Wewe ndo mimi ila nimekosa imani na bayern kidogo pale aliporuhusu Goli mbili pale kwake pia kurudishwa kwa goli mbili kule Italy.
Hawa majamaa ili kuwaweza ni kuanzia Game kwao kisha kumaliza Camp Nou.
Jana nilikuwa na watu nawachambulia soka nikawaambia Bayern leo ndo ilikuwa safari.
Kilichowaumiza Juventus ni ile kasi ta Bayern, Juve walishachoka kabisa. Bonucci, Chielin, Evra n.k wote walishachoka tayari na goli zote mbili za mwanzo zimefungwa wakati mmoja. Goli zingine mbili za mwisho zimepigwa pia wakati mmoja.
Bayern nzima jana waliwaanzisha vijana tuu, kasoro Frank Ribery ambaye naye alienda bench.
Ili Barca kumpiga Bayern inabidi umiliki wewe mpira mda mwingi pia uwe na watu ambao wakipata nafasi hawakuachi, apa nazungumzia akina Neymar na Messi au Kun Aguero.
Dah game ilinipita kamanda...leo ndio nimecheki youtube, dah msn wamepiga ball c mchezo! Ila magoli ya Messi & Suarez ni balaa aisee, big up kwa wote msn