Nawashukuru Jamiiforum.com kwa kutoa furusa hii ya kuuliza maswali. Nina imani mlengwa atayatendea haki maswali yetu kwa kuyajibu kwa ufasaha na kwa staha.
Maswali yangu ni haya kwa kuanzia.
1. Miaka kadhaa iliyopitia, Mtanzania mwenzetu ndugu Lissu, ukiwa bado mbunge ulinukuliwa ukiitakia mabaya Tanzania na watanzania wote hasa wale wenye uwezo mdogo kiuchumi. Ndugu Lissu ulinukuliwa ukisema kuwaunaitaka dunia/ ulimwengu iifungie/ iwekee vikwazo vya kiuchumi, kidiplomasia, kisiasa, kijamii na mengine kama hayo, yaani dunia itemee mate Tanzania. Kwa uhalisia vikwazo hivi vilipotumika kwenye nchi nyingine mfano Zimbabwe, Iran, hata Venezuela uathiri wananchi wenye vipato vya chini na kati, ambao kwa hapa Tanzania ndio walio walio wengi.
Je, Katika mazingira kama haya Watanzania hawa, sisi, tulio wengi tutapa sababu gani za kukuamini kuwa unaweza kuwa kiongozi wa nchi yetu na kujali maslahi ya nchi hii na watu wake wakati kwa vikwazo ulivyotuombea sisi vitupate vina lenga kukuimarisha wewe binafsi mbele ya wale ambao hawatutakii mema sisi watanzania na nchi yetu kwa ujumla wake!?
2. Siku kadhaa zilizopita ukiwa Mkoani Kilimanjaro, ulinukuliwa kupitia vyombo vya habari ikiwemo televisheni ya ITV ukisema kuwa utarudisha madaraka kwa wananchi kama ilivyokuwa wakati wa Ukoloni. Tulio wengi tunajua wakati wa ukoloni watanzani/wananchi walifanywa manamba na wengine kuuzwa nje kama watumwa.
Je, Kwa kauli hii sisi watanzania tutaachaje kuamini kuwa kipindi tu Ndugu Yetu Lissu utakapopata madaraka ya nchi hii utatuuza watanzania kwa mafungu kama bidhaa sawa na kipindi cha Ukoloni na hivyo ni halali tukunyime kura!?
3. Vyombo kadhaa vya kimataifa na baadhi vya humu nchini vimeandika habari kuwa unasimamiwa na mwansheria wa kimataifa ambaye si mtanzania. Pia wakati wamchakato wako wakupat nafasi ya kugombea inasemwa ulishawishi wajumbe wa mkutano kuvuruga wimbo wa Taifa kwa kuongeza maneno ambayo hayapo. Je, Kwa mambo yote mawili yaliyotajwa sisi watanzania tunakosaje haki ya kukunyima kura kwa kuonyesha unatudharau watanzania na pia unadharau mambo yanayotambulisha utanzania wetu!?
Karibu kwa majibu.