokana na matatizo kibao kufanyishwa kazi muda mrefu bila kupumzika, no likizo, chakula cha watoto wa boss na uchafu mwingine kibao. Kibaya zaidi ukifika huko unanyangwa pass ya kusafiria na hivyo hata wakunyanyase vipi huwezi kuondoka kwao.

Kwa kweli nisingewashauri wadogo zangu kwenda arabuni kufanya kazi za ndani, waarabu hawafai (Sitaki kuja kushambuliwa hapa, nimezungumzia waarabu, sijazungumzia dini yao).

Tiba
 
Kweli tumefikia pabaya, kumbe wale mabinti wa TMK, mbunge wao anajidai anawatafutua kazi uarabuni na kwenye magazeti anatangazwa kwa mbwembwe kumbe wanaenda kufanya kazi za ndani, loh dada zangu chungeni sana, someni mjikwamue na mkwamue wenzenu. Unasifia uhausgeli wa uarabuni kisa laki 2!!? Shame on you
 
isije kuwa huyo dada chakula ya bosi. vipi lakini gharama za maisha maana hiyo hela ilivyoletwa kwenye tsh imeonekana ndefu sana kwa hg lakini si ajabu kwa maisha ya huko utaishia kununua chakula tu cha mwezi.

@Husniyo,

Arabuni hasa Oman, kwa vile wanaoagiza hao dada wa nyumbani wengi wao ni wenyeji wa Tanzania, Kenya, Uganda, Congo na Ruwanda na Burundi. Hivyo basi mazingira ya uhusiano wao baina ya Dada na Bosi (Mama wa nyumba) hasa wa Tanzania hayana tofauti na huku nyumbani.

Mara nyingi wanaishi kama ndugu, wanatakiwa wawe weledi wa kazi zao, na wawe wasafi kimwili na katika kitunza mazingira ya ndani ya nyumba. Kuwa Muislam na kujuwa Kiingereza au Kiarabu or any of the three is an added value.

Kazi ni kusafisha nyumba ndani na nje, kufua nguo kwa automatic machines, kusaidia kupika au kupika na kazi za jikoni.
Wengine hutakiwa ulezi wa mtoto tu au kusaidia kizee cha nyumbani kama vile kufuatana nae katika mazoezi ya kutembea, kumtandikia kitanda, kumtayarishia.chakula chake maalum hata kumsimamia.msalani kwa wale vizee wagonjwa.

Wengine hata kumwagia maji bustani.
Wengine dereva wa kupeleka watoto shule na mama sokoni.

Mambo anayopata free:

Malazi mazuri sana chumba chake mwenyewe, self contained with A/C.
Chakula ndio hicho hicho kitakachopikwa na ikiwa mfano anataka kupika cha kwake mwenyewe mfano Ugali.
Matibabu na gaharama zake ni juu ya mwajiri wake. Mara nyingi hufunguliwa Life Insurance account ikawa analipiwa na Insurance firm.

Mara akifika tu hupewa induction na pia kusaidiwa nguo na hata kupewa simu kama hana.

Kwa hivyo mshahara wake ni.safi tax free.

Asiyotakiwa kufanya:

1. Umbea, ikiwamo kuwa asishiriki maongezi ya wanafamilia wala kuchonganisha.

2. Kuvaa nguo sisizo staha kama vimini na vitop. Anatakiwa asionekane, makwapa yake na kifua wazi au kitovu wala sehem za mwili wake sehemu zengine zinazoleta uchokozi.

3. Uzinzi wa ndani na nje, ulevi, na kudandia baba au watoto wake. Hili litamwondoa na kumrudisha nyumbani Bongo siku ifuatayo.

Hata hivyo mambo yote hayo yamo kwenye mkataba ambao unasimamiwa na Ubalozi wa Tanzania. Kama huna huo mkataba huoni ndani ya ndege katika.viwanjavyetu JKNIA, AAKIA znz.

Muwe na hadhari kuhusu maeneo ya kazi. Maagenti wengine hawasemi ukweli. Msikubali kupelekwa kufanya kazi nje Mji Mkuu wa Muscat. Ombeni mhakikishiwe kama mwajiri wenu yuko mji mkuu au at least awe ana asili ya huku kwetu.

Msikubali kufanya kazi kwenye nyumba za wasio ongea Kiswahili na wenye watoto wengi wadogo.

Mishahara nayo inategemea mabosi wenyewe huwa inatofautiana na kazi zenyewe lakini si chini ya 200,000.
 
Halafu mtu anajikakamua kabisaaa..."ANALIPWA LAKI MBILI"!!!!..tzs 6700 kwa siku!!!!! kwa kazi ya utumwa!!!! dada zangu bakini bongo tu tulime, huyo aliyeenda kutumikishwa mwaka mzima amerudi na simu ya samsung!
 
ahsante Averoes kwa ufafanuzi mzuri. vipi gharama za maisha lakini. kwa mfanyakazi anaepokea tsh 200000 huko uarabuni anaweza kumudu maisha kama anajitegemea mwenyewe?
 
Last edited by a moderator:
WE NDIO MBURULA.....mtoa mada kazungumzia mshahara sio matumizi.........unaonyesha umbulula wako UK mlo unapata hadi GBP 2 mshamba wewe....chips kuku/burger/chinese mitaani huku hazina bei....chakula bei ya kutupa.....mcdonals,kfc,burger king ukiwa na GBP 4 unakula fresh tu.....
hivi mburula maana yake nini?, maana naona mnaitana mburula, nikijua maana yake mimi ndiyo nitajua yupi ni mburula mkubwa na yupi ni mburula mdogo
 
ARABUNI?...kazi za ndani? hahahhaahaaa, USIPELEKE NDUGUYO!

mkuu, hebu tupe kilichomo ndani..

mimi ndugu yangu nimeleta tu feedback.. sikuchimba kiundani kwa sababu ya muda..

karibu
 
hivi mburula maana yake nini?, maana naona mnaitana mburula, nikijua maana yake mimi ndiyo nitajua yupi ni mburula mkubwa na yupi ni mburula mdogo

tafadhali mkuu.. dont fight with RRONDO.. ongeeni future ya wadogo zenu na ndugu zenu waendao arabuni..

huwezi jua labda kuna vitu zaidi wanafanyiwa ambavyo sivyo..
 
Last edited by a moderator:
Halafu mtu anajikakamua kabisaaa..."ANALIPWA LAKI MBILI"!!!!..tzs 6700 kwa siku!!!!! kwa kazi ya utumwa!!!! dada zangu bakini bongo tu tulime, huyo aliyeenda kutumikishwa mwaka mzima amerudi na simu ya samsung!

mkuu mbona unaongea kwa kashfa namna hiyo? laki mbili kwa mwaka si ni sawa na tshs 17000 tu kwa mwezi?

sasa nani yuko tayari kufanya hio kazi?

tafadhali sana usipindishe kauli..
 
it could be true, angalaia mahesabu hapa chini

200,000/2500= UK paund 80 ambapo kwa saa ni paund 10
 
Back
Top Bottom