EXTRAVAGANZA Safari's za treni ya SGR reli ya kati

EXTRAVAGANZA Safari's za treni ya SGR reli ya kati

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
23,251
Reaction score
28,406
Ukiingia kituo cha treni ya SGR Dar es Salaam ili upate tikiti ya shs. 13,000/= utahudumiwa na wafanyakazi kama wanne ukianza na kaunta ya mapokezi ambaye hana kazi.

Ukienda dirisha la tikiti yupo unayemuambia unakokwenda na muda wa treni unayotaka, kisha anaelekeza kwa mwandika tikiti naye anakurusha kwa mpokea malipo ya tikiti na kukurusha kwa mtoa tikiti!

Mlolongo huu umepunguza ukosefu wa ajira ila umepunguza faida kwenye tikiti hiyo ya sh.13,000/= kwenye hatua ya kwanza ukiacha ngazi za umeme zinazokupeleka kwenye malipo na kukushusha.

Hatua ifuatayo ni sehemu ya ukaguzi wa kabegi kako, hapo ipo skana na wakaguzi zaidi ya watatu wanapiga soga, safi sana maana bila soga watasinzia, nao mshahara unatoka kwenye ile tikiti ya sh.13,000/=, hapa angalau waweke malipo ya gharama za ukaguzi kufidia hasara.

Hatua ya mwisho ni baba lao, kusafirishwa kwa treni ya umeme kwa kutumia tikiti hiyohiyo ya sh 13,000/=!Humo ndani ya treni sasa kunawafanyakazi wengi kuliko hoteli ya kitalii ambao utawaona wakipanda treni lakini mpaka unafika Morogoro hautawaona wanachokifanya ndani ya treni, nao mshahara unatoka ndani ya hiyohiyo sh.13,000/= na treni ya SGR bado inapata faida! Kweli Mungu Mkuu.

Asante TRC mmenifikisha salama japo kachupa kangu ka maji ya kunywa na mfuko wangu wa shangazikaja mmeninyanganya(mmeninyang'anya).
 
nashauri tu maintanance. vile vidude vya kutundika kakitu pale kwenye seat baafh vimeng'olewa.
 
Umeongea point tupu tangu mwanzo mpaka mwisho halafu lile bibi shetani la baharini linasema tunafanya vizuri kuliko marekani na ulaya. Sijui wanaokota wapi hizi takataka watanganyika wenzangu. Yani majitu na bakora zao mbele kama tai yanafyata kwa kinyago yalichokichonga yenyewe eti. Mabeyo huna akili kabisa
 
Kuna abiria 1000 humo na wewe ndio umelipa bei ya chini kabisa.
Kwenda na kurudi×30.
We unadhani wao hawana akili
 
Kuna abiria 1000 humo na wewe ndio umelipa bei ya chini kabisa.
Kwenda na kurudi×30.
We unadhani wao hawana akili
Ungekuwa umewahi kufanya biashara ungejua kuwa ukipunguza gharama za matumizi yasiyo ya lazima unaweza kuikuza biashara yako, kwa wanaojua kifo cha mabasi ya Kamata wanakumbuka jinsi yale mabasi yalivyokuwa yakitenga kiti cha nyuma mwisho kwa ajili ya fundi endapo likiharibika! Kiti namba moja na mbili cha kondakta na dereva! Mabasi ya shirika la reli yslikuwa na madereva wawili tu ambao walikuwa mbele kwenye chumba chao, haya yalifanya vizuri mpaka EAC ilipovunjika.
Hebu tuseme ukweli hilo kundi la wahudumu wanawake na wanaume wanafanya kazi gani wakati hawaonekani na hakuna mtu anahitaji huduma zao.
 
Umeongea point tupu tangu halafu lile bibi shetani la baharini linasema tunafanya vizuri kuliko marekani na ulaya. Sijui wanaokota wapi hizi takataka watanganyika wenzangu. Yani majitu na bakora zao mbele kama tai yanafyata kwa kinyago yalichokichonga yenyewe eti. Mabeyo huna akili kabisa
😁😁😁😁😁
 
Tatizo ni kunyang'anywa 'shangazi kaja'

Hao wote ulowaona ni 1/3 ... bado wengineo walioko kwenye mifumo ya ict / umeme / ulinzi usioonekana / wamasai etc
Usafiri umeleta mabadiliko sana kiuchumi, malazi, etc
 
Yaani ukisoma tu comment unajua kabisa tanzania kuna sehemu tumemkosea muumba wetu,
Na wengine hawajawahi hata kuitumia hiyo SGR. Mleta mada alichokisema huo ndio uhalisia wenyewe ni kero na matumizi mabaya ya rasilimali watu na pesa. Kwa wenzetu ni mashine moja tu unalipa tickett inatoka , PERIOD
 
Tatizo ni kunyang'anywa 'shangazi kaja'

Hao wote ulowaona ni 1/3 ... bado wengineo walioko kwenye mifumo ya ict / umeme / ulinzi usioonekana / wamasai etc
Usafiri umeleta mabadiliko sana kiuchumi, malazi, etc
Acha uchawa, reli imeishia Dodoma, safari nne kwenda nne kurudi wewe unasema imeleta mabadiliko makubwa kiuchumi wakati haibebi mizigo! Uchumi upi! Uchawa usio na tija.
 
Tatizo ni kunyang'anywa 'shangazi kaja'

Hao wote ulowaona ni 1/3 ... bado wengineo walioko kwenye mifumo ya ict / umeme / ulinzi usioonekana / wamasai etc
Usafiri umeleta mabadiliko sana kiuchumi, malazi, etc
Ila SGR inawanyima riziki Watanzania wengi na inatufundisha "uchoyo na ubinafsi".

Mimi nikisafiri kati ya Dar na Dodoma kwa njia ya barabara,lazima ninunue vitu pale Chalinze (nyama), Mbande, Kibaigwa, Gairo, Dumila, Ruvu, Chalinze kwa ajili ya zawadi.
Wale wauzaji wanapata japo kidogo, lakini pia kule niendapo wanajua kweli Babu kaja kutokana na zawadi nibebazo.

Kwa SGR hayafanyiki haya, hata dhabibu kubeba ni shida.
Nafikiri ingekuwa vyema kama kungekuwa na behewa/mabehewa ya kuweka mizigo kwa kila safari, ili watu tusafiri na zawadi zetu na " shangazi kaja" zetu.
 
Ila SGR inawanyima riziki Watanzania wengi na inatufundisha "uchoyo na ubinafsi".

Mimi nikisafiri kati ya Dar na Dodoma kwa njia ya barabara,lazima ninunue vitu pale Chalinze (nyama), Mbande, Kibaigwa, Gairo, Dumila, Ruvu, Chalinze kwa ajili ya zawadi.
Wale wauzaji wanapata japo kidogo, lakini pia kule niendapo wanajua kweli Babu kaja kutokana na zawadi nibebazo.

Kwa SGR hayafanyiki haya, hata dhabibu kubeba ni shida.
Nafikiri ingekuwa vyema kama kungekuwa na behewa/mabehewa ya kuweka mizigo kwa kila safari, ili watu tusafiri na zawadi zetu na " shangazi kaja" zetu.
Humo mwenye shangazikaja ndimo mnabeba ndumba ili treni isimame porini.
 
Nikipanda treni huwa nawaza sana ilivyo kwa sasa halafu baada ya miaka mitano masikini ije iwe kama mwendokasi kweli.........!
 
Back
Top Bottom