Fastjet ni jipu

Fastjet ni jipu

Ukiangalia kwa uhalisia sasa hivi Fastjet hawana bei nafuu nimewahi kupoteza ticket ya 245,000/- Safari ya kwenda tu Dar-mbeya(one way) baada ya kuchelewa ticket ikawa imepotea ukiangalia wanatudanganya sana.
Tofauti na Precision Air kipindi cha nyuma nilikata ticket 195,000/- baada ya kuchelewa nilichajiwa gharama ya 60,000/- kama gharama ya kuchelewa na kubadilisha ticket ambayo kimsingi niliiafiki .

Lakini hili la fastjet kucharge gharama kubwa alafu ticket hauwezi kubadilisha kwakeli wanatuibia sana.
 
Jumatano ilikuwa mzee asafiri tukawa tumeshamkatia tiketi ila kwa bahati mbaya tukapata msiba ile kuomba kubadilishiwa tiketi kusogeza mbele gharama ikawa kubwa kuliko tiketi mpya

Tukakata tiketi mpya ya kuondoka leo

Leo mzee alipaswa kuondoka sa nne na dak kumi asubuh tukafika pale Airport na akaingia cheking! Pale akarudishwa mara tatu mzigo wako ulikuwa na pafyum na kachuma kadogo eti alipofanikiwa kupita mbele wakamrudisha kuwa kachelewa dak mbili

Kuwaeleza amecheleweshwa na walinzi wakagoma na hapo ni sa 3 na nusu inamaana bado dak 40 nzima ndege iondoke

Mzee akarudi nje baada ya kuelekezwa aende ofisi za kampun anayotaka kusafiri nayo ili wao ndo wampeleke pale apitishwe

Kufika ofisi ya fastjet pale eti wanagoma hawana nafasi ya kutoka hivyo mzee akate tiketi nyingine

Nilijikuta nawatukana matusi mpaka nikaondolewa na walinzi

Mtu yupo palepale uwanja wa ndege na bado muda wa kuondoka ndege anazuiwaje kuingia???

na hizi pesa tulizomkatia mzee mara mbili anashindwa kusafiri nani anazila?

Magufuli tusaidie hili jipu

Pole sana ndugu yangu, ila tambua kosa la chupa ya perfume si la FASTJET ni la kiusalama na sio wao wanashughulikia usalama. Ulipaswa kuelewa taratibu ya kusafiri na ambazo nadhani zimeelezwa katika kila ticket hata kama ulikata online.

Wewe waweza ona dakika bado nyingi lakini pia mashirika ya ndege yanabanwa na sheria za kiusalama. Hawawezi hatarisha leseni yao kwa abiria huyu mmoja ndio maana kuna zaidi ya masaa 2 kucheck in ili litokeapo lolote uweze tatua kabla ya muda kwisha. Pole sana lakini naelewa ni kiasi gani ticket mbili na msafiri asiende inavyo umma maana imewahi nikuta kwa makosa madogo madogo kama hayo kwa washirika wa FASTJET wanaitwa EASYJET huko Ulaya.
 
Jumatano ilikuwa mzee asafiri tukawa tumeshamkatia tiketi ila kwa bahati mbaya tukapata msiba ile kuomba kubadilishiwa tiketi kusogeza mbele gharama ikawa kubwa kuliko tiketi mpya

Tukakata tiketi mpya ya kuondoka leo

Leo mzee alipaswa kuondoka sa nne na dak kumi asubuh tukafika pale Airport na akaingia cheking! Pale akarudishwa mara tatu mzigo wako ulikuwa na pafyum na kachuma kadogo eti alipofanikiwa kupita mbele wakamrudisha kuwa kachelewa dak mbili

Kuwaeleza amecheleweshwa na walinzi wakagoma na hapo ni sa 3 na nusu inamaana bado dak 40 nzima ndege iondoke

Mzee akarudi nje baada ya kuelekezwa aende ofisi za kampun anayotaka kusafiri nayo ili wao ndo wampeleke pale apitishwe

Kufika ofisi ya fastjet pale eti wanagoma hawana nafasi ya kutoka hivyo mzee akate tiketi nyingine

Nilijikuta nawatukana matusi mpaka nikaondolewa na walinzi

Mtu yupo palepale uwanja wa ndege na bado muda wa kuondoka ndege anazuiwaje kuingia???

na hizi pesa tulizomkatia mzee mara mbili anashindwa kusafiri nani anazila?

Magufuli tusaidie hili jipu
vigezo na masharti havikuzingatiwa mkuu,hata mimi nilishawahi kuachwa na concord na sikurudishiwa hata centi tano
 
Ukiangalia kwa uhalisia sasa hivi Fastjet hawana bei nafuu nimewahi kupoteza ticket ya 245,000/- Safari ya kwenda tu Dar-mbeya(one way) baada ya kuchelewa ticket ikawa imepotea ukiangalia wanatudanganya sana.
Tofauti na Precision Air kipindi cha nyuma nilikata ticket 195,000/- baada ya kuchelewa nilichajiwa gharama ya 60,000/- kama gharama ya kuchelewa na kubadilisha ticket ambayo kimsingi niliiafiki .

Lakini hili la fastjet kucharge gharama kubwa alafu ticket hauwezi kubadilisha kwakeli wanatuibia sana.

wao wanajiita "BUDGET AIRLINE". Nadhali regulator sasa ndio mwenye jukumu la kufuatilia kama wanakidhi matakwa ya "BUDGET AIRLINE" services. Lakini wanatakiwa waadhibiwe na kuwepo na competition ya kutosha maana mimi naona kama wana monopoly ya aina fulani hivi. Taarifa niliyo ambiwa ni kuwa wakubwa wengi wana shares.
 
Naombwa kujuzwa hivi fastjet ni airline au charter company?
 
Rais wa Marekani huyooooo!
 

Attachments

  • downloadfile-23.jpeg
    downloadfile-23.jpeg
    94.3 KB · Views: 37
Kwa msaada zaidi peleka malalamiko yako FAIR COMPETITION COMMISSION UBUNGO. This are industry regulators and consumers protectors. Usisubiri magufuli afanye kila kitu wakati kuna waliopewa majukumu hayo.. fanya nilivyokuambia utaona matokeo yake
Pamoja sana mkuu
 
Wewe ndio jipu!, unatakiwa kutumbuliwa! pafyumu, vyuma unapeleka wapi? kufiwa na biashara wapi na wapi?
 
Boarding gate inafungwa dakika 40 kabla ya ndege kuondoka, ukichelewa kufika hapo ujue umechelewa hata kama kwingine umepita
 
hivi check in inaanzia wapi? unapovuka scanner au unapokaguliwa ticket?
Check in ni kabla ya yote, na kwa mashirika mengi ya ndege huduma hii unaifanya kwenye mtandao. Ukifika airport kazi yako ni kukabidhi mizigo na kuendelea na ukaguzi.
 
Ukiangalia kwa uhalisia sasa hivi Fastjet hawana bei nafuu nimewahi kupoteza ticket ya 245,000/- Safari ya kwenda tu Dar-mbeya(one way) baada ya kuchelewa ticket ikawa imepotea ukiangalia wanatudanganya sana.
Tofauti na Precision Air kipindi cha nyuma nilikata ticket 195,000/- baada ya kuchelewa nilichajiwa gharama ya 60,000/- kama gharama ya kuchelewa na kubadilisha ticket ambayo kimsingi niliiafiki .

Lakini hili la fastjet kucharge gharama kubwa alafu ticket hauwezi kubadilisha kwakeli wanatuibia sana.
Kwa gharama za ndege hapa nchini ni kubwa sana. Nauri ya kwenda kigoma kutoka Dar inalingana na nauri ya kwenda India! Hii yote imesababishwa na nchi kushindwa kufanya uwekezaji na hivyo viongozi wengi wasio na huruma na walio mafisadi na wabinafsi wanatumia chance hiyo kutuumiza
 
wao wanajiita "BUDGET AIRLINE". Nadhali regulator sasa ndio mwenye jukumu la kufuatilia kama wanakidhi matakwa ya "BUDGET AIRLINE" services. Lakini wanatakiwa waadhibiwe na kuwepo na competition ya kutosha maana mimi naona kama wana monopoly ya aina fulani hivi. Taarifa niliyo ambiwa ni kuwa wakubwa wengi wana shares.
PMM hakuna leseni ya budget airline au category hiyo kisheria bali ni business modal ambayo shirika linaamua kufanya kama mkakati wa kushindana! Regulator ataaingilia kama wataweka nauli za chini kuliko gharama za uendeshaji wakiwa na nia ya kuwaua wengine ili wabaki pekee yao ( predatory pricing) na kuwa na monopoly. Tatizo ni hilo la kukosa washindani na pia usisahau hali halisi ya watumiaji na ambao wangependa kutumia huduma hii, yaani umaskini! Hivyo anaweza kujiita budget airline na akafanya shughuli zake Kama conventional airlines au kwa kuchanganya business modals tofauti bila kuingiliwa na regulator as long as anakidhi matakwa ya leseni kibiashara
 
PMM hakuna leseni ya budget airline au category hiyo kisheria bali ni business modal ambayo shirika linaamua kufanya kama mkakati wa kushindana! Regulator ataaingilia kama wataweka nauli za chini kuliko gharama za uendeshaji wakiwa na nia ya kuwaua wengine ili wabaki pekee yao ( predatory pricing) na kuwa na monopoly. Tatizo ni hilo la kukosa washindani na pia usisahau hali halisi ya watumiaji na ambao wangependa kutumia huduma hii, yaani umaskini! Hivyo anaweza kujiita budget airline na akafanya shughuli zake Kama conventional airlines au kwa kuchanganya business modals tofauti bila kuingiliwa na regulator as long as anakidhi matakwa ya leseni kibiashara
Sorry read business model not modal
 
naomba nijuzwe wenye kujua , kuna jamaa yangu mmoja alienda kukata tiketi asubuhi, akatisha tiketi alikagua passport mchana ilipofika mida ya usafiri kwenye ukaguzi jamaa akamzuia, kisa cha kumzuia ni kwamba passport imechanika. mihuri ya yote inaonekana vizuri tu, ila jamaaa akamwekea ngumu hawezi kupanda ndege kwa passport ile, ila akitaka aende ubalozini akachukuwe hati ya dharula ya kusafiria. Jamaa ilibidi atafute msaada wa watu wa uhamiaji, wakamwambia passport haina tatizo, afisa uhamiaji kila akimuliza jamaa passport inamatatizo gani? yule mkaguzi anang'ang'ania hawezi kusafiri na hii passport. Cha kujiuliza kwanini walikubali kumkatia tiketi kama passport inamatatizo?
 
PMM hakuna leseni ya budget airline au category hiyo kisheria bali ni business modal ambayo shirika linaamua kufanya kama mkakati wa kushindana! Regulator ataaingilia kama wataweka nauli za chini kuliko gharama za uendeshaji wakiwa na nia ya kuwaua wengine ili wabaki pekee yao ( predatory pricing) na kuwa na monopoly. Tatizo ni hilo la kukosa washindani na pia usisahau hali halisi ya watumiaji na ambao wangependa kutumia huduma hii, yaani umaskini! Hivyo anaweza kujiita budget airline na akafanya shughuli zake Kama conventional airlines au kwa kuchanganya business modals tofauti bila kuingiliwa na regulator as long as anakidhi matakwa ya leseni kibiashara

Nashukuru sana. Mimi si mtalaam wa aviation industry, lakini conventional airline nyingi zinaruhusu kuchukua mzigo hadi kilo 20 na hata 40 na zaidi kwa international flights. Kwa uzoefu wangu naona budget airlines tu ndio haziruhusu kubeba mzigo na ukiwa nao unalipia. Lakini honestly speaking bei wanayo charge FASTJET si ya budget, na hivyo warudishwe kwenye za kawaida na wafuate taratibu hizo. Ndio maana bado narudi suala la regulator, vinginevyo walaji watazidi kuonewa sana. Tueleweshwe kama wao ni budget ni vigezo vipi wananchi wajue wazi.

Nasema hivyo kwa sababu nimewahi tumia sana budget airline na FASTJEt pia, lakini naona tofauti kubwa sana hasa kwa bei. Hata muda wa mteja kuweza nunua ticket afaidi nauli ni mrefu sana.
 
Kwa msaada zaidi peleka malalamiko yako FAIR COMPETITION COMMISSION UBUNGO. This are industry regulators and consumers protectors. Usisubiri magufuli afanye kila kitu wakati kuna waliopewa majukumu hayo.. fanya nilivyokuambia utaona matokeo yake
Sasa na wewe! Yaani hujui kabisa kwamba kama umeamua kutumia wingi tunasema "these are?". Tutumieni lugha yetu jamani hii ya kuja na meli tuachane nayo hatuiwezi!
 
Kwa gharama za ndege hapa nchini ni kubwa sana. Nauri ya kwenda kigoma kutoka Dar inalingana na nauri ya kwenda India! Hii yote imesababishwa na nchi kushindwa kufanya uwekezaji na hivyo viongozi wengi wasio na huruma na walio mafisadi na wabinafsi wanatumia chance hiyo kutuumiza[/
QUOTE]


Tumekosa uzalendo nilishawahi kusema humu kwamba ni jambo la aibu sana kwa nchi kama Tanzania kuruhusu shirika la kigeni kuweka base yake. Huku tukisema tunataka kufufua Atcl hapa tunajidanganya na haya ndio madhara yake. Ndio maana ndugu zetu Wakenya wanatucheka na kutudharau sana.

Sasa hv Fastjet ndio imekuwa Airtanzania alafu humu kuna watu wanisifu bila haya sijui ni lini sisi watanzania tutasimama wenyewe na kujivunia chetu.

Mimi nasubiri nione mzee magu atalitumbuaje hili jipu.
 
Nashukuru sana. Mimi si mtalaam wa aviation industry, lakini conventional airline nyingi zinaruhusu kuchukua mzigo hadi kilo 20 na hata 40 na zaidi kwa international flights. Kwa uzoefu wangu naona budget airlines tu ndio haziruhusu kubeba mzigo na ukiwa nao unalipia. Lakini honestly speaking bei wanayo charge FASTJET si ya budget, na hivyo warudishwe kwenye za kawaida na wafuate taratibu hizo. Ndio maana bado narudi suala la regulator, vinginevyo walaji watazidi kuonewa sana. Tueleweshwe kama wao ni budget ni vigezo vipi wananchi wajue wazi.

Nasema hivyo kwa sababu nimewahi tumia sana budget airline na FASTJEt pia, lakini naona tofauti kubwa sana hasa kwa bei. Hata muda wa mteja kuweza nunua ticket afaidi nauli ni mrefu sana.
PMM naelewa concerns zako, ila kama nilivyojaribu kuainisha tatizo ni la washindani dhaifu. Kama wako makini na huo upotoshaji wa fastjet wangetumia huo mwanya kwa kupata abiria zaidi na kuishikisha adabu fastjet. Tatizo bado fastjet ni reliable kuliko hao washindani wake otherwise huna haja ya kununua tiketi zake. Swala la kuchelewa na cancellation ya ticket yako ni muhimu watu wakaelewa kuwa hiyo tiketi ina masharti magumu na inakuwa ghali ukikiuka masharti hayo iwe kwa bahati mbaya au kupenda! Hivyo jiulize mara mbili kabla ya kukata tiketi yao na kujidhihirisha kuwa utamudu masharti yao. Kuwa budget au kutokuwa budget ni swala la ushindani na wewe mlaji kuamua unafaidika vipi na hao budget ukilinganisha na conventional business model!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom