wakikosi
JF-Expert Member
- Feb 28, 2015
- 1,354
- 1,493
Ukioa wanawake ma feminist ninyi ni sawa na kuwa na wanaume wawili ndani ya nyumba.Huwa amumbiwi wala kusikia ninyi.Jeuri iko wapi, mambo yamebadilika nakupa ukweli uliopo tu.
Kinachowasumbua wanaume wengi ni kwamba unataka mwanamke awe kama mwanao unamtuma, unamkaripia, unampiga na unamtisha anatetereka... Ni sawa maandiko yanaagiza wanawake wawaheshimu waume zao wengi wanafanya hivyo na Wapo waliovumilia sana wakafika mahali wakachoka maana akili za wanaume wengi hasa wa kiafrika ni kwamba wao wajuaji wa kila kitu wanasahau na wanawake wana akili tena sana tu. Na mwanamke huwa anareact kutokana na unavyo-mtreat vinginevyo ni tabia yake tu.
Kuna wanawake bahati mbaya wameolewa na wanaume wapumbavu (kama nabali ktk biblia,stori ya Daudi) hawa wanawatetea waume zao na kuwafichia aibu lkn wanaume huwatesa ili kijitutumua kwamba wako juu. Mwanaume mwenye akili hatishiki na mafanikio ya mkewe, anajua kuna siku atasaidiwa, asilimia kubwa pesa ya mwanamke inatumika katika familia ataona vyombo atanunua n.k wakati baba analewa na kuhonga.
Ni vema muoe wanawake wa hadhi zenu na wanaowapenda, wanawake wenye mafanikio waachieni wanaume wenye akili.
Mkeo ni partner katika maendeleo ya familia sio mtumwa wala dobi, anatafuta hela ndo maana yuko bize. Tafuta msaidizi wa ndani au saidia kuziba gepu unaloona katika familia ikiwemo kusaidia kufua.
Hizi ni zama mpya, isaidie familia kwa kuipa mama mwenye kipato kizuri.
Uanaume wako uonekane katika matunzo na malezi bora ya familia.
. Dawa msiwasomeshe mabinti zenu na mkaoe kijiji wale std seven. Kukaa mnawakandia wanawake wanaofanya kazi na waliopitia shida na majaribu wakafanikiwa katika maisha ni ishara ya udhaifu.