Siku zote ananitoa out, tunaenda viwanja vikali vikali nikajua nimepata bae ambaye ni ofisa. Hee!! Kumbe mfuga kuku!!
Mara kadhaa amekuwa akijieleza kuwa hatokuwa na nafasi siku hii na hii kumbe anaenda kwenye mabanda yake ya kuku.
Tangu anitokee ni miezi 2 na kitu imepita, tulishafika hatua ya kukubaliana kuoana. Lkn muda wote huo nilikuwa sijaenda kwake.
Leo ktk kuupokea mwaka mpya ndiyo nimeenda mpk kwake nikakuta shughuli yake ya kumuingizia kipato ni kufuga kuku
Come on!! Nimekasirika sana. Yaani mm niwe na mume ambaye asubuhi namuandalia chai ili akafagie mabanda ya kuku? Nitaificha wapi sura yangu mbele ya mashosti zangu tuliomaliza nao chuo wakija kunitembelea? Never on earth!
Nataka mume namuandaa anaenda airport kuhudhuria kongamano mikoani ama nchi za watu. Siyo anahangaika na kinyesi cha kuku!
Ameniharibia sikukuu yangu huyu! Ananionaje kwanza mm? Nafaa kuwa mke wa mfuga kuku mm?? Huyo mwalimu tu asitie maguu hapa.
Aghiiiiiiii!!! Sitaki.