ESTIM Construction ni kampuni ya nchi gani?

Kazi zinadesigniwa na wahandisi washauri, wao wanafuata michoro tu

Kuwa wachina walikimbia kazi ni uongo!..haukupendezi umri huu


Kuwa waachiwe kazi zote, ni upuuzi pia ambao nikianza kuuchambua, utaharibu Idd yako


Usiyoyajua uliza!

Hakuna mtu yeyote atakayewapa kazi estim bila ushindani!..kuwapa wao tu unavunja sheria ya manunuzi PPRA
 
uko sawa kiasi,estim walikuwa sub contractors wa konoike enzi konoike wakiwa na kambi ubungo zilipojengwa hostel mpya,kazi yao kubwa ilikuwa ni kutengeneza makalavati,cabstone na road barriers,Mmiliki wake ni Giri ambaye ni mtanzania mwenye asili ya india,mtu poa sana...muhindi wa kwanza kumuona mwenye utu! alikuja kununua vifaa vya konoike na kambi yao pale mikocheni cocacola
 
Estem inamilikiwa na mtanzania mwenye asili ya India anaitwa GIRI ofisi zake zipo pale kama unaelekea ITV jengo ilipo kampuni ya MM steel na Sayona kampuni za Shubash, huyu jamaa ni swahiba mkubwa sana Shubash , kwa wale wakongwe wenzangu huyu jamaa alianza enzi hizo miaaka ya 90 akitengeza the best finished fenitures hapa jijini ndiyo baadaye akaanza kupata miradi ya ujenzi baada ya kuwa karibu sana na viongozi wa serekali hasa wa awamu ya nne.

Huyu ndiye alipata deal la kujenga jengo la umoja wa vijana ccm ambapo mkataba wake uligubikwa na rushwa na ufisadi ndiye mmiliki wa hizo appartment hapo karibu na jengo la imoja wa vijana ccm

Ukiacha Eastem ana vikampuni zaidi ya kumi na vinafanya biashara mbalimbali, pia anamiliki zaidi ya magorofa 20 maeneo mbali mbali hapa jijini, mikocheni na upanga.
 
Duh!

Zote zake?
Wewe nawe jiongeze,huoni kuwa neno nyanza linapatikana usukumani!! So by now ushajua uwanja wa ndege wa kimataifa wa chato ulijengwa bila idhini ya bunge na kampuni gani
 
Unamaanisha kuwa hiyo M katika hilo jina la kampuni ni kifupi cha jina la aliyekuwa mheshimiwa waziri wa ujenzi? Umesikia wapi kama si umbea? Kama ni umbea usilete humu JF.
Mwana wa nuru asiyependa ukweli!
 
Mzee baba hii barabara haina tuta hata moja.. ni mwendo wa zebra na vibao vya 50.. unaendesha kwa raha zoote..

Funika bovu ni Kahama to Rusahunga kupitia Ushirombo,Runzewe na Nyakanazi ni barabara bora sana sijui kwa kuwa inaenda Rwanda kwa Kagame..
 
MKEHA,
Acheni mapenzi ya gizani na estim.

Barabara waliyojenga chini ya konoike, Mwenge-Tegeta haina viwango na walipiga cha juu ikabidi Konoike warudie sehemu zilizokuwa mbaya sana.
 
Unapotosha.. Contractor alikua Konoike na estim alikua ni moja ya sub contractor wa konoike na walikuwepo ma sub contractor wengi tuu kila mmoja na eneo lake.

Hata sasa ivi tunapo ongea estim ni sub contractor wa BAM pale terminal 3 sidhani kama utamlaumu estim kwa ubovu wowote wa terminal 3 au utamsifia estim kwa ubora wowote wa terminal 3.

Tofautisha contractor na sub contractor.
Acheni mapenzi ya gizani na estim.
Barabara waliyojenga chini ya konoike, Mwenge-Tegeta haina viwango na walipiga cha juu ikabidi Konoike warudie sehemu zilizokuwa mbaya sana.
 
Tupo tunaojua kilichojiri,wewe unakariri ulichoambiwa.
Sub contract yote kujenga barabara Mwenge Tegeta ilikuwa ya estim, chini ya marehemu Jagdish.
Estim walivurunda, na hata leo lami ina matuta.
 
Kama na akili mbovu niambie mradi wowote ambao walau umelalamikiwa kwamba umejengwa chini ya kiwango.


Hata kampuni yako ingefanya vizuri ningefanya the same.

Kuna makapuni kibao yanachoma kodi za wananchi.

Bagamoyo Msata wamejenga hao Estim na kulingana na viwango vya kitaamu ile layer ya lami ilifeli ikasababisha mipasuko na waliamriwa warudie ile kazi. Sasa sijui hapo mbona hukupaona.
Halafu usiwasifie tuu hii kupanda majani ni sehemu ya mkataba na si wao wanaamua tu. Hata ingekuwa Kampuni X wanajenga ingekuwa ni lazima kupanda hayo majani. Uwe unauliza kwanza na si kupayuka tu
Lakini kama umetumwa it’s okay
 
Mkuu estim wamejenga madaraja tuu.. sehemu nyingine zimejengwa na mchina.
 
Endelea na tafiti, utapata source baada ya muda.
 
Kama ndio welijenga Tangibovu - Goba - Mbezi basi hawa jamaa wapo vizuri.
Nikipita ile barabara huwa naikubali sana.

Vilevile haohao ndio waliojenga Tegeta Mwenge umeuina? Ba walijenga kupitia Konoike
 
Mkuu estim wamejenga madaraja tuu.. sehemu nyingine zimejengwa na mchina.
Du....kweli eewe ndio hujui kitu.
Mchina hakutia mguu mradi wa Msata Bagamoyo.
Kazi ilikuwa estim mwanzo mwisho, tena kwa gharama za kutisha Tshs 2bn kwa kilometa!
Ulizia Tanroads upate facts.
Hapa si chit chat.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…