Facts 13 kuhusu Lowassa na Uchaguzi 2015

Facts 13 kuhusu Lowassa na Uchaguzi 2015

Haya yote ungekiambia chama chake ungekua umemsaidia sana.
 
km 5 zipi wakati mtu amekimbia km 1.akalazwa German?

achana na fitna mzee yuko dubai kwenye sherehe za muungano na watanzania wanaoishi kule na picha katuma ningekua na namba yako ya watsap ningekutumia yuko fiti
 
achana na fitna mzee yuko dubai kwenye sherehe za muungano na watanzania wanaoishi kule na picha katuma ningekua na namba yako ya watsap ningekutumia yuko fiti
Kwanini hajahudhuria sherehe za muungano na yeye anategemea kuchaguliwa kuwa kiongozi wa taifa hili?Ina maana amedharau?
 
Hata kama chama chake kikimpitisha siwezi kumchagua mtu ambae amekaa bungeni miaka 8 kama bubu hata kuchangia wala kutoa hoja moja kuwasemea wananchi wake leo eti anapewa sifa za wajinga kwa sababu tu watu wanalipwa,kweli watanzania tunanunulika kwa bei ya ubuyu.ukimlipa mjinga senti ya mboga kidogo hata ukimnyea kichwani atakusifia.
 
Kwanini hajahudhuria sherehe za muungano na yeye anategemea kuchaguliwa kuwa kiongozi wa taifa hili?Ina maana amedharau?

alihuzulia za dubai mkuu nako kuna watanzania mkuu usiwe na wasiwasi tunashinda
 
Hata kama chama chake kikimpitisha siwezi kumchagua mtu ambae amekaa bungeni miaka 8 kama bubu hata kuchangia wala kutoa hoja moja kuwasemea wananchi wake leo eti anapewa sifa za wajinga kwa sababu tu watu wanalipwa,kweli watanzania tunanunulika kwa bei ya ubuyu.ukimlipa mjinga senti ya mboga kidogo hata ukimnyea kichwani atakusifia.

ukiwa mbuge kazi sio kubwabwaja watu wanataka vitendo hao wanaobwabwaja wamefanya nini
 
14.Lowassa ndio fisadi pekee kutoka ccm ambae amepata heshima ya kutajwa na baba wa taifa kwamba asipewe uongozi wa nchi hii milele na milele.




Stop lying....Mwalimu Nyerere HAKUNA HATA SIKU MOJA ALISEMA LOWASSA ASIPEWE UONGOZI...Hizi ndizo habari za vijiweni....UNAWEZA PROVE ..?? Ulikuwepo ww..!!? Hizi ndio tabia za uongo za team Membe...!!! Hv mmezaliwa ktk uongo nn..!!?

Mkatae mkubali, Lowassa ni habari ya mujini, vijijini, vyuoni, Misikitini, Makanisani, Abroad, hadi UKAWA..ni Lowassa tu....!!! Hatuchaguai chama au nn...TUNACHAGUA MTU...NA MTU KWA SASA NI LOWASSA....No objection...hutaki utake, tht is the fact...!!!

Lowassa 🏃🏃🏃🏃🏃 ==>> 2015
 
Mleta mada,

Katika hitimisho lako ulipaswa useme "Lowassa kwa sasa nakuhitaji....."

Hii ni kukukumbusha tu kuwa usichukulie mambo sensitive kama ya rais wa nchi kwa ujumla ujumla.

Am out here.
 
ukiwa mbuge kazi sio kubwabwaja watu wanataka vitendo hao wanaobwabwaja wamefanya nini

Yanapokuja mambo ya maslahi kwa taifa mbunge ni lazima aseme. Kwa mfano mambo kama bajeti, katiba, miswaada mbalimbali nk

Ila kuhusu kuhudumia jimbo lake hayo sisi wengine hayatuhusu. Hata akiwa kiziwi, bubu sisi hatutaki kuyajua.

Ila sijawahi kusikia Lowassa akitoa msimamo wake kulingana na maoni yaliyotolewa na wananchi. Yeye kimya. Sasa kama alitaka kuwafurahisha CCM, basi aongee nao hao CCM wenzake huko.
 
Kwanini hajahudhuria sherehe za muungano na yeye anategemea kuchaguliwa kuwa kiongozi wa taifa hili?Ina maana amedharau?



Lowassa aliwakilisha Taifa Dubai...kwa mualiko maalum na watanzania wanaoishi huko siku ya muungano wa miaka 51....una swali lingine...
 
Lowasa ndiye mgombea pekee ambaye afya yake si nzuri
 
Mwl hawahi kumkataa Lowassa tuache kutunga uongo,Michael Mimi kwaka 1997 tuliwahi kwenda na Mwl Burundi na wakati wote alipenda kuniita katika sehemu ya ndege ile iliyokuwa ikitwa ya CCM tunakaa nae niliwahi kumuliza mawaziri wa Mkapa ambao a nadhani ni wachapa kazi alimtaja Lowassa hapo nakumbuka tulikuwa na walinzi wake Mlazabi na Tendewa...pia mwanzoni mwa mwaka 1999 tukiwa na Mzee Butiku,Mh Mkono wakati huo hakuwa mbunge nakumbuka alikuwa amekuja balozi mmoja pale Butiama waliambatana na MH Kikwete cha kwanza alisalimia Kikwete alisema naridhishwa na itendaji wa Edward kisha alitania tumsaidie kusomba tofari za ujenzi w shule ya sekondari y Chief Wanzagi wakati hakujua kama ingejengw na Mh Mkono na kuitwa kina hilo hapo ndipo alipomtania pia Mkono kuwa uchaguzi wa mwaka 2000 ajitokeze kugombea ubunge ili aweze kumaliza ukabila na jusaidia uboreshaji wa sekta ya elimu sasa uzushi unasemwa eti Mwl alimkataa Lowassa ujinga wa kupindukia,nimewataja watu hapo na wapi hai muwatafute wawape ukweli...tuaMarato asa za maji taka kwa kutumka vibaya jina la Mwl Nyerere.G.Marato
 
Hizo nguvu zote zinazotumika kwa ajili ya Lowasa zinanitia shaka sana. Hivi Lowasa asipopitishwa na CCM hamtakufa kwa kihoro ninyi?

Ni kama vile hatima yenu yote iko mikononi mwa Lowasa.

Vv
 
1. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee mwenye wapenzi na mashabiki wengi kwa sasa....

2. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee mwenye wasifu na historia kubwa na iliyotukuka katika utendaji wake ndani ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali kwa ujumla..

3. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee ambaye mpaka sasa kashawishiwa na makundi mengi sana ya kijamii, eg. Wakulima, wafanyabiashara, bodaboda, wafugaji, Mamalishe, wachimbaji wadogo wa madini, wanafunzi, wachungaji n.k

4. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee mwenye ushawishi na nguvu ndani ya Chama Cha Mapinduzi na jamii kwa ujumla (rejea tafiti na takwimu mbalimbali)

5. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee aliyeonyesha uzalendo wake kwa kupigania Nchi yake katika vita vya Kagera 1978/1979. Kwa Nchi nyingi duniani kupigana vita ni sifa muhimu na ziada kwa mtu anayewania uongozi. Kushiriki kupigana vita huchukuliwa kuwa ni kiwango cha juu kabisa cha uzalendo...

6. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee mwenye maono yaliyowazi katika kuwakomboa wananchi kwa kuonyesha vipaumbele vya Taifa eg. Elimu, Elimu, Elimu, Afya, Kilimo, Kuondoa umasikini, kukuza uchumi n.k

7. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee aliye maarufu na ambaye wananchi wana matumaini naye kwa sasa. Hii inatokana na utendaji kazi wake na uwezo wake mkubwa wa kusimamia jambo eg. Shule za kata, mradi wa maji ziwa Victoria, Chuo cha UDOM, maamuzi ya City Water, viwanja vya Mnazi Mmoja na plot No. 125~157 Mikocheni n.k

8. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee mwenye maamuzi magumu na sahihi kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla...

9. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee atakayeweza kusimamia, kurudisha na kuleta nidhamu kwa viongozi na watendaji wa serikali na mashirika ya Umma...

10. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee mwenye nguvu wa ushawishi wa hoja kwa wananchi na katika vikao mbalimbali vya maamuzi (rejea kikao cha maamuzi kuhusu matumizi ya maji Ziwa Victoria nchini Misri, rejea kikao cha kupitisha maamuzi ya ujenzi wa UDOM n.k)....

11. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee aliyejiandaa kisaikolojia kuingia Ikulu (rejea uchambuzi wa Prof. Kitila Mkumbo)....

12. Lowassa ndiye mgombea mtarajiwa pekee mwenye sifa za ziada kama...
i. Mchapakazi kwa bidii
ii. Msikivu
iii. Mbunifu
iv. Muadilifu
v. Mpenda watu/wananchi
vi. Mvumilivu & Mstahimivu

13. Lowassa, ndiye mgombea mtarajiwa pekee mwenye dhamira na nia ya dhati kuondoa umasikini uliokithiri (Absolute Poverty)....

Mytake: kwa hizi facts zote, ni wazi Lowassa kwa sasa tunakuitaji kuliko kipindi chochote kile katika historia ya Nchi hii...

14. Lowasa ndio mgombea pekee mwenye uhakika wa kupitishwa kugombea uraisi maana asipopita ccm atachaguliwa act-zito
 
Back
Top Bottom