MVUMBUZI
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 5,182
- 2,304
Kwa muda mrefu serikali yetu imekuwa ikisisitiza kuwa ajira ambazo watanzania wana uwezo wa kuzifanya wageni kutoka nje hawaruhusiwi kuzifanya. Msisitizo huu unatokana na malalamiko ya waTanzania katika sekta nyingi kujikuta ajira zao zikichukuliwa na wageni kutoka nje ya nchi yetu tena bila kuwa na kibali cha kufanya kazi.
Zamu hii ni kilio cha Tour Guides wa Kitanzania ambao walikuwa wanajipatia riziki yao kubwa kutokana na tip walizokuwa wanapewa na watalii wanao wapeleka kuona vivutio vyetu mbalimbali vya kitalii hasusani mbuga za wanyama.
Namwomba nimweleze Ezekiel Maige kuwa makampuni mengi ya kitalii kutoka nje yamewaajiri Tour Guides kutoka nje(wazungu wenzao) huku wale wa kitanzania wakibakia kuwa madereva tu.
Tour guide hawa wamekuwa wakijichanganya na watalii na kwa sababu wote ni wazungu inakuwa vigumu kugundua kama mmojawapo siyo mtalii bali ni tour guide wa kizungu. Madereva wanawajua na wameanza kulalamika kwa sababu hawa tour guide wa kizungu ambao hawajui lolote kuhusu mbuga zetu wamekuwa wakichukua ile tip ambayo ni stahili ya madereva ambao wengi wamesoma tour guide.
Kampuni ya kitalii ya KER & DOWNEY SAFARIES inayomilikiwa na Tom Fredkin ambaye ni raia wa Afrika ya Kusini aishiye Marekani na yenye ofisi yake Ngaramtoni mjini Arusha inaongoza kwa kuwa na Tour guide wote wazungu lakini hujichanganya na watalii ili wasijulikane. Madereva wake wamekuwa wakilalamikia hali hiyo ambayo wamesema inawafanya kuwa hohehahe kutokana na tips zao kuchukuliwa na tour guide fake wa kizungu. Kinachosikitisha zaidi ni kwamba hawa wazungu uchwara hawana vibali vya kufanya kazi nchini na hawana ujuzi wowote wa Tour guide na mara nyingi hutumia mgongo wa madereva wa Ki tanzania kufanya hiyo kazi.
Mbaya zaidi kuna wazungu ambao wameanzisha makampuni ya kubeba watalii ambao huishi tu porini na huwa hupokea wageni wanaotumia usafiri wa ndege zinazotuwa ndani ya viwanja vya ndege vilivyoko katika mbuga zetu mbalimbali.
Mh. Ezekieli Maige naomba utueleze kama unajua hili na kama unajua basi tujibu sisi watanzania ambao mbuga ni zetu kuwa hawa wazungu wanafanya nini kwenye mbuga zetu?
Inakuwa mgeni kumwelekeza mgeni katika mbuga zetu huku serikali imelala usingizi tu huku wenye rasilimali wakibakia wasindikizaji tu?
Mpaka lini waTZ tutabaki tukitazama bila msaada rasilimali zetu ziporwa na wwageni mchana kweupe bila kufaidi hata ile staili ndogo kama tip?
Maige naomba usikie kilio cha watanzania wenzako inawezekana Mungu alikupa hiyo nafasi utusaidie kama Yusufu alivyowekwa Misri kuwasaidia ndugu zake.
Kama uko tayari details zote utazipata na ili kurudisha heshima ya nchi maana hawa wazungu wanatuonea na kutuona mama huruma.
Zamu hii ni kilio cha Tour Guides wa Kitanzania ambao walikuwa wanajipatia riziki yao kubwa kutokana na tip walizokuwa wanapewa na watalii wanao wapeleka kuona vivutio vyetu mbalimbali vya kitalii hasusani mbuga za wanyama.
Namwomba nimweleze Ezekiel Maige kuwa makampuni mengi ya kitalii kutoka nje yamewaajiri Tour Guides kutoka nje(wazungu wenzao) huku wale wa kitanzania wakibakia kuwa madereva tu.
Tour guide hawa wamekuwa wakijichanganya na watalii na kwa sababu wote ni wazungu inakuwa vigumu kugundua kama mmojawapo siyo mtalii bali ni tour guide wa kizungu. Madereva wanawajua na wameanza kulalamika kwa sababu hawa tour guide wa kizungu ambao hawajui lolote kuhusu mbuga zetu wamekuwa wakichukua ile tip ambayo ni stahili ya madereva ambao wengi wamesoma tour guide.
Kampuni ya kitalii ya KER & DOWNEY SAFARIES inayomilikiwa na Tom Fredkin ambaye ni raia wa Afrika ya Kusini aishiye Marekani na yenye ofisi yake Ngaramtoni mjini Arusha inaongoza kwa kuwa na Tour guide wote wazungu lakini hujichanganya na watalii ili wasijulikane. Madereva wake wamekuwa wakilalamikia hali hiyo ambayo wamesema inawafanya kuwa hohehahe kutokana na tips zao kuchukuliwa na tour guide fake wa kizungu. Kinachosikitisha zaidi ni kwamba hawa wazungu uchwara hawana vibali vya kufanya kazi nchini na hawana ujuzi wowote wa Tour guide na mara nyingi hutumia mgongo wa madereva wa Ki tanzania kufanya hiyo kazi.
Mbaya zaidi kuna wazungu ambao wameanzisha makampuni ya kubeba watalii ambao huishi tu porini na huwa hupokea wageni wanaotumia usafiri wa ndege zinazotuwa ndani ya viwanja vya ndege vilivyoko katika mbuga zetu mbalimbali.
Mh. Ezekieli Maige naomba utueleze kama unajua hili na kama unajua basi tujibu sisi watanzania ambao mbuga ni zetu kuwa hawa wazungu wanafanya nini kwenye mbuga zetu?
Inakuwa mgeni kumwelekeza mgeni katika mbuga zetu huku serikali imelala usingizi tu huku wenye rasilimali wakibakia wasindikizaji tu?
Mpaka lini waTZ tutabaki tukitazama bila msaada rasilimali zetu ziporwa na wwageni mchana kweupe bila kufaidi hata ile staili ndogo kama tip?
Maige naomba usikie kilio cha watanzania wenzako inawezekana Mungu alikupa hiyo nafasi utusaidie kama Yusufu alivyowekwa Misri kuwasaidia ndugu zake.
Kama uko tayari details zote utazipata na ili kurudisha heshima ya nchi maana hawa wazungu wanatuonea na kutuona mama huruma.