son of the most high-01
Member
- Nov 14, 2023
- 5
- 66
Sijui nifanyaje hapa, ni miaka kumi na sita sasa tangu baba yangu afariki.
Baba kuna kosa alifanya enzi za uhai wake. Kosa hilo limesababisha mateso na dhiki kuu hii leo kwa familia nzima. We are paying heavy price.
Nimefikiria nimtafute aliyekosewa nijaribu kumuomba msamaha, naona hii ndio njia pekee iliyobaki. Tumejaribu kila njia kujiokoa hapa tumeshindwa, labda baba angekuwepo ingekuwa rahisi, lakini sijui nitampata wapi na kama ikiwa bado yuko hai.
Jamani jitahidini sana kuwatendea watu mema katika haya maisha. Hata ikiwa hauwezi kuwatendea mema basi usiwatendee mabaya, usiwaumize watu.
Unajua unaweza ukajiona mjanja hii leo kwa kufanya jambo flani lakini watoto wako wakaja kulipa gharama kubwa.
Wema na ubaya ni akiba.
Baba kuna kosa alifanya enzi za uhai wake. Kosa hilo limesababisha mateso na dhiki kuu hii leo kwa familia nzima. We are paying heavy price.
Nimefikiria nimtafute aliyekosewa nijaribu kumuomba msamaha, naona hii ndio njia pekee iliyobaki. Tumejaribu kila njia kujiokoa hapa tumeshindwa, labda baba angekuwepo ingekuwa rahisi, lakini sijui nitampata wapi na kama ikiwa bado yuko hai.
Jamani jitahidini sana kuwatendea watu mema katika haya maisha. Hata ikiwa hauwezi kuwatendea mema basi usiwatendee mabaya, usiwaumize watu.
Unajua unaweza ukajiona mjanja hii leo kwa kufanya jambo flani lakini watoto wako wakaja kulipa gharama kubwa.
Wema na ubaya ni akiba.