Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Arusha sasa hivi ukitembea mjini kwenye kuta utakuta matangazo yanasema kuanzia tarehe 4/5/2011 siku ya tangazo hilo lilipowekwa hadi kufikia siku 60 mtu au watu au vikundi vilivyojihusisha kwa njia moja au nyingine kumsingizia au kumtuhumu kijana wao kwa ile kesi iliyokua inamkabili mfanyabiashara maarufu wa mawe aina ya Tanzanite jijini Arusha mwenye asili ya Kimeru ambaye alituhumiwa kwa kesi ya kutmia silaha na unyang'anyi na akakaa jela kwa muda kama wa miaka 5 hivi lakini mahakama ikamuachia baada ya kukata rufaa na akashinda kesi hiyo. Sasa familia ya mfanyabiashara huyo imejiandaa kuvunja chungu kwa yeyote aliyejihusisha kwa kumsingizia kijana wao! jamani hizi ndizo habari nyepesinyepesi na mseto kutoka jijini Arusha nawatakia jumapili njema.