Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 2,564
- 7,324
Leo wanajamiiforum tuzungumzie kuvunjika kwa Uume "Mbolo" ambayo kitaalamu uitwa Penile fracture hii hali uwa ni yenye kuhitaji Matibabu ya dharula au haraka yani ni medical emergency 🚨— ingawa ya jina hilo, lakini hakuna Mfupa ndani ya uume. Hii hali inaweza kukutokea ukiwa unaichapa au huko faragha na ukichukulia poa na usijue nini cha kufanya, kumbe inaweza kukuletea madhara hapo badae.
Kuvunjika kwa Uume utokea pale tunica albuginea (nyama ngumu inayozunguka sehemu za ndani ya Uume) inapochanika wakati Uume umesimama au kudinda. Nyama hii uchanika na kupelekea uume kukosa uwezo wa kusimama kidete kuhimili mapambano ukiwa faragha.
Watu wengi ambao wamekumbana na hali hii usema:
Kama haitatibiwa haraka, inaweza kusababisha:
✅ Upasuaji wa haraka wa kurekebisha uume ndio jawabu la moja kwa moja
👉 Wai hospitalini mapema kwenye huduma ya dharula
👉 usijaribu kusubiria
👉 usijaribu kuifanyia masaji au kuinyoosha
Je ni hali gani?
Kuvunjika kwa Uume utokea pale tunica albuginea (nyama ngumu inayozunguka sehemu za ndani ya Uume) inapochanika wakati Uume umesimama au kudinda. Nyama hii uchanika na kupelekea uume kukosa uwezo wa kusimama kidete kuhimili mapambano ukiwa faragha.
Visababishi
- Kufanya Mapenzi kwa vurugu, kasi au kwa nguvu (Hiki ndio kisababishi kikuu). Wewe unaichapa kwa kukomoa au kwa sifa unaona ndio ujanja mwisho wa siku uume unavunjika
- Kukunjika kwa ghafla kwa uume uliosimama. Hii inaweza kutokea wakati wa kujamiiana kwa bahati mbaya mwanamke akakalia uume kupelekea kuvunjika, au mwanaume mwenyewe anaweza kuisukuma vibaya na kupelekea kukunjika na kuvunjika.
- Kujichua kwa nguvu au kwa purukushani. Wale wazee wa puchu au kujichukulia sheria mkononi unaweza kufanya masterbation kwa nguvu sana au kasi kwa kubinya kwa nguvu ukavunja uume bila kujua
- Kuulalia uume uliosimama wakati umesinzia au umelaliwa. Hii utokea labda umelala na ukapata hali ya uume kusimama alafu gafla ukajigeuza na kulalia uume na kupelekea kuuvunja
Dalili kuu
Watu wengi ambao wamekumbana na hali hii usema:
- Kusikia mlio wa kitu kupasuka au kuchanika
- Maumivu ya ghafla baada ya kuuvunja
- Kushindwa kusimamisha uume ndani ya muda mfupi
- Kuvimba na michubuko (Uume unaweza kuwa na rangi ya zambarau — “ulemavu wenye kufanana na biringanya” 🍆)
- Uume uonekana uliopinda au kukunjika
- Damu kwenye tundu la uume au Kushindwa kukojoa (inadhihirisha mrija wa mkojo umepata shida — hatari zaidi)
Kwa nini ni hatari
Kama haitatibiwa haraka, inaweza kusababisha:
- Tatizo la kudumu la Kushindwa kusimamisha uume au kudinda
- Maumivu makali wakati wa kusimamisha uume
- Uume uliopinda (Kama ulemavu)
- Matatizo ya kupitisha mkojo
Tiba (Muhimu Zaidi)
✅ Upasuaji wa haraka wa kurekebisha uume ndio jawabu la moja kwa moja
- Matokeo uwa mazuri kama utawai tiba ndani ya masaa 24
Nini cha kufanya
👉 Wai hospitalini mapema kwenye huduma ya dharula
👉 usijaribu kusubiria
👉 usijaribu kuifanyia masaji au kuinyoosha