ESTIM Construction ni kampuni ya nchi gani?

ESTIM Construction ni kampuni ya nchi gani?

Kuna kampuni ilikuwa inaitwa KOJIFA. Ilikuwa ni kampuni ya kiitaliano ilijenga bara bara Mwaka 1996 kutoka Sirari wilaya ya Tarime mpaka Makutano wilaya ya Musoma, ile kampuni ilikuwa inajenga bara bara zenye ubora wa kiwango cha hali ya juu, mpaka leo hii ile bara bara ni imara. Kwangu Mimi ile ndo kampuni bora.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ohooo tayari usharambishwa asali kwa kidole cha kati

Haya tumekusikia ila mwambie aliekutuma kwamba kampuni za ujenzi zina mamna ya kutathmini ubora wake na sio kuangalia kwa macho yako halafu unapitisha wapewe !!!

Nafkiri Ma'engineer na wadau wa barabara huwa hawatumii utaratibu wa kuangalia kwa macho na kupitisha kwamba APEWE !!! kuna vigezo vingi wanaangalia Ndg. Yangu Tabutupu Wakuvanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama na akili mbovu niambie mradi wowote ambao walau umelalamikiwa kwamba umejengwa chini ya kiwango.


Hata kampuni yako ingefanya vizuri ningefanya the same.

Kuna makapuni kibao yanachoma kodi za wananchi. Gullam,
Mwanzoni niliamini ni mtu anayetaka tu kujua hii kampuni, ila kwa comment hii, wewe ni sehemu ya hiyo kampuni na ulikuwa unafanya matangazo hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wame secure tena Tender ya Kujenga Ofisi ya Makao Makuu ya CCM, Tambuka Reli Dodoma
Kama Mkandarasi Mkuu
 
Katika uchunguzi wangu wa miradi ya barabara nimegundua kampuni inayojulikana kama ESTIM inajenga barabara zenye ubora wa hali ya juu sana. Cha ajabu zaidi hawa ESTIM wapo vizuri sana kwenye madaraja na majengo hasa yale makubwa.

Kuna picha nimeona wanavyo jenga barabara ya Kimara kibaha kule Dar es salaam. Kilicho nivutia ni jinsi wanavyo jali mazingira kuhakikisha kwamba sehemu ambazo wameharibu uoto wakati wanajenga wanajitahidi kurudiashia uoto huo kwa kupanda nyasi na miti hata kabla barabara haijaisha kitu ambacho sijakiona kwa kampuni nyingi za kichina.

Jambo kama hilo limeonekana hasa kwa wale jamaa wanaojenga SGR pekee.

Pamoja na hayo yote hawa jamaa wanaonekana kuleta namna mpya ya ujenzi wa barabara zenye quality.

Baadhi ya barabara niliwahi kuipita ni ile ya Goba jijini Dar es salaam sijui kwa sasa kama bado nzima lakini kwa ujenzi ule naamini hadi sasa itakua bado imara.

Kuna wachina walipewa kujenga barabara ya Bagamoyo Msata, nasikia waliopoona lile bonde walikimbia, nasikia kazi iliyo fanywa na ESTIM ya kujenga Madaraja katika bonde lile ni ya kutukuka.

Sijajua kampuni hii inatoka nchi gani lakini serikali inahitaji kuitambua kwa mchango wake.

Mapendekezo

Kwenye issue za madaraja waachiwe hawa jamaa.

Barabara za magari makubwa waachiwe hawa jamaa.

Majengo ya taasisi kama vyuo etc waachiwe hawa jamaa.

Nasema kutoka moyoni, sijawahi kusikia kashfa ya kazi mbovu toka hii kampuni.

Kama ipo ni ya bahati mbaya.View attachment 1118532
Ipewe barabara zote za tz tuachane na hawa watching
 
Back
Top Bottom