Mondoros
JF-Expert Member
- Aug 29, 2015
- 629
- 472
Dangote labda abadilike ndio tutaweza kufaidi uwepo wake hapa Tanzania, ila kwa jinsi alivyo na ninavyomfahamu..kwa sasa kuondoka kwake ni nafuu kwa Watanzania na Taifa.
Yule bwana hawezi kufanya biashara bila utapeli hata mfanyakazi wake wa chini kabisa anajua. Jamaa anaingia mahali kwa lugha tamu sana na ahadi kibao, lakini si mtu yule.
Wapo wanaosema kuhusu ajira za watanzania walioko pale, ni hivi wafanyakazi wataalamu walioko pale ni wale waliokuwa kwenye viwanda vingine vya cement vilivyokuwa vinawalipa vizuri ila baada ya kusikia tishio la ujio wa likiwanda kubwa ambalo lingepewa gas, exemption ya kodi n.k likapunguza bei ya cement viwanda hivyo vingekufa kwa kushindwa kujiendesha,
Hatua mojawapo zilizochukuliwa na viwanda bora kama vile Twiga na vingine ni kupunguza wafanyakazi kwa kiasi kikubwa ambao wengi walienda Dangote kulipwa ujira mdogo sana maana yeye Dangote anatumia management ya Wahindi.
Kule Nigeria alianza biashara zake kwa style ya kuwahonga viongozi wakuu na wakampa excemption ya kodi, matumizi ya barabara hovyo na vitu vingine akashusha bei ya Cement, viwanda vingine vikafa akabaki yeye mwenyewe akishikilia kama 90% ya soko la cement na Lafarge kama chini ya 10% vingine vilikufa baada ya kuhakikisha kwamba ameviua akapandisha bei ikarudi kama zamani.
Hivyo ndivyo alitaka kufanya Tanzania, JK alimpa maeneo makubwa sana, mpaka na eneo la kujenga bandari yake binafsi, jambo ambalo kwa maoni yangu naona ilikuwa hatari hata kwa usalama wa nchi.
Eneo lililojengwa kiwanda na mining lilikuwa la vijiji vitano, ni eneo kubwa ambalo lilikuwa mali ya wananchi, Dangote kwa kushirikiana na viongozi wa serikali ya awamu ya nne waliwatapeli wale wazee kwa kuwapa vitu vidogo vidogo na ziara ya kwenda kuhiji kwa wazee wachache pamoja na laki tano tano na ahadi kibao wakabariki kuiacha ile ardhi na wale wazee wakatumika kuwashawishi wengine wakaingia kingi.
Mara kadhaa nilikuwa nikiwaona hawa wazee wanaojiita wenyeviti wa vijiji vile wakiambaa ambaa pale nje ya kiwanda cha Dangote wakitapeli watu kwa ahadi ya kuwaunganishia vibarua kiwandani wakati hata wao hawana ruhusa ya kuingia ndani ya kiwanda, wazee wamepigika wanajuta tu kimoyo moyo.
Niliwahi kujaribu kuongea na mmoja wao ambaye alikuwa mwenyekiti wa wenyeviti wakati huo nikiwa kiongozi wa chama cha wafanyakazi hapo Kiwandani, nilipomuuliza sababu ya wao wazee kugawa ardhi bure kwa Dangote aliniambia kwamba wao waliamini Dangote si mfanyabiashara ni Alhaji kwa hiyo walitoa ardhi kwa Alhaji ili ajenge kiwanda kiwasaidie watu..
Nilishangaa sana, lakini kilichonifurahisha ni kwamba wanajuta maana zaidi ya laki tano na ziara ya Mecca hawajafaidika tena kwa namna walivyotarajia.
Mtindo wa ufanyaji kazi wa Dangote ni wa kitapeli tapeli tu, anatapeliwa kuanzia mfanyakazi wake wa chini mpaka Rais na mawaziri wakiingia kingi wanatapeliwa.
Kule Nigeria, ana kiwanda kikubwa Four kiln lines kwenye state ya Obajana na kingine Ibese, wafanyakazi zaidi ya 60% ni wahindi, wanaishi vizuri kila kitu wanachotumia ni tofauti na weusi, magari, nyumba za kuishi n.k ni tofauti kabisa.
Wahindi wanaletwa wakiwa hawajui kitu kabisa wanafundishwa na weusi (wanigeria) halafu wakishajua wanawasimamia weusi, wanawanyanyasa sana waafrika, pale ndipo nilipojua kwamba Tanzania ni nchi nzuri sana na siku zote nawambia ukitaka kujua uzuri wa nchi yetu Tanzania nenda Nigeria. Hususanu kufanye kazi kwa Dangote.
Wakati Dangote anafungua kiwanda Tanzania, alikuwa anaahidi kuajiri watanzania lakini ukweli ni kwamba alikuwa ameandaa makontena ya wahindi kuja Tanzania kama ilivyo Nigeria, thanks to God Magufuli akaingia Madarakani.
Wale wahindi wachache waliokuwepo walichukia sana wakaanza hata kukuza mambo au kutunga uongo wakiilaumu Serikali ati kwa kuweka vikwazo vingi, wakati mwingine wanamdanganya Dangote kuhusu Serikali yetu na Watanzania ili wao wapate faida. Ninao ushahidi wa mambo baadhi ambayo kwa makusudi kabisa management ya kihindi ilikuwa ikimdanganya Dangote kwa faida yao.
Mojawapo ilikuwa ni ubora wa makaa ya Mawe ya Tanzania, tulikuwa na vijana wetu maabara pale, hata mimi niliposikia kwamba makaa yetu ya mawe yana quality ya chini niliumia sana niliwauliza wahandisi wetu waliokuwa maabara wakasema ni uongo.
Hiyo ilikuwa mbinu ya wahindi kufanya biashara na makampuni ya South Afrika kwa faida yao huku wakichafua bidhaa zetu.
Lingekuwa jambo la ajabu sana kama serikali ingekubali uhuni huo, nawapongeza sana Mawaziri hawa wa awamu ya tano kwa kutumia elimu yao vizuri kuchunguza hilo kwa sababu hata enzi zile tulikuwa tuwaeleza serikali kila tunapopata nafasi lakini enzi ya awamu ya nne ilikuwa enzi ya aina yake. tulionekana wapuuzi au maskini wanoko.
Watanzania tunapopinga au kutetea ni vema tukatafuta ukweli kwanza, Dangote industries ukiisikia kwenye vyombo vya habari utaona ni mkombozi kwa watanzania, lakini kwa namna ilivyo na inavyotaka ifanyiwe ni hatari sana kwa taifa.
Tumshukuru sana Rais na serikali kwa msimamo wake. Dangote hana tofauti na akina Carl peters wa zamani labda abadilike.........
Itaendelea wiki ijayo
Yule bwana hawezi kufanya biashara bila utapeli hata mfanyakazi wake wa chini kabisa anajua. Jamaa anaingia mahali kwa lugha tamu sana na ahadi kibao, lakini si mtu yule.
Wapo wanaosema kuhusu ajira za watanzania walioko pale, ni hivi wafanyakazi wataalamu walioko pale ni wale waliokuwa kwenye viwanda vingine vya cement vilivyokuwa vinawalipa vizuri ila baada ya kusikia tishio la ujio wa likiwanda kubwa ambalo lingepewa gas, exemption ya kodi n.k likapunguza bei ya cement viwanda hivyo vingekufa kwa kushindwa kujiendesha,
Hatua mojawapo zilizochukuliwa na viwanda bora kama vile Twiga na vingine ni kupunguza wafanyakazi kwa kiasi kikubwa ambao wengi walienda Dangote kulipwa ujira mdogo sana maana yeye Dangote anatumia management ya Wahindi.
Kule Nigeria alianza biashara zake kwa style ya kuwahonga viongozi wakuu na wakampa excemption ya kodi, matumizi ya barabara hovyo na vitu vingine akashusha bei ya Cement, viwanda vingine vikafa akabaki yeye mwenyewe akishikilia kama 90% ya soko la cement na Lafarge kama chini ya 10% vingine vilikufa baada ya kuhakikisha kwamba ameviua akapandisha bei ikarudi kama zamani.
Hivyo ndivyo alitaka kufanya Tanzania, JK alimpa maeneo makubwa sana, mpaka na eneo la kujenga bandari yake binafsi, jambo ambalo kwa maoni yangu naona ilikuwa hatari hata kwa usalama wa nchi.
Eneo lililojengwa kiwanda na mining lilikuwa la vijiji vitano, ni eneo kubwa ambalo lilikuwa mali ya wananchi, Dangote kwa kushirikiana na viongozi wa serikali ya awamu ya nne waliwatapeli wale wazee kwa kuwapa vitu vidogo vidogo na ziara ya kwenda kuhiji kwa wazee wachache pamoja na laki tano tano na ahadi kibao wakabariki kuiacha ile ardhi na wale wazee wakatumika kuwashawishi wengine wakaingia kingi.
Mara kadhaa nilikuwa nikiwaona hawa wazee wanaojiita wenyeviti wa vijiji vile wakiambaa ambaa pale nje ya kiwanda cha Dangote wakitapeli watu kwa ahadi ya kuwaunganishia vibarua kiwandani wakati hata wao hawana ruhusa ya kuingia ndani ya kiwanda, wazee wamepigika wanajuta tu kimoyo moyo.
Niliwahi kujaribu kuongea na mmoja wao ambaye alikuwa mwenyekiti wa wenyeviti wakati huo nikiwa kiongozi wa chama cha wafanyakazi hapo Kiwandani, nilipomuuliza sababu ya wao wazee kugawa ardhi bure kwa Dangote aliniambia kwamba wao waliamini Dangote si mfanyabiashara ni Alhaji kwa hiyo walitoa ardhi kwa Alhaji ili ajenge kiwanda kiwasaidie watu..
Nilishangaa sana, lakini kilichonifurahisha ni kwamba wanajuta maana zaidi ya laki tano na ziara ya Mecca hawajafaidika tena kwa namna walivyotarajia.
Mtindo wa ufanyaji kazi wa Dangote ni wa kitapeli tapeli tu, anatapeliwa kuanzia mfanyakazi wake wa chini mpaka Rais na mawaziri wakiingia kingi wanatapeliwa.
Kule Nigeria, ana kiwanda kikubwa Four kiln lines kwenye state ya Obajana na kingine Ibese, wafanyakazi zaidi ya 60% ni wahindi, wanaishi vizuri kila kitu wanachotumia ni tofauti na weusi, magari, nyumba za kuishi n.k ni tofauti kabisa.
Wahindi wanaletwa wakiwa hawajui kitu kabisa wanafundishwa na weusi (wanigeria) halafu wakishajua wanawasimamia weusi, wanawanyanyasa sana waafrika, pale ndipo nilipojua kwamba Tanzania ni nchi nzuri sana na siku zote nawambia ukitaka kujua uzuri wa nchi yetu Tanzania nenda Nigeria. Hususanu kufanye kazi kwa Dangote.
Wakati Dangote anafungua kiwanda Tanzania, alikuwa anaahidi kuajiri watanzania lakini ukweli ni kwamba alikuwa ameandaa makontena ya wahindi kuja Tanzania kama ilivyo Nigeria, thanks to God Magufuli akaingia Madarakani.
Wale wahindi wachache waliokuwepo walichukia sana wakaanza hata kukuza mambo au kutunga uongo wakiilaumu Serikali ati kwa kuweka vikwazo vingi, wakati mwingine wanamdanganya Dangote kuhusu Serikali yetu na Watanzania ili wao wapate faida. Ninao ushahidi wa mambo baadhi ambayo kwa makusudi kabisa management ya kihindi ilikuwa ikimdanganya Dangote kwa faida yao.
Mojawapo ilikuwa ni ubora wa makaa ya Mawe ya Tanzania, tulikuwa na vijana wetu maabara pale, hata mimi niliposikia kwamba makaa yetu ya mawe yana quality ya chini niliumia sana niliwauliza wahandisi wetu waliokuwa maabara wakasema ni uongo.
Hiyo ilikuwa mbinu ya wahindi kufanya biashara na makampuni ya South Afrika kwa faida yao huku wakichafua bidhaa zetu.
Lingekuwa jambo la ajabu sana kama serikali ingekubali uhuni huo, nawapongeza sana Mawaziri hawa wa awamu ya tano kwa kutumia elimu yao vizuri kuchunguza hilo kwa sababu hata enzi zile tulikuwa tuwaeleza serikali kila tunapopata nafasi lakini enzi ya awamu ya nne ilikuwa enzi ya aina yake. tulionekana wapuuzi au maskini wanoko.
Watanzania tunapopinga au kutetea ni vema tukatafuta ukweli kwanza, Dangote industries ukiisikia kwenye vyombo vya habari utaona ni mkombozi kwa watanzania, lakini kwa namna ilivyo na inavyotaka ifanyiwe ni hatari sana kwa taifa.
Tumshukuru sana Rais na serikali kwa msimamo wake. Dangote hana tofauti na akina Carl peters wa zamani labda abadilike.........
Itaendelea wiki ijayo