Eti ameniacha kisa kofi moja tu

Eti ameniacha kisa kofi moja tu

Habari,wandugu natumaini mko poa, mmi Nina mpenzi wangu tumekuwa nae kwenye mahusiano huu ni mwezi wa tatu,sio siri huyu binti nampenda sana, nimejitahidi kumhudumia kadri niwezavyo kwa mda mfupi nilikuwa nae, kwa sababu Nina nia ya kumuoa,sasa juzi nilikuwa na rafiki Yangu tupo maeneo ya Sinza tukapita kwenye bar moja hivi ghafla nikamuona mpenzi wangu nae yupo mle ndani ya bar anakunywa kinywaji wakiwa wamekaa na mwanaume mmi simjui, ndipo nikaamua kumpigia Simu mpenzi wangu nakumuuliza yuko wapi.

Akapokea Simu nakunijibu yupo nyumbani kwao anapika na wakati minamuona yupo na kijeba wanakunywa vinywaji huku wanacheka, sio siri nilipatwa na hasira ndipo nikaamua kumtuma rafiki Yangu akamuite ili niongee, aliponiona alishangaa na aliponisogelea2 sikumsemesha neno lolote nikampiga Kofi moja la nguvu rafiki Yangu akanishika mikono na watu wakajaa kidogo, nikaamua kuondoka na yule binti akawa amekipingia.

Sasa zimepita siku mbili yule binti nimempigia Simu akapokea akaniambia yule alikuwa kaka yake mtoto wa baba yake MDOGO na pia ameniambia mmi na yeye basi amesema hawezi kuishi na mtu kama mmi tena, nimejaribu kumuomba msamaha lakini wapi amekataa katakata, naombeni msaada wa mawazo jamani nifanyeje?

Eti Kofi moja2 lini koseshe mke jamani?

Kosa ulilolifanya ni apo nilipo koleza kwa kijani...
hivi hawa wanawake wanawapa nini adi mnawaamini na kuomba msamaha???
 
Eti "kofi moja tu", hivi mnaonaga ufahari kupiga wanawake eeh!! Huna adabu, bora kakuacha maana leo kofi moja kesho sita keshokutwa panga kabisa, wanaume wa hivi sio kabisa.
 
Yaani kwanza nikishaona mtu mwongo mwongo huwa sina imani nae kabisa. Najua huko mbele atakuja kunidanganya mambo makubwa. Na ukiona hivyo ujue hiyo sio mara ya mwanzo kukudanganya, inawezekana ndio 40 yake hiyo. Just imagine ndani ya miezi 3 keahakudanganya mara 40. Huyo hafai tafuta tu mwingine
 
Mtumie kama laki moja hvi kwenye M-PESA yake then urudishe mrejesho hapa jamvini kama ataendelea na msimamo wake.
 
Yaani kwanza nikishaona mtu mwongo mwongo huwa sina imani nae kabisa. Najua huko mbele atakuja kunidanganya mambo makubwa. Na ukiona hivyo ujue hiyo sio mara ya mwanzo kukudanganya, inawezekana ndio 40 yake hiyo. Just imagine ndani ya miezi 3 keahakudanganya mara 40. Huyo hafai tafuta tu mwingine

Hakika nyani haoni kundule,nyinyi wenyewe waongo wa kutupwa hafu mnashadadia wanawake wanawake,mfyuuuuuu
 
Kofi moja huanzisha lingine na baadaye huwa mazoea. Au wewe ni Mura amang'ana gasalikile?
 
Kofi ni kipimo cha kujua mke mvumilivu kwenye ndoa, kama anakupenda atarudi, usimpigie simu. Mpe mda wa wiki mbili, asipokupigia achana nae, hakupendi.
 
Hujafanya kosa kumpiga kofi kwa sababu ulishindwa kuhimili hasira zako ila siku nyingine jifunze kuhimili hasira.halafu kwanini akudanganye? Kama hataki kukusamehe achana nae tafuta msichana mwingine.kwanza mmedumu kwa miezi bado penzi halijaota mizizi hilo.
 
Mwanamke anayekupenda ukimpiga kwa makosa yake anarudi nyumbani mwenyewe.ukiona hataki kurudi huyo tayari si wako ana mipango yake.
 
Hahahaha!
Na wewe umeamini ni kaka yake mtoto wa baba yake mdogo siyo?
Haya subiria siku uwakute mtu na kaka yake lodge
 
Wewe kofi moja tu ningekua mimi huyo sijui kakaake sijui bwana wake ningempukutisha kila kitu na demu anakula mtama mmoja na nnamwambia tangulia nyumbani nikukute hapo bar unaanzia tifu la hatari..
 
ACHA ujinga mkuu.... hakuna mambo ya ndugu hapo... kwanza kama ni ndugu kwanini akudanganye kuwa yuko nyumbani anapika.. wewe ulichofanya ni sahihi kabisa... maana unamalengo nae marefu hivyo lazima ikuume kuona unamkamata red handed alafu anakudangaya...
Mungu kakuonyesha mapema kuwa huyo sie maana Mungu kaona moyo wako ulivokolea sehemu siyo... we endelea na maisha yako.
 
I naonekana ilikuwa kelbu ya nguvu kisha ukamalizia na maneno haya bloodfully(blalifu).duh hizo mbata zilikuwa maarufu sana miaka ya utoto wetu.

Hahhhahahaha 😂😂😂😂😂😂😂
 
nyaggad

Mm naona ipo sahihi wala usijilaum maana yeye kwann akudanganye kuwa yupo nyumban, kwann asikwambie tu ukweli kama ni kweli alikuwa ni Kaka ake, apeleke ujinga huko! Mm nakusupport Kaka kwa hilo!!
 
Last edited by a moderator:
Hapo hakuna mwanamke wa kuoa fanya yako Brother wanawake wa siku hizi ni pasua kichwa.
 
Ulitaka umpige makofo mangapi ndio akukimbie? Jmn jmn nani alikuambia mwanamke ni wa kupiga? They are delicate, they must be handled carefully, pampered n what mot. Hujamuoa unadiriki kumpiga hadharani!!!!!! Akiingia kwako si atakuwa dekio?? Pole sana. Hata km alikudanganya hilo kofi halifuti kosa lake. Sahau tafuta kwingine na urekebishe tabia zako
 
Back
Top Bottom