Eti ukihamia mbezi lazima uibiwe?

Eti ukihamia mbezi lazima uibiwe?

Simba Mkali

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2012
Posts
620
Reaction score
243
Wadau nimemwambia jamaa yangu kwamba nimeanza kujenga mbezi na niko katika hatua nzuri tu hata kama nikitaka kuhamia mwisho mwa mwaka huu. Alichonijibu ndicho kilichoni acha hoi eti nikihamia Mbezi lazima nivamiwe na majambazi mara tatu. jamani kuna mwenye ukweli wa jambo hili?
 
ukweli gani sasa, haya ukweli ni: utavamiwa, uliza swali lingine
 
Mbezi ipi unayoizungumzia hapa?

kuna mbezi(kwa kina mdee) na mbesi (moro road). Sasa jamaa sijui atahamia wapi maana kila eneo lina aina tofauti ya wezi. Mbezi watu wanakuja na gari na bastola kupakia vitu vyao na mbesi vibaka wanakuja na mapanga kukuibia.
 
nimeamia mbezi mwaka wa tatu sasa na wala sijavamiwa na wengi waliovamiwa baadaye inagundulika kuwa walidhulumiana na wengine walitembea na wake za watu.
 
..Mcheki vizuri huyo jamaa yako. Kuvamiwa ni kama eneo lingine llote tu la Dar. Unaweza ukahamia na siku hiyo hiyo ukavamiwa na unaweza ukahamia na ukakaa miaka kumi bila hata kuibiwa soksi kwenye kamba! Muangalie vizuri huyo Rafiki. Labda anaona wivu kwamba umekamilisha Mjengo wako ama ndio anataka kuchora deal uvamiwe! Mbona wakati unajenga hakukuambia hivyo??
 
kuna mbezi(kwa kina mdee) na mbesi (moro road). Sasa jamaa sijui atahamia wapi maana kila eneo lina aina tofauti ya wezi. Mbezi watu wanakuja na gari na bastola kupakia vitu vyao na mbesi vibaka wanakuja na mapanga kukuibia.
huku kwa akina mbesi (analogy) ndiko ninakotaka kuhamia mkuu unaweza kunipa sifa zake?
 
nimeamia mbezi mwaka wa tatu sasa na wala sijavamiwa na wengi waliovamiwa baadaye inagundulika kuwa walidhulumiana na wengine walitembea na wake za watu.

Sio mbezi tu,mara nyingi watu wanahamia katika nyumba mpya kwa pressure na hyvo kuhamia bila kukamilisha vitu ambavyo ni muhimu kwa ulinzi wa nyumba km grills nk. Kwa maana hyo unamrahishia kibaka kazi. Na hii ni popote iwe kunduchi,mbezi au popote pale.
 
Mimi nadhani ugeni ndio nafuu ya kibaka maana ni vigumu kuwatambua wao kirahisi au tabia za mtaani kwa ujumla.
 
Back
Top Bottom