ESTIM Construction ni kampuni ya nchi gani?

ESTIM Construction ni kampuni ya nchi gani?

Estim hata enzi za JK kajenga kwa weledi mzuri sana.
Tatizo la kujenga miundombinu mibovu na isiyokuwa ya kiwango linaanzia kwenye tenda, ili ushinde tenda na kupewa kazi mnakaa mezani kwanza, mzabuni anaweka cost zote kukidhi viwango kutokana na TOR, anasema itagharimu 300bil, afu jamaa wanamwambia ili tukupe kazi 150bil ni zetu. Kwa kuwa mzabuni hataki kukosa kazi, anakubali anajibana na kutoa kitu kisicho na ubora kuhofia kukosa kazi siku za mbele.
Kuna co. Inajenga barabara kutoka sinza kijiweni kwenda tandale, kutoka tip top Hadi mtogole, anajenga mifereji kwa kwa zege na nondo zilizosukwa kwa uhakika. Akatokea mkuu mmoja kukagua akasema barabara zinajengwa kwa ghalama kubwa km chache. Hapo engeneer si itabidi aachane na viwango akidhi quantity? Siasa na rushwa ndivyo vinajenga barabara mbovu na si maengeneer
 
Iyovi mafinga walijitahidi.. japo kuna maeneo walizingua.. ila ni moja ya barabara za kimataifa tanzania. Mafinga igawa iliyo zinduliwa na magufuli juzi ni balaa.. ni mkeka mkali kuliko yote tz.
Na moja ya barabara zilizojengwa kwa viwango ni barabara kutoka Iyovi hadi Mafinga, na wale wanajenga Mafinga Mbeya, hata ile ya Masasi, tunduru si mbaya ukolinganisha na ya mbagala

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe una personal interest, andiko lako lina bias.
Anayefahamu ubora wa hiyo kampuni ni client na consultant wa project.

Unafanya kazi ya kupiga debe ndugu, kazi zinatolewa kwa kushinda zabuni kwa mujibu wa regulator PPRA.
 
Gullam,
Huku Swax kuna Sumry enterprises anajenga vizuri,kuna ile sigh and sons ya Moshi inajenga vizuri na nyingine nyingi za kibongo,,ujenzi wa barabara ni less complicated kuliko majengo marefu
 
Ila waliojenga barabara ya Dodoma Iringa ni shida barabara imeanza kuwekwa viraka hata miaka 3 haijafika!
Tatizo pale ni usimamizi afu nilichunguza ile barabara nikagundua pavement layers zilitumia materials waliyo cut ile milima ukiangalia ni ile miamba laini iko kama mabapa mabapa chunguza cutting mule kwenye milima,aina ile ya materials sio ngumu
Pili sijaona kambi waliyokuwa wanasagia kokoto nzuri na pili eneo lile halina maji ya kutosha zaidi ya mtera so nadhani maji hayakutosha na mwisho ni kama tabaka la lami ile thickness ni nyembamba sijui ni single dressing au vp waliosimamia watuambie.Kiufupi consultant alizembea
 
Rostam Aziz-->Caspian--Estim--Masasi Construction--Kasco Construction--Nyanza Construction

Najaribu kuota
Uwongo mtupu, Estim ni kampuni ya akina Patel wenye MM.steel, Kiwanda cha Sayona, hoteli za Whitesands na Sea Cliff. Tena katoa udhamini kwa Taifa Stars wakae Whitesands wakijiandaa kwenda Misri pia Patel ni swaiba wa MZEE wa Msoga walisoma pamoja Lugoba zama hizo.
 
@mafili unaujua uhusiano wa Jeetu/Subhash Patel, R.A na jamaa mmoja alishakimbia nchi Shailes Vithlan?

Ni vile tu R.A amecash in kampun zake nyingi
 
Sasa ile ndio nilikuambia ni aina ya moja ya viwango vya barabara za rami. Ile ni ya Kiwango cha tatu, inaanzia nduli Airport mpaka maeneo ya Mkonze unapoingia Dodoma. Ndio single surface dressing.
Hapo sawa kumbe observation yangu iko powa ila walio design waliwaza nini wakati hii barabara inabeba malori zaidi?
 
Yes kiwanda cha nondo ni mm steel na ESTIM ofisi zao ni opposite na Mm steel na kampuni hizi mbili ndizo zilizoingia ubia na kujenga mradi wa jengo la Uvccm
 
Yes kiwanda cha nondo ni mm steel na ESTIM ofisi zao ni opposite na Mm steel na kampuni hizi mbili ndizo zilizoingia ubia na kujenga mradi wa jengo la Uvccm
Basi huyu jamaa ni shida.. maana estim kwa sasa inashindana na China Civil, China railway, Bam, straberg etc.
 
Back
Top Bottom