Eti ameniacha kisa kofi moja tu

Eti ameniacha kisa kofi moja tu

Kwanza unefanya kosa kubwa kumpiga
Ungepaswa kumfata na kuniuliza labda kweli alikuwa ni kaka yake ila na yy pia ni muongo ingekuwa ni kaka yake asingekudanganya yuko home
Nakushaur usije unatisha kosa la kumpiga mpenz wako kumbuka hata Pete hujamvalisha . Yaelekea unahasira sana kaka ww kama unampenda vumilia mbembeleze au kama VIP tafuta mwingine muda 3 sio mingi sana
 
Wewe nae una matatizo, kama alikuwa na kaka yake, kwanini akudanganye? Hujiulizi tu? Huyo hajafanya maamuzi, ingia barabarani kutafuta mwingine, acha kumpigia kabisa. Na huo mkwara wa yeye na wewe basi ni kwa sababu anajua yeye ndie mwenye makosa. Mara nyingi alie na kosa huwa anaoverdo mambo akidhani ndicho kinachopaswa kufanyika ili ionekane kweli. Angekuwa mkweli, angetaka kukuumbua palepale kwa kumuita kaka yake athibitishe kuwa ni kweli wana undugu.
Hivi mbona mnakuwa mazuzu kirahisi hivyo? Mtu unataka kumuoa, adanganye yuko home, umkute bar yuko na jamaa, anadai nivkaka yake baada ya kuwa umempiga kibao, kwanini asimuite huyo kaka amtetee?
 
Wewe nae una matatizo, kama alikuwa na kaka yake, kwanini akudanganye? Hujiulizi tu? Huyo hajafanya maamuzi, ingia barabarani kutafuta mwingine, acha kumpigia kabisa. Na huo mkwara wa yeye na wewe basi ni kwa sababu anajua yeye ndie mwenye makosa. Mara nyingi alie na kosa huwa anaoverdo mambo akidhani ndicho kinachopaswa kufanyika ili ionekane kweli. Angekuwa mkweli, angetaka kukuumbua palepale kwa kumuita kaka yake athibitishe kuwa ni kweli wana undugu.
Hivi mbona mnakuwa mazuzu kirahisi hivyo? Mtu unataka kumuoa, adanganye yuko home, umkute bar yuko na jamaa, anadai nivkaka yake baada ya kuwa umempiga kibao, kwanini asimuite huyo kaka amtetee?

Mkuu nilitaka niseme hivi hivi. Hongera kwa kuiba point yangu...


Toka lini mdogo mtu na kaka mtu wakakaa bar !?
 
nyaggad

Usipoteze muda ....mim napataga hasira sana mtu akibidanganya bt siwez mim kumpiga mtu.
 
Last edited by a moderator:
Kama alikuwa na kaka hapakuwa na sababu ya kukwambia uwongo na pia asingeshtuka kukuona na vilevile asingekimbia..nadhani alikufanya ATM. Ndo dada zetu walivyo ck hizi..walio wengi japo wapo waaminifu wachache

Ni kweli uyasemayo mkuu!
 
Habari,wandugu natumaini mko poa, mmi Nina mpenzi wangu tumekuwa nae kwenye mahusiano huu ni mwezi wa tatu,sio siri huyu binti nampenda sana, nimejitahidi kumhudumia kadri niwezavyo kwa mda mfupi nilikuwa nae, kwa sababu Nina nia ya kumuoa,sasa juzi nilikuwa na rafiki Yangu tupo maeneo ya Sinza tukapita kwenye bar moja hivi ghafla nikamuona mpenzi wangu nae yupo mle ndani ya bar anakunywa kinywaji wakiwa wamekaa na mwanaume mmi simjui, ndipo nikaamua kumpigia Simu mpenzi wangu nakumuuliza yuko wapi.

Akapokea Simu nakunijibu yupo nyumbani kwao anapika na wakati minamuona yupo na kijeba wanakunywa vinywaji huku wanacheka, sio siri nilipatwa na hasira ndipo nikaamua kumtuma rafiki Yangu akamuite ili niongee, aliponiona alishangaa na aliponisogelea2 sikumsemesha neno lolote nikampiga Kofi moja la nguvu rafiki Yangu akanishika mikono na watu wakajaa kidogo, nikaamua kuondoka na yule binti akawa amekipingia.

Sasa zimepita siku mbili yule binti nimempigia Simu akapokea akaniambia yule alikuwa kaka yake mtoto wa baba yake MDOGO na pia ameniambia mmi na yeye basi amesema hawezi kuishi na mtu kama mmi tena, nimejaribu kumuomba msamaha lakini wapi amekataa katakata, naombeni msaada wa mawazo jamani nifanyeje?

Eti Kofi moja2 lini koseshe mke jamani?

Wewe Ni Muongo!

 
Mkuu nilitaka niseme hivi hivi. Hongera kwa kuiba point yangu...


Toka lini mdogo mtu na kaka mtu wakakaa bar !?

Hahaha! Nimekuwahi sio? Kwanza kukaa Bar mkiwa ndugu si tatizo hata kidogo inategemea tu na culture ya ndani ya ukoo/familia n.k Ila issue ni kwamba, wewe upigwe kibao wakati kaka yako yuko karibu, ukivumilie kimya kimya bila kumuita akutetee kweli?
Unaficha nini?
Okay, baada ya vumbi kutulia, unaugulia kofi, na labda ulisahau kuwa kaka yupo bar baada ya kula kibao cha ghafla, sasa umetulia, kwanini usimuumbue aliekupiga kwa kumuita kaka athibitishe kuwa mna undugu?
Kumbuka aliekupiga kibao ni mtu rasmi, mchumba huyo ambae kama hujamtambulisha, basi utamtambulisha soon nyumbani so hakuna siri. Na kingine ni kuwa huyo mwanaume unampenda na hutaki apate picha tofauti akuache, kweli bado utimue mbio kutoka eneo la tukio tu? Unakimbia nini?
Au basi una hasira sana, kakudhalilisha mbele za watu, kwanini na wewe usimuumbue hadharani kuwa kakosea ili watu waone kwa kumuita kaka yako aje amthibitishie ili aumbuke? Na ikiwezekana na yeye apigwe vibao na kaka yako au apelekwe polisi?
Bado tu unaomba msamaha kweli? Hayo yote mtu hujiulizi kweli?
 
Eti nipo nyumbani wakati yupo bar, ungeenda tu pale kuonyesha kama umemuona nadhani ingemuuma kuliko ulivyompiga, kiufupi wote mna makosa sitetei upande wowote, inabidi muombane msamaha nyote ila kwa hulka ya wanawake usitegemee hilo
 
Wewe nae una matatizo, kama alikuwa na kaka yake, kwanini akudanganye? Hujiulizi tu? Huyo hajafanya maamuzi, ingia barabarani kutafuta mwingine, acha kumpigia kabisa. Na huo mkwara wa yeye na wewe basi ni kwa sababu anajua yeye ndie mwenye makosa. Mara nyingi alie na kosa huwa anaoverdo mambo akidhani ndicho kinachopaswa kufanyika ili ionekane kweli. Angekuwa mkweli, angetaka kukuumbua palepale kwa kumuita kaka yake athibitishe kuwa ni kweli wana undugu.
Hivi mbona mnakuwa mazuzu kirahisi hivyo? Mtu unataka kumuoa, adanganye yuko home, umkute bar yuko na jamaa, anadai nivkaka yake baada ya kuwa umempiga kibao, kwanini asimuite huyo kaka amtetee?

Sikubali umeniigia hahahaa(joke)
 
Kama ni ndugu yake kwa nn akudanganye yuko home anapika? Think big
 
Mkuu nafikiri utakuwa na matatizo ya fikra...unataka ushahidi gan tena kuwa huyo mwanamke siyo muaminifu???acha upuuzi acha kulialia katika maswala yakipumbavu...huyo hakufai
 
Wewe na yeye nyote mna makosa.

1. Wewe: Kwa nini unyooshe mkono wako kumpiga mwanamke? Regardless kakufanyia nini...

2. Yeye: Kwa nini akudanganye?

Salama yenu muachane tu kwa amani...move on bro!
 
umefanya kosa kubwa sana kumpiga mtoto wa watu bila hta kumuuliza aliyekaa naye ni nani

ukaamua kuchukua silaha mkononi ona sasa ushakosa maji ya moto

kumbuka kuwa

HASIRA HASARA UMESHAJIKOROGA UNA BUDI KULINYWA

hata ingaekuwa mm umenidhalilisha kwa watu kiasi hicho umenipiga bila sababu nakusepa tu kimtindo bila hata kupiga honi

Unadhani kwa nini alishindwa kusema ukweli? Alistahili makofi zaidi kwa kosa la uongo.
 
Back
Top Bottom