Faida ya maharage ya soya

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,315
33,108
soya.gif




Soya ina vitamin A,B,C,D,E na K. hakuna chakula duniani chenye vitamini nyingi kama hiki, soya ina protini ya ajabu na mafuta pia ambayo huifanya kuwa chakula pekee na safi. Uboreshaji wake wa afya ulifanya watu wa zamani kuitambua kama chakula cha pekee kwao ikawa chakula kizuri cha mbadalaambacho walikitumia badala ya nyama, maziwa na mafuta (butter) pamoja na mayai.walitumia watu wa rika zote, na wagonjwa pia, ilitumiwa pia kulisha ndama, ng’ombe, na kwa kufanya hivyo 90% ya ugonjwa wa kifua kikuu ulipungua kwa ndama. Soya ina mambo mengi na misaada katika miili ya wanadamu.




KAZI YA SOYA MWILINI


Soya ina glycerine na fatty acid ambayo inasaidia kazi nzuri ya ufanyaji kazi wa ubongo na maini. Pia ina chakula kizuri kwa neva ya ufahamu iliyochoka maana ina licitini, hii huifanya kuwa chakula kizuri sana kwa wazee.




PROTINI YAKE


Kilogram 1 ni sawa na protein inayopatikana katika mayai sabini.
Kilogram 1 ni sawa na protein inayopatikana katika nyama kilo 3
Kilogram 1 ni sawa na protein inayopatikana katika maziwa lita 2.




MATUMIZI


Soya hutengenezwa karanga za kutafunwa
Soya hutengenezwa chakula cha nyama.
Soya hutengenezwa maziwa mazuri sana
Unga wa soya hutumiwa kwa:-
Kukaangia chakula
Kupikia ugali
Kupikia chapati na mikate.




MATAYARISHO


Weka maharage ya soya kwenye maji, kwa masaa 24. kisha yaanikwe na kusagwa ili kupata unga .


SOYA HUTIBU YAFUATAYO


Hutibu vidonda vya tumbo
Kisukari
Saratani
Tumbo
Figo
Ini n.k


MAELEZO ZAIDI KUHUSU MATAYARISHO NA MATUMIZI YA MAHARAGE YA SOYA


Ikumbukwe, kama tulivyoona hapo juu kwamba, maharage ya soya ni chanzo kizuri sana cha protein ifaayo kwa ukuzi na ustawi wa binadamu. Hata hivyo ni vyema izingatiwe kuwa, ndani ya maharage hayo vimo viini ambavyo visipodhibitiwa huudhuru mwili wa mlaji, viini hivyo vinajulikana kama “Anti Nutritional Factor” mojawapo na maarufu ni vile viitwavyo “Trypsin initiator” ambavyo vinapotumiwa huzuia protein isitumike mwilini mwa mlaji. Salama ni kuhakikisha kuwa hizo “Anti – Nutritional Factors” zimeangamizwa, nazo huweza kuangamizwa kwa njia ya joto kwa kuchemsha au kukaanga. Kwa matokeo mazuri, kabla ya kuchemshwa au kukaanga ni vyema kuyaloweka majini – kikombe kimoja cha soya katika vikombe 5 vya maji kwa muda wa masaa 6, kisha chemsha kwa dakika 30, yakaushe barabara ndipo yasagwe
ZINGATIA UWIANO UFUATAO


1:5 kwa kuyaloweka (soya : maji)
1:9 kwa ajili ya uji (unga wa soya : unga mwingine)
1:3 kwa wjili ya maziwa (unga wa soya : maziwa)


KWA MAZIWA


Baada ya kukoroga mchanganyiko huo, chujavyema na kitaambaa safi. Kimiminika kinachopatikana ndiyo maziwa ya soya. Ni vyema maji yatumiwe yaliyo salama baada ya kuchujakiasi.


Kukaanga maharageya soya yaliyolowekwa kwa masaa 6 hadi yanapo kuwa na rangi kama ya majani makavu (brown) kuangamiza trypsin initiators. Ikiwa maharage ya soya yasiyolowekwa yamekaangwa hadi kuwa na rangi kama ya majani makavu (brown) trypsin initiators huwa imeangamizwalakini protini huwa pia imedhurika. Hivyo salama na uloweke kwa masaa 6 kabla ya kukaanga, tumia moto kidogo ili usiyaunguze.


MUHIMU


Ili kuandaa unga wa soya wenye mwonjo wa lishe unaokubalika, tumia maharage ya soya mazima kabisa.
 
leo naenda kununua kilo moja ya soya na nitayachemsha kama maharagwe then nitayaunga kwa nyanya, hoho, kitunguu, nyanya chungu. nadhani itakuwa mboga safi...... mnaonaje hapo wakuu?? karibuni
 
leo naenda kununua kilo moja ya soya na nitayachemsha kama maharagwe then nitayaunga kwa nyanya, hoho, kitunguu, nyanya chungu. nadhani itakuwa mboga safi...... mnaonaje hapo wakuu?? karibuni
Mboga ya kutosha na mimi nitakuwa mgeni wako unifungulie mlango.
 
leo naenda kununua kilo moja ya soya na nitayachemsha kama maharagwe then nitayaunga kwa nyanya, hoho, kitunguu, nyanya chungu. nadhani itakuwa mboga safi...... mnaonaje hapo wakuu?? karibuni

Hautaweza kula. Ni mabaya haina mfano ukiamua kuyapika kwa namna ulivyoeleza. Ili ujifunze vizuri na usinione muongo pia usipate hasara, pika kikombe kidogo kimoja. Matokeo tujuze.
 
soya.gif




Soya ina vitamin A,B,C,D,E na K. hakuna chakula duniani chenye vitamini nyingi kama hiki, soya ina protini ya ajabu na mafuta pia ambayo huifanya kuwa chakula pekee na safi. Uboreshaji wake wa afya ulifanya watu wa zamani kuitambua kama chakula cha pekee kwao ikawa chakula kizuri cha mbadalaambacho walikitumia badala ya nyama, maziwa na mafuta (butter) pamoja na mayai.walitumia watu wa rika zote, na wagonjwa pia, ilitumiwa pia kulisha ndama, ng'ombe, na kwa kufanya hivyo 90% ya ugonjwa wa kifua kikuu ulipungua kwa ndama. Soya ina mambo mengi na misaada katika miili ya wanadamu.




KAZI YA SOYA MWILINI


Soya ina glycerine na fatty acid ambayo inasaidia kazi nzuri ya ufanyaji kazi wa ubongo na maini. Pia ina chakula kizuri kwa neva ya ufahamu iliyochoka maana ina licitini, hii huifanya kuwa chakula kizuri sana kwa wazee.




PROTINI YAKE


Kilogram 1 ni sawa na protein inayopatikana katika mayai sabini.
Kilogram 1 ni sawa na protein inayopatikana katika nyama kilo 3
Kilogram 1 ni sawa na protein inayopatikana katika maziwa lita 2.




MATUMIZI


Soya hutengenezwa karanga za kutafunwa
Soya hutengenezwa chakula cha nyama.
Soya hutengenezwa maziwa mazuri sana
Unga wa soya hutumiwa kwa:-
Kukaangia chakula
Kupikia ugali
Kupikia chapati na mikate.




MATAYARISHO


Weka maharage ya soya kwenye maji, kwa masaa 24. kisha yaanikwe na kusagwa ili kupata unga .


SOYA HUTIBU YAFUATAYO


Hutibu vidonda vya tumbo
Kisukari
Saratani
Tumbo
Figo
Ini n.k


MAELEZO ZAIDI KUHUSU MATAYARISHO NA MATUMIZI YA MAHARAGE YA SOYA


Ikumbukwe, kama tulivyoona hapo juu kwamba, maharage ya soya ni chanzo kizuri sana cha protein ifaayo kwa ukuzi na ustawi wa binadamu. Hata hivyo ni vyema izingatiwe kuwa, ndani ya maharage hayo vimo viini ambavyo visipodhibitiwa huudhuru mwili wa mlaji, viini hivyo vinajulikana kama "Anti Nutritional Factor" mojawapo na maarufu ni vile viitwavyo "Trypsin initiator" ambavyo vinapotumiwa huzuia protein isitumike mwilini mwa mlaji. Salama ni kuhakikisha kuwa hizo "Anti – Nutritional Factors" zimeangamizwa, nazo huweza kuangamizwa kwa njia ya joto kwa kuchemsha au kukaanga. Kwa matokeo mazuri, kabla ya kuchemshwa au kukaanga ni vyema kuyaloweka majini – kikombe kimoja cha soya katika vikombe 5 vya maji kwa muda wa masaa 6, kisha chemsha kwa dakika 30, yakaushe barabara ndipo yasagwe
ZINGATIA UWIANO UFUATAO


1:5 kwa kuyaloweka (soya : maji)
1:9 kwa ajili ya uji (unga wa soya : unga mwingine)
1:3 kwa wjili ya maziwa (unga wa soya : maziwa)


KWA MAZIWA


Baada ya kukoroga mchanganyiko huo, chujavyema na kitaambaa safi. Kimiminika kinachopatikana ndiyo maziwa ya soya. Ni vyema maji yatumiwe yaliyo salama baada ya kuchujakiasi.


Kukaanga maharageya soya yaliyolowekwa kwa masaa 6 hadi yanapo kuwa na rangi kama ya majani makavu (brown) kuangamiza trypsin initiators. Ikiwa maharage ya soya yasiyolowekwa yamekaangwa hadi kuwa na rangi kama ya majani makavu (brown) trypsin initiators huwa imeangamizwalakini protini huwa pia imedhurika. Hivyo salama na uloweke kwa masaa 6 kabla ya kukaanga, tumia moto kidogo ili usiyaunguze.


MUHIMU


Ili kuandaa unga wa soya wenye mwonjo wa lishe unaokubalika, tumia maharage ya soya mazima kabisa.

MZIZIMKAVU; AHSANTE SANA KWA POSTS ZAKO AMBAZO ZIMELENGA KUTUSAIDIA NA KUTUEPUSHA NA MATATIZO MBALIMBALI YA MAGONJWA.

USIKUTE KUNA MTU ATATOKEA HAPA NA SOURCE UNAFIKIRI TUNAANDIKA THESIS, WEWE USIKATISHWE TAMAA NA WALE WANAOPENDA KUKOSOA HATA JAMBO ZURI. KWANI HAO LAZIMA WAWEPO KTK JAMII YOYOTE ILE. WEWE ENDELEA KUTUPA MAMBO KAMA NI MAZURI TUTACHUKUA NA KAMA NI MABAYA TUTAYAACHA. KWANI UKIWA WEWE SOURCE KUNA TATIZO? AU SOURCE MPAKA IWE MZUNGU? EBU TUACHE KUWAKATISHA TAMAA WENZETU WENYE MOYO WA KUSAIDIA JAMII KAMA MZIZIMKAVU ANAVYOFANYA. Hongera sana na Mungu azidi kukutia nguvu hata mwakani uzidi kutushushia mambo ya maana hapa.
 
kaka mzizi je yatosha kuyaloweka maharage ya soya kilo 1 kwa lita 9 za.maji kwa masaa 6 kisha kuyaanika na kuyasaga bila kuyatoa maganda?
 
Back
Top Bottom