Eti ameniacha kisa kofi moja tu

Eti ameniacha kisa kofi moja tu

Mkuu nafikiri utakuwa na matatizo ya fikra...unataka ushahidi gan tena kuwa huyo mwanamke siyo muaminifu???acha upuuzi acha kulialia katika maswala yakipumbavu...huyo hakufai

Short and precise! Jamaa anahisi ila hataki kuikubali reality kuwa huyo mwanamke si wake peke yake.
 
sawa amekudanganya,, hukupaswa kumpiga sio mwanao huyo.....kifupi ushaliwa.....na hamu ya kuchunwa bado unayo.....
 
Kisa kofi moja tu? Kama ni moja tu jilabue mwenyewe....
 
mkuu kofi moja tu, mi naona halitoshi, hapo ungeongea naye then mwache,mwambie mkutane baadaye. Huko akileta majibu yasiyo eleweka nimakofi matatu ya harakaharaka,akijifanya kasusa aondoke muache tu kwani hujamuoa bado.
 
Hata kwao hujajitambulisha yameshaanza makofi!!!
Biashara ya kupigana imepitwa na wakati best.
 
Kama alikuwa na kaka hapakuwa na sababu ya kukwambia uwongo na pia asingeshtuka kukuona na vilevile asingekimbia..nadhani alikufanya ATM. Ndo dada zetu walivyo ck hizi..walio wengi japo wapo waaminifu wachache

Wewe nae una matatizo, kama alikuwa na kaka yake, kwanini akudanganye? Hujiulizi tu? Huyo hajafanya maamuzi, ingia barabarani kutafuta mwingine, acha kumpigia kabisa. Na huo mkwara wa yeye na wewe basi ni kwa sababu anajua yeye ndie mwenye makosa. Mara nyingi alie na kosa huwa anaoverdo mambo akidhani ndicho kinachopaswa kufanyika ili ionekane kweli. Angekuwa mkweli, angetaka kukuumbua palepale kwa kumuita kaka yake athibitishe kuwa ni kweli wana undugu.
Hivi mbona mnakuwa mazuzu kirahisi hivyo? Mtu unataka kumuoa, adanganye yuko home, umkute bar yuko na jamaa, anadai nivkaka yake baada ya kuwa umempiga kibao, kwanini asimuite huyo kaka amtetee?
Ww umefanya kosa kumpiga lakin yeye kafanya kosa zaidi kwan anaonekana dhairi kwamba ni msaliti na sio mkwel hata kidogo na anatumia upendo wako kwake kukunyanyasa na kuto kukusamehe kisa kupigwa Kofi nakushauri piga kibuti atarudi tu mwenyewe
 
Wewe unatakiwa uoe kwenu ili muwe mnapigana vizuri na dada zako.
 
Mi sijaona kosa lako...tatizo moja tu, hukuwa umejiandaa kwa impact ya maamuzi uliyoyachukua...kwanza yeye ndiye mwenye makosa kwann akudanganye kuwa yupo home .?? Kingine unaonekana wewe ndo unamuhitaji sana kuliko yeye anavyokuhitaji, kwanini baada ya kumshikisha adabu ukaenda tena kumpigia simu.? Ungekaa kimya siku kadhaa aanze yeye kukutafuta, akiwa kimya na wewe kula buyu..

Kuhusu kuachwa wala kama anakupenda hawezi kukuacha msikilizie siku kadhaa atajileta mwenyewe kwa phone..na wewe uweke ka-mkwala ka kiume sio unajiwahi kuomba msamaha wakati hata kosa lako hulijui...yaani unajigeuzia kibao mwenyewe...?????arrrrggghhhhaaaa...!!
 
sii kiivo kawaida inatakiwa mwanamke umnusue kidogo sometimes
 
Hapo hakuna mke kaka....ka kwel yule ni kaka ake kwann akudanganye kua yupo nyumban anapka.....hata hakuna haja ya kumuomba msamaha...labda yeye ndo akuombe huo msamaha...let her go 4 ya own good.
 
Haaa..haaaa..Mkuu umenifurahisha...jamaa baada ya huduma ya miezi mitatu anahisi hati miliki anayo yeye peke yake...!

Yeye akubaliane na ukweli tu, kama hawezi kukaa kwenye foleni, aendelee na yake la sivyo atampiga sana huyo binti kwa sababu ya surprise nyingi atakazokutana nazo.
 
Yeye akubaliane na ukweli tu, kama hawezi kukaa kwenye foleni, aendelee na yake la sivyo atampiga sana huyo binti kwa sababu ya surprise nyingi atakazokutana nazo.

Labda pia atueleze walikutana mazingira yepi..usijekuta naye alimkuta huko huko.
 
Kwanza unampiga mkeo? umemtolea mahari? mahusiano ya miezi mi3 unampiga yangekua miezi sita? au akitimiza mwaka na meno hana, Mwanamme anatakiwa awe muelewa ungemuuliza kwa hekma na upole ungejua yote lakini kwakipigo anajitambua huyo mwanamke ndio mana anaona naiwe basi, ivi mpaka leo kuna wanaume wanaopiga wanawake kweli?
Kaka kama mmeshindwana TABIA muache na huo mchezo kwanza amekufundisha nani au umeona wapi? huyo ni mtoto wawatu unampiga kofi na anakufia unafanyaje? tumia busara sana mara nyengine,sorry kama ntakua nimeongea sana.

Mimi nadhani jambo la msingi ni kulaani tabia aliyoifanya ya kumpiga huyu dada. Na kwa kiasi kikubwa kutokuonyesha uvumilivu. Suala la kusema hajamtolea mahari au sio mkewe sioni kama lina mantiki, kwani kwa wake za watu na wale waliotolewa mahari kwao ruksa kupigwa? Na kama hajatolewa mahari kwa nini anakula vya watu?
 
nyaggad

Mapenzi ya walevi humalizwa na walevi,nenda kaombe ushari kwenye ile ile bar uliomkuta.Cha kufanya,nenda pale Bar itisha CC na sekretariet ya bar halaf mwaga agenda,ikiwa wanahisi unafaa kukatwa jina lako basi watamshauri demu akukate jina lako..Unaweza ukamualika na kada yyte wa CCM ahudhurie,napendekeza mualike mtia nia yyte.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom