Fastjet, mkiendelea na tabia hii, mtapoteza wateja

Fastjet, mkiendelea na tabia hii, mtapoteza wateja

We acha tu mi ilikua niondoke j2 ilopita saa sita mchana tukaja kuondoka sa moja na nusu jioni na hata hawajali... Anyway nadhani kwakuwa sahv wanaenda Nairobi inawezekana ndege ni chache... Kesho natakiea niondoke sa nne nasubiri tu simu yao hapa kuskia kama wataahirisha maana nshajiandaa vyovyote.. Si mbaya lakin bado wamejitahid kuleta mapinduzi hayo ni mapungufu ya kawaida
 
Mkuu Fastjet ni jipu linalijitegemea. Sasa hivi ukibook tiketi online wanatoza dola tano ili wakuwekee nafasi afu baada ya mda mfupi wanafuta booking afu vituo vyao vya kulipa kwa cash ni vichsche na hawataki kulipia kwa mtandao. Ni wahuni hao .
Siku hizi booking zao wanakupa dakika 12 tu kulipa kwa mpesa /tigo pesa
 
Duniani usafiri wa ndege ni usafiri salama na wafanyakazi wake ni watu wenye weledi wa hali ya juu na kumjali mteja.

Lakini ghafla shirika hili la ndege (Fastjet) wameamua kwa makusudi kuingiza uswahili katika biashara hii ikiwemo KUAHIRISHA/KUFUTA SAFARI bila taarifa za mapema, kuchelewa kupokea simu ya huduma kwa wateja (+255784108900) na kutokutoa majibu sahihi kulingana na tatizo la mteja, lugha mbovu kwa wateja.

Naiona Fastjet kama kampuni ya daladala kwa sasa.
@ C.T.U
Sote tunakibaliana na uzembe huo... la zaidi ni kuwa Hatuna ushindani ktk biashara za anga (aviation) Hivyo FastJET atatamba sana...
SERIKALI lazima ikaribishe mashirika ya ndege mengine haraka.... !!! pawepo na choices za usafiri!!!
 
Mleta mada nakupa pole Kama bado unapanda hiyo basi ya angani,
Nimepanda mara kadhaa kwenda South Africa yaani utafikiri nipo kwenye basi tu, kila kitu kinauzwa ndani ya ndege yaani hakuna utofauti utadhani Sio international route

Kiufupi fastjet si ndege ya kupanda labda waboreshe management yao ya sasa hivi la sivyo itafikia hatua watu hawatapanda kabisa ndege zao.
Mjirekebishe fastjet nyie ni kampuni ya nyumbani tunawategemea mfike mbali na kutanua anga za kuvuka Africa
Mbinu zimefanyika kuua precision ya mtoto wa nyumbani ili kupisha njia kwa fastjet and the like.
 
Pole mkuu, ndio mashirika ya kitanzania yanavyofanya kazi. Kauli ni hizi hizi '' network ipo down''; '' kuna matatizo ya kiufundi'';

Ila inaonekana wana wateja maana ile foleni pale kwenye ofisi zao mtaa wa Samora ipo kila siku..
 
Mkuu upo sahihi SAA wamepewa siku 90 na serikali yao wawe wame recover kutoka katika hali mbaya waliyonayo maana vitabu vyao vya Accounts 2013/2014 vinaonesha hasara zaidi ya $ milion 100.Management wametoa sababu ya kushuka kwa thamani ya rand against $ kwa 34% kwa kuanzisha safari ndefu kama za beijin,dakar na abudhabi ambazo wamefanya kwa hasara kwa kipindi icho..SAA wanachangia 0.3% ya GDP ya South Africa. Wanategemea kuungana na kamapuni ya Etihad ili kupata rescue.kama serikali hawatawapatia kiasi kinachotakiwa..
 
mi nimelipia kwa mpesa jumatatu wamechukua hela alafu ticket hawajanipa telling me eti system imesumbua so tunakurudishia hela, hadi leo bado naisubiria, sooon nawapeleka mahakamani, i have the time na resources kabisaa
 
Fastjet nawadai refund yangu toka mwezi wa 11 kwa tiketi ya kusafiri mwezi wa 3, wana bahati nipo nje ya nchi vinginevyo ningetimua kila kitu hapo ofisin kwao mpaka wanilipe mmama zao
 
Siku hizi booking zao wanakupa dakika 12 tu kulipa kwa mpesa /tigo pesa
Sasa dakika 12 huu si ni ile wilaya anayotoka Ngeleja? Nini maana ya booking? Huu ni mzaha kabisa.
Halafu hui tabia ya kysema wanam refund mtu baada ya siku tatu ni kucheza na hela na mipango ya watu.
Kama wanaona hela nu kitu chepesi hivyo mbona wao booking zao ni za muda mchache tu then wanataka walipwe?
 
Mbinu zimefanyika kuua precision ya mtoto wa nyumbani ili kupisha njia kwa fastjet and the like.
Hao nao ndiyo usiwataje kabisa. Hao hakuna aliyewaua bali wamejifia wenyewe, wanatoza manauli makubwa ajabu lakini vindege wanavyikupajia vinechakaa na ni vidogo, ukiwa angani kelele zote za injini zinakurudieni ndani.
 
Tigo pesa na
Siku hizi booking zao wanakupa dakika 12 tu kulipa kwa mpesa /tigo pesa
mpesa wanadai system mbovu dakika 12 unazopewa ni za kulipa kwa kutumia kadi za elektroniki mkuu au la ufanye booking ya simu na ukalipie kwa wakala au wakufanyie reserve kwa $5
 
Duniani usafiri wa ndege ni usafiri salama na wafanyakazi wake ni watu wenye weledi wa hali ya juu na kumjali mteja.

Lakini ghafla shirika hili la ndege (Fastjet) wameamua kwa makusudi kuingiza uswahili katika biashara hii ikiwemo KUAHIRISHA/KUFUTA SAFARI bila taarifa za mapema, kuchelewa kupokea simu ya huduma kwa wateja (+255784108900) na kutokutoa majibu sahihi kulingana na tatizo la mteja, lugha mbovu kwa wateja.

Naiona Fastjet kama kampuni ya daladala kwa sasa.
kibaya zaidi ni kuwa wao ukiahirisha safari hawakubali na hela hawarudishi, ati wao wanaahirisha kwa sababu za kiusalama kwa binadamu kuwa wakisafiri watahatarisha maisha, yaani wanafanya wizi wa waziwazi kabisa kisa tu tiketi wameandika ni non-refundable, mimi najipanga soon nitapiga hela kupitia hawa watu, tutafikishana mahakamani kama hawa Mamlaka ya ndege wameamua kujifanya hawaoni
 
Hio ni low cost Airline what do you expect? A 5 star qatar airways service? Wangekuwa wanaruhusiwa ata mabusati wangeeka badala ya seats
 
Wengi wetu tunadhani kuingia kwenye biashara kubwa ni LELEMAMA; Kila kazi inahitaji kufuata KANUNI na TARATIBU za kufuata ili kuweza kuduma na kuwa RELIABLE, vinginevyo tutasikia inakuwa HISTORIA.
Wengi wetu sio wote kama ni Watanzania tumeshasikia juu ya huduma na mashirika yaliyovuma sana kwa nguvu ya kiutendaji na kiuchumi enzi za miaka ya 1970's na 80's ila leo hayapo, km TAZARA, NASACO, AIR TANZANIA, na hata TANESC0 enzi hizo, bila kusahau NATIONAL PANASONIC MATSUSHITA sina maana hii ya Japan (ni ile iliyokuwa Nyerere Rd, zamani Pugu Rd karibu na TCC.)
Leo hii havipo kabisa imebaki historia tena ya kutafuta.
Mafanikio ya kudumu iwe kwa kiwango cha mtu binafsi, jumuia, nchi au hata kampuni huhitaji NIDHAMU isiyoteteleka na ya kudumu itakayofanywa kama mtindo wa maisha ya kila siku au utamaduni wa watu/mtu/taasisi husika.
Vinginevyo, tutafanya mambo kwa kukurupuka au kuiga au kuigilizia ambayo hupelekea kushindwa vibaya sana na kupotea kabisa katika ulinwengu wa tasnia husika.
 
hii ni shida unabook on line wanacharge dola 5 ukienda kununua tikete kwa wakala elfu tano tsh. ukiingiia kwenye ndege unauziwa vitu wanaboa sanaa
Hivi ninyi mnaosafiri kutoka Mwanza muja Dar ama Dar Mbeya, mnahitaji kula nini huko hewani kwa muda wa saa moja mnayokuwa huko? Cheap flights zote huwa unajinunulia kila kitu ukiwa ndegeni. Precision wanatoa korosho za buku na kiji soda kidogo, lakini bei kubwa. Kipi bora?
 
Back
Top Bottom