Tabutupu
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 13,262
- 18,706
- Thread starter
- #41
Estim hata enzi za JK kajenga kwa weledi mzuri sana.
Tatizo la kujenga miundombinu mibovu na isiyokuwa ya kiwango linaanzia kwenye tenda, ili ushinde tenda na kupewa kazi mnakaa mezani kwanza, mzabuni anaweka cost zote kukidhi viwango kutokana na TOR, anasema itagharimu 300bil, afu jamaa wanamwambia ili tukupe kazi 150bil ni zetu. Kwa kuwa mzabuni hataki kukosa kazi, anakubali anajibana na kutoa kitu kisicho na ubora kuhofia kukosa kazi siku za mbele.
Kuna co. Inajenga barabara kutoka sinza kijiweni kwenda tandale, kutoka tip top Hadi mtogole, anajenga mifereji kwa kwa zege na nondo zilizosukwa kwa uhakika. Akatokea mkuu mmoja kukagua akasema barabara zinajengwa kwa ghalama kubwa km chache. Hapo engeneer si itabidi aachane na viwango akidhi quantity? Siasa na rushwa ndivyo vinajenga barabara mbovu na si maengeneer
