mkuu mbona unaongea kwa kashfa namna hiyo? laki mbili kwa mwaka si ni sawa na tshs 17000 tu kwa mwezi?
sasa nani yuko tayari kufanya hio kazi?
tafadhali sana usipindishe kauli..
Kweli tumefikia pabaya, kumbe wale mabinti wa TMK, mbunge wao anajidai anawatafutua kazi uarabuni na kwenye magazeti anatangazwa kwa mbwembwe kumbe wanaenda kufanya kazi za ndani, loh dada zangu chungeni sana, someni mjikwamue na mkwamue wenzenu. Unasifia uhausgeli wa uarabuni kisa laki 2!!? Shame on you
Usinielewe vibaya tu mkuu, kule hawaitwi wafanyakazi wanaitwa "watumwa" na mila za kiarabu zinaruhusu kutenda chochote mtumwa wako! wale watu wanafanyishwa kazi masaa ya kuzidi, hakuna kupumua na manyanyaso juu, sasa mshahara wa 200K hailipi, ni heri kulima matuta ya viazi hapahapa bongo!
Hapana, labda uwe na bahati ya mtende kupata tajiri mzuri. Hawa watu ni wabaguzi na wanawa-treat wafanyakazi wao kama watumwa vile. Nilipata maelezo kutoka kwa dada mmoja wa Kenya aliyelazimika kutoroka kutoka kwa bosi kutokana na matatizo kibao kufanyishwa kazi muda mrefu bila kupumzika, no likizo, chakula cha watoto wa boss na uchafu mwingine kibao. Kibaya zaidi ukifika huko unanyangwa pass ya kusafiria na hivyo hata wakunyanyase vipi huwezi kuondoka kwao.
Kwa kweli nisingewashauri wadogo zangu kwenda arabuni kufanya kazi za ndani, waarabu hawafai (Sitaki kuja kushambuliwa hapa, nimezungumzia waarabu, sijazungumzia dini yao).
Tiba
Matumizi ya UK ni bilaha vitu bei ghali ata misosi kwenye mgahawa. Hiyo laki 2 kwa siku wala uwezi kuishi vizuri London
Hapo bado kulipa bills na nyumba etc. Watu wako bize balaha
ahsante mkuu kwa maelezo mazuri.. sikujua kabisa kama haya mambo bado yapo..
pia sidhani kama kuna mtu atakayechanganya na dini... serikali inazungumzia nini kuhusu hili mkuu? kwanini kimya lakini?
Mkuu serikali iseme nini wakati watu wanajipeleka utumwani wenyewe? Zamani waarabu walikuwa wanafunga safari kutufuata huku kwetu lakini sasa upepo umebadirika, sisi wenywe tunaangaika kutafuta nauli na visa na kujipeleka wenyewe utumwani.
Tiba
umepewa feedback mkuu, mbona unalalamika?
hivi ulishawahi hata kuulizia nini kinaendelea huko baada ya wao kwenda?
mbona sasa walia baada ya kupewa ukweli?
Aliekwambia nalia nani ndugu, fursa zote hizi tulizo nazo hapa nyumbani kuna haja gani ya likiongozi zima kuwataftia sistaz kazi ya ubeki tatu uarabini??? Kama anawajali si angewawezesha kiuchumi mfano wajikusanye vikundi awataftie ardhi mkuranga wakalima mboga mboga kwa ustadi tuna shopping malls na masoko pia, taratibu wangeeleshwa juu ya vikoba na saccos wakiwa wanazalisha shambani, after time na wao wangeajiri. Lakini uhouse girl, wamusomea VETA au? Ndugu? Tujipange
MKUU, aina ya uchumi iliyopo sasa ni free market.. nadhani unaelewa hilo!
ni mara ngapi watu wanaambiwa kilimo lakini wanagoma kufanya kazi?
hivi unadhani kilimo ni rahisi tu kama inavyotamkika? kwa wadada wa dar es salaam wanavyopenda simple life, nani atakaeenda kulima?