Fatma Karume nyani haoni kundule, kaa kimya

Fatma Karume nyani haoni kundule, kaa kimya

Nibora ifike mahali Bi Fatma akae kimya maana upo msemo unasema nyani haoni kundule, ikiwa anasema Dk Shein sio rais wa znz basi ajiulize Aman Karume alikuwanani na kwa nini hakuwahi fanya haya anayafanya, nadhani anapaswa kuogopa Mungu maana familia yao ni moja ya familia inafaidi matunda ya ccm. nakuliko kuwa ndumila kuwili na watu kumshanga basi bora kuwa kimya.

Akuna mtu mwenye akili anamuelewa huyu bib labda awe muwazi anatumiwa na akina nani kwa maana akumbuke kuwa hawezi kuwa double agent ndani ya taifa ambalo yeye anaishi bora angekuwa akina snowden akaenda uwamishoni nakuanza kuchonga ila kwa sasa anachokifanya kama kweli anajuwa sharia basi anafanya ujuma inayoweza kuzaa uhaini ambapo penalt yake ni mbaya sana. Pia ukumbuke muda huo majuto huwa ni mjukuu au kitukuu.

Kama ni mzazi unaweza kufikiri labda maisha yamemvuruga au kuna jambo anapitia ktk maisha limemchanganya. Lakini sii kweli Bi Fatma anajuwa kile anakifanya na kwakuwa nimsomi mzuri wa sharia anajuwa kile kinaweza kumpata au kumfika kwa kauli zake zisizo jenga umoja na mshikamano baina ya wa zanzibari wenyewe kwa wenyewe na ata watanzania wote kwa ujumla.

Nini kinamsumbuwa hasa bib huyu? kama wewe ni mgeni wa chama Fulani kilichosusa uchaguzi hivi majuzi basi waweza fikiri Fatma ni mropokaji hajuwi kile anazungumza, tuseme ule ukweli hiki chama kinawekeza kwa kiasi kikubwa ktk propaganda za uongo,chuki na hata unafiki na hoja yao ni moja sii tu kuvunja huu muungano ila chuki na fitina mbaya kati ya wabara na wazanzibari, waunguja na wapemba kwa wale tunao penda kusikiliza hotuba za mwalim utajuwa kwa nini alisema nje ya muungano hakuna Zanzibar bali kunawao wapemba sisi waunguja. Kile anakifanya uwenda kwa kurubuni watu eti anakosoa serikali kwa kutumia kifung 18 cha katiba sii kweli huu ni mtaji mkubwa kwa chama Fulani kuleta matokeo chanya ya znz kutotawalika na kwakuwa yupo mtu kama Fatma lazima wamtumie vizuri hata kama gharama itakuwa kubwa kiasi gani wao wapo tayari.

Haya sio mambo yakufunga macho ila nimambo yanahitaji akili ya hali ya juu kujuwa nini kinamsibu mtu kutoka familia ya muwasisi wa taifa kuropoka maneno kama yale ameropoka. Ninani kati yetu anaweza kusimama aseme hajuwi kile kinapangwa na kufanywa chini kwa chini ktk kuharibu umoja wa wazanzibari na chuki inayokaribia watu kuuwana inayo sababishwa na chama fulani chini ya mwavuli mtu, watu na nchi Fulani.

Usaliti anaufanya Fatma karume akiwa ndani ya ccm na kadi ya ccm ni sawa nakuchukua silaha nakuinyoosha kwa rais je wategemea nini utafanyiwa na mlinz wa rais, majibu mnayo. Au kujifisha bomu nakujilipua ktk ya umati wa watu. Huu ni usaliti ambao ktk siku za mbeleni Fatma aweza kulipia gharama kubwa kwake yeye na familia yake maana upo msemo unasema achumae janga hulila na wanyumbani kwake. Huwezi ukasimama tena mtoto wa kike unadiriki kumkashifu rais tena ktk mtandao ukahisi upo salama, hiyo haipo duniani hata kama ndio democrasia basi haipo duniani na kama ipo tueleze hilo taifa na kwa sharia gani?.

Nakukumbusha mifano michache ya watu walio wahi ropoka na kwa hivi sasa wanajutia uropokaji wao nikupe mmoja tu John Mnyika.
Mnyika akiwa bungeni na akijuwa sharia ya kinga na madaraka ya mbunge bungeni alimtusi Mh Rais Jakaya Mrisho kuwa yeye ni dhaifu. Hii Hoja ilivuma sana ila muulize huyo mnyika nini alikutana nacho na kwa nini uwenda atalipi hiyo dhambi mpaka mwisho wake.

Labada nikuelimishe kidogo juu ya taasisi Rais maana inawezekan ni mwanasheria ila hili hulijuwi. Hujamdhailisha Dk Shein ila umeidhalilisha taasisi nzima ya Rais ambayo ndani yake kuna hako kaneno ka jeshi, je unajuwa walinzi wasiri wa rais? Huwajuwi? je wawajuwa watu wanalinda hilo dola la watu wa znz hujuwi, je wajuwa nani wanafanya nini kumlinda Rais hujuwi. Acha mara moja hii mambo tena ukiwa ndani ya chama na serikali unayoibeza. Nakushauri uwache nikiwa kama Raia mwema wa taifa hili mwambie aliekutuma akupe kazi nyingine maana hii huiwezi ama akuruhusu umtaje hadharani alie kutuma maana niukweli usio pingika unayo ajenda ya siri kwa kipindi sasa ila unatoa vipande vipande. wasaliti adhabu yao ni mbaya na hakuna mtu amewahi rudi kusimulia ilikuwaje. Unapoteza muda kwa kuchota maji baharini na kujaza kwenye kishimo ukifikiri bahari itahamia kwenye kishimo ulicho chimba, kiukweli unapoteza muda kuwahadaa wa znz na taifa kwa ujumla ila ukasahau nyani haoni kundule.

Labda Mimi nisema huna hata misuli yakimapinduzi bora ukae kimya nakunywa urojo siku ziende, maana anayotafuta yatakuwa mabaya sana na wenye hekima watakukumbusha tulikwambia chunga mdomo wako. Hili ni taifa na rais kesha apishwa huku kila idara inayo mzunguka ipo kazini , ukumbuke msemo wa Rais mstaafu Kikwete wakati mwingine akili zakuambiwa changanya nazakwako...

Hata hizi zakuandikiwa changanya uchukue au uache ni uamuzi wako
sasa na wewe unatumiwa na nani? kukosoa ndani ya serikali yako au chama chako wakiwa wanafanya sivyo ni wajibu wa kila mtu, hata uwe mbunge au waziri, kama rais amekosea basi wewe una haki ya kumwambia kuwa hivyo sivyo, hiyo ndiyo siasa ya kuleta maendeleo. inaoneka wewe mtoa mada ni mbinafsi au una chuki binafsi na vile vile hupendi maendeleo ya nchi yetu.Yaani ukiona kiongozi wako au serikali yako inafanya sivyo unyamaze tu ati kwa kuwa wewe ni mshabiki wake?
Soma hiyo link niliyoweka hapo uone siasa za wanaopenda maendeleo ya nchi zao. Iain Duncan Smith alikuwa waziri wa serikali ya uingereza na aliikosoa serikali kwa kufanya sivyo, na aliwaambia kila mara kwamba sivyo, na alipokuwa hasikilizwi aliamua ajiuzulu, huyu bwana anaungwa mkono na wananchi wengi sana wa uingereza.Hayo yametokea kama wiki 2 tu nyuma. Sasa mtoa mada ungekuwa wewe na hiyo akili yako ndogo uliyokuwa nayo basi ungeendelea tu kubaki unakufa na tai shingoni lakini hutaki kusema ukweli. Kwa hiyo mimi ushauri wangu ni kuwa tusiwe na siasa za chuki, tuwe na siasa za kuleta maendeleo.
Iain Duncan Smith quits over planned disability benefit changes - BBC News
 
Kung'ang'ania historia inayopalilia uadui badala msamaha na toba basi Zanzibar daima itaendelea kutawaliwa na kukaliwa na DODOMA

Kumsomesha mtoto usitegemee mtoto huyo kukutii kwa kila kitu hata kwa mabaya, kama haya yaliyofanywa na CCM na Dr Shein kwa kubarikiwa Jecha .
Fatma amesutwa na UZALENDO & USOMI wake
usomi wake ungeonekana wa kizalendo km angeanzia kweny mzizi wa tatizo kuliko kuanzia sehemu ambayo anajua wachambuz wakianza kuchambua kauli zake ajikute nje ya ulingo kwann asiseme historia alf akajitetea kuwa alishiriki haramu bila kujua?
 
Mleta mada umefanya la maana kumuonya huyu dada lakini sidhani kama atakuelewa kwa kuwa ameshakubali kutumiwa na wanasiasa kwa maslahi yao. Pili huyu pinti kaonekana kajeuri flani hivi inaonekana hata mumewe anapata naye tabu sana kwa tabia yake. Ningekuwa ndiye mumewe ningeshamlima talaka tatu bila huruma kitambo sana.
 
warudishe ardhi walizopora wazanzibar kipindi baba yake akiwa madarakani mpaka wakawa wanamuita pangu hapa halafu ndio aje na hadithi zake
 
Back
Top Bottom