Falling in love...

Falling in love...

I guess bado nafundisha bila kuitwa mwalimu..

Hehehehe niwe naandaa mitihani nini kabisa?!
Lo! Mitihani Hapana, Kwa Umri huu mambo ya kuzungusha hayafai! Si unajua zile story tunazowazingua nyumbani? Watashtuka, Kuonekana kilaza uzeeni no!! Please ! Confidence itashuka.
 
Hahahaha GeeCee namba 8 wewe inakuhusu?!
Mimi namba 3 hainisumbi sana..sema kuna wakati inabidi ikae chonjo kidogo.

Alafu namba 12 mbona rahisi sana?!Hata kumwambia asante kwakunipikia/nipa kitu fulani inatosha kabisa.

Ah.. Lizzy..
Kuna wadada ambao,hupenda kuonekana mbele za watu kwamba wanapendana na wenzi wao... Wakati ndani ya mahusiano,wao ndiyo pasua kichwa hatari!

Atakiuka ile no ngapi ya kulazimisha kumbadili mwenza tabia zake...

Anapenda kumkosoakosoa mwenzi... "Yaani pale wageni walipokuja,we ulifanya hivi..sio vizur"i.."ulichangamka sana","..ulisema asante kwa ile zawadi utadhani tulikuwa na shida nayo sana",mwingine anasema kabisa "pale uliniboa!"..n.k.

Sasa pata picha,mnaishi hivyo,na labda mnaalikwa kwenye events tofauti,hapo ataforce kukumbatia aonekane na wanawake wenzake,kana kwamba love iko hot vibaya mno! Akuchezee vidole,akuegemee wakati unaongea na watu... Yaani full kujiadvertize,wakati mkirudi ndani kwenu hali inakuwa hiyo! Na mnaishi hivyo miaka kadhaa...

Pata picha..
 
Wagumu wagumu haswa Naima.

Tatizo ni mashindano...watu hua wanasahau kwamba mtu uliye nae kwenye mahusiano sio mshindani wala adui bali ni mwenzi. Matokeo yake maneno kama POLE...AHSANTE...SAMAHANI hayatolewi kwasababu ADUI ATAONA AMESHINDA.

Hili bonge la pointi...

Shida ni kwamba tunaishi kama vile tunshindana..
 
Nauliza wewe kiswahili umesomea wapi? Vipi utaendelea kumpenda mtu bila ya wewe kumuonyesha unampenda.

Anaongelea jambo lililokuja natarally la kumpenda mwenza... Hilo lisipotee,liendelee kwa njia hizo hapo juu..

Wewe unaonekana unaongelea kitu cha kupangilia kuwa nimwoneshe nampenda kwa kuwa wanaopendana huonekana wakifanya mambo fulani,nami niyaige hayo aone nampenda..

Umeona tofauti...?
 
I have to say this, ni mhimu kumjua mtu unayeingia naye kwenye mahusiano. Mjue mwenzako vizuri na ukimkubali basi ufahamu pia namna ya kuishi naye, kumshirikisha na kujua kuwa ipo siku moja mwenzako anaweza asiwe alivyo!

Kingine ni kuwa na uwanja mpana wa kufikiria (exposure na kudadisi mambo), don't constrain yourself to only one type of life, try different kinds of life at different stages of your relationships iwe kwenye uchumba, ndoa au kabla ya kupata watoto na baada ya kupata watoto, inasaidia kujiona mnapendana kila wakati!!. Vitu kama kuwa kuaminiana, kumpenda, kuheshimiana na vingine vitaendeleakuwepo kutokana na mnavyoishi.
 
Anaongelea jambo lililokuja natarally la kumpenda mwenza... Hilo lisipotee,liendelee kwa njia hizo hapo juu..

Wewe unaonekana unaongelea kitu cha kupangilia kuwa nimwoneshe nampenda kwa kuwa wanaopendana huonekana wakifanya mambo fulani,nami niyaige hayo aone nampenda..

Umeona tofauti...?
Hakuna love ya kulazimisha hata mimi naongelea naturally kama navyo jua...ukipenda huwezi kuchukia na ukichukia huwezi kupenda, sasa sijui tuseme nini ngoja tuombe msaada :biggrin:
 
Last edited by a moderator:
Lizzy, watu wanapishana.
Kuna mtu unaweza kumpenda hivo akaona kama you are suffocating him...
Wengine wanapenda uwaachie nafasi kubwa sana.
sio kila mara umwambie unampenda, au kila mara umkumbushe how good he is to you.
It increases the pressure... don't do too much, keep it very very simple.
Nadhani pamoja na mmoja wao kujitahidi as you describe hapo juu
Wapensi wajaribu zaidi kujenga pamoja framework inayo ruhusu mapenzi kujitokeza.
Only through joint efforts will they succeed.
Mfano kama wanapenda kwenda out, wahakikishe wanaenda out.
Kama wana penda kuangalia movies nyumbani wahakikishe wanaangalia.
At those moments when they are both doing what they like doing together love will just blossom.
 
Enzi za Mwl. Haya maishu ya kitchen party,cjui bed party, masomo kama haya mitandaoni hayakuwepo.. Lakin wazee wetu walidumu ktk mahusiano kwa raha...
Sasa hii dunia ambayo imeja kila aina ya MKUFUNZI ndo taaabu... ktk Mahusiano..... WHY? Naongea na ww Lizzy.
 
Well done Mchumbaangu Lizzy.
Halaf mbona sjaona kapengele ka sex therapy? umeanza uchoyo sio?
 
Falling in love...
Kabla ya kumuweka mtu mikononi sauti yake tu inaburudisha akili, moyo na mwili...akiongea unatamani asimalize. Kila anachosema kinakukaa akilini, utani wake unachekesha na maneno matamu yanakuingia. Mkifikia kwenye kugusana, kushikana mikono tu kunatoa raha ya kipekee. Ukimuwaza/fikiria/kumbuka tabasamu na utulivu moyoni vitawala.
Ukisikia kakuongelea sehemu basi raha tupu alimradi kakuongelea kwa uzuri.

1. Get him/her to miss you...and you to miss him/her.
2. Let him/her be who he/she is.
3. Be easy on them.
4. Talk to him/her about NOthing..SOMEthing and EVERYthing.
5. Take him/her NOwhere..SOMEwhere and EVERYwhere.
6. Mpe nafasi....
7. Ongoza..
7. Usiwe mlalamikaji sana.
8.Kumbuka....
9. Be a team player...
10. Be MORE of a lover and LESS of a mother/father.
11. Shukuru...
12. Mjulishe/mkumbushe umuhimu wake kwako.
13......
MPENDE...
MHESHIMU..
MUAMINI...
MTHAMINI...
MJALI...nk
14. USIJARIBU na kama tayari ACHA kumlinganisha na wanaume/wanawake wengine unaowafahamu/kutana nao unless yeye unamuweka juu. Kama hao wengine unawaona bora sana utaishia kumuona wako si lolote...si chochote.
15. SAMEHE (Zinagatia pia No.6&8 juu): Kwa kuwa hakuna mkamillifu, ukikosewa samehe (ikitegemea na aina ya kosa). Sio tena makosa madogo ya kawaida unayajengea mnara wa kumbukumbu.
16. JIAMINI (Zingatia pia 13 juu): Mbali na kumwamini mwenzako, inakupasa na wewe kujiamini pia. Isipokuwa katika mazingira tete, elewa kuwa yuko na wewe kwa sababu amekuchagua wewe. Kukosa kujiamni kunaweza kuzua na kuzaa wivu kupindukia ambapo ukizidi, unaweza kuwa kero na sababu ya kukorofishana.
17. WIVU (Zinagatia 16 juu): Ingawa inasemwa na ni hakika kuwa wivu ni ishara ya mapenzi, kuwa na kipimo cha wivu wako. Na zaidi isiwe wivu wa kutomwamini bali kumwonesha tu kuwa unamjali (bila ya kumkosesha raha na kumwadhiri).
18. TATUENI MATATIZO YENU WENYEWE: Isiwe tena suala dogo mnalitafutia washenga. Jengeni utamaduni wa kuzungumza, kujadili na kutatua matatizo yenu bila ya kuwashirkisha watu wa nje. Na pale inapobidi, washauri hao wawe wazazi/walezi wenu kabla ya shoga wala rafiki.
...........
...........
...........
 
15. SAMEHE (Zinagatia pia No.6&8 juu): Kwa kuwa hakuna mkamillifu, ukikosewa samehe (ikitegemea na aina ya kosa). Sio tena makosa madogo ya kawaida unayajengea mnara wa kumbukumbu.
16. JIAMINI (Zingatia pia 13 juu): Mbali na kumwamini mwenzako, inakupasa na wewe kujiamini pia. Isipokuwa katika mazingira tete, elewa kuwa yuko na wewe kwa sababu amekuchagua wewe. Kukosa kujiamni kunaweza kuzua na kuzaa wivu kupindukia ambapo ukizidi, unaweza kuwa kero na sababu ya kukorofishana.
17. WIVU (Zinagatia 16 juu): Ingawa inasemwa na ni hakika kuwa wivu ni ishara ya mapenzi, kuwa na kipimo cha wivu wako. Na zaidi isiwe wivu wa kutomwamini bali kumwonesha tu kuwa unamjali (bila ya kumkosesha raha na kumwadhiri).
18. TATUENI MATATIZO YENU WENYEWE: Isiwe tena suala dogo mnalitafutia washenga. Jengeni utamaduni wa kuzungumza, kujadili na kutatua matatizo yenu bila ya kuwashirkisha watu wa nje. Na pale inapobidi, washauri hao wawe wazazi/walezi wenu kabla ya shoga wala rafiki.
...........
...........
...........


waaohh..!
 
Back
Top Bottom