Esther Bulaya (MB) Achemka Katika Interview EATV Chanel 5...!

Esther Bulaya (MB) Achemka Katika Interview EATV Chanel 5...!

Status
Not open for further replies.
Pamoja na kuonekana amechemka ila nasikia ni kipenzi kikubwa kwa wananchi wa jimbo la Bunda, na kwa kiasi kikubwa anatishia maisha ya kisiasa ya Mzee Tyson, watu wa Jimbo la Bunda wanaweza kutupatia ukweli

Inawezekana Esther akawa anatishia maisha ya Kisiasa ya Mzee Tyson ndani ya CCM si zaidi ya hapo (kwenye kura za maoni). Nje ya CCM hawezi kufurukuta. Ni kweli amejitahidi kuanzisha mashindano yake ya mpira ili kukusanya vijana na kujiweka sawa, lakini hata yeye anajua hawezi kushinda jimbo hili la Bunda. Ninazo sababu mbili kubwa za kusema hivyo, Mosi; Kwa mujibu tu ya mazoea, mila za Mkoa wa Mara, bado ni ngumu sana sana kwa mwanamke kuongoza jimbo lolote ndani ya Mkoa wa Mara, Pili, Kwa sasa CHADEMA ina nguvu za kutisha katika jimbo hili la Bunda na dalili zote za CHADEMA kuchukua jimbo hili ziko wazi kabisa labda wenyewe wajichanganye kwenye kuleta aina mgombea. Mzee Tyson alilijua hili na ndio maana anafanya jitihada ya kukata jimbo la mjini lijitegemeee na yeye agombee eneo la juu kuelekea Nyamuswa na Esther anajikita mjini ambapo hawezi kuonja hata halufu ya ushindi. Ushahidi anayo Nape na Katibu wake walipokuja katika ziara zao za kutembelea kanda ya ziwa
 
Mbunge wa viti maalum kupitia kundi la vijana toka chama cha mapinduzi akiwakilisha mkoa wa Mara wilaya ya Bunda alikuwa akifanyiwa mahojiano katika kipindi cha ''hot mix'' kinachorushwa kupitia kituo cha television cha EATV - Chanel 5!

Akaulizwa swali kuwa nje ya siasa anapenda kufanya shughuli gani?mojawapo ya shughuli aliyoitaja kwamba huifanya ni pamoja na kusoma vitabu na kusikiliza hotuba za wanaharakati kama Martin Luther King Jr., Mwalimu Nyerere na Mandela!
Katika kukoleza maelezo yake akasema anapenda sana kusoma kitabu kinachoitwa ''How to be a Good Political Leader''. Mtangazaji akamuuliza jina la Author wa hicho kitabu lakini mheshimiwa mbunge akashindwa kumtaja kwakuwa alikuwa hamkumbuki pamoja na kuomba apewe muda ili amkumbuke!!

MY TAKE:
Kwa mtazamo wangu si rahisi mtu kusahau jina la author wa kitabu unachokipenda kukisoma mara kwa mara! Pengine Mh.Esther alikuwa anatafuta mileage kwamba ni msomaji mzuri wa vitabu lakini kachemka kwa kutomjua author wa kitabu akipendacho!

Huna kazi, katafute kibarua, kwani wewe kutuletea huu ujinga unatafuta nini? Uonekane ili mradi umechangia JF. Waste of time
 
Mbunge wa viti maalum kupitia kundi la vijana toka chama cha mapinduzi akiwakilisha mkoa wa Mara wilaya ya Bunda alikuwa akifanyiwa mahojiano katika kipindi cha ''hot mix'' kinachorushwa kupitia kituo cha television cha EATV - Chanel 5!

Akaulizwa swali kuwa nje ya siasa anapenda kufanya shughuli gani?mojawapo ya shughuli aliyoitaja kwamba huifanya ni pamoja na kusoma vitabu na kusikiliza hotuba za wanaharakati kama Martin Luther King Jr., Mwalimu Nyerere na Mandela!
Katika kukoleza maelezo yake akasema anapenda sana kusoma kitabu kinachoitwa ''How to be a Good Political Leader''. Mtangazaji akamuuliza jina la Author wa hicho kitabu lakini mheshimiwa mbunge akashindwa kumtaja kwakuwa alikuwa hamkumbuki pamoja na kuomba apewe muda ili amkumbuke!!

MY TAKE:
Kwa mtazamo wangu si rahisi mtu kusahau jina la author wa kitabu unachokipenda kukisoma mara kwa mara! Pengine Mh.Esther alikuwa anatafuta mileage kwamba ni msomaji mzuri wa vitabu lakini kachemka kwa kutomjua author wa kitabu akipendacho!

- Ok So what?

Le Mutuz
 
- Ok So what?

Le Mutuz
Kama hujaelewa kalale utakuwa umechoka, kesho ukiamka rudia kuisoma na kuangalia coments za wenzako unaweza ukaelewa na ikishindikana uliza tena tutakuelewesha. KALAMBALALE UKATEELE (KALALE UMECHOKA).
 
Alidhamiria kudanganya lakini mungu akampiga kikumbo , badala ya kusema anapenda kuangalia sinema za kanumba akataka kutupiga changa la macho , poor we dada esta !
 
ukisema taarabu utakuwa unakosea,esta husikiliza nyimbo za komba tu kama vile ule wa "TIENI TIENI KWA MOYO MMOJAA....."
Dada Ester anauzika,chongeni sana na sanamu lenu,tena nakumbuka Tyson alikuwa mgeni rasmi kufungua bwawa la kunyweshea mifugo alipoinama kuangalia maji,akawauliza wanazengo; mmeshaanza na kufunga mamba? Watu tehe tehe tehe tehe.
 
wabongo kila kitu kusiliba,kwani hapo juu nani yuko perfect hajawahi kukosea jambo??????????
 
Mnajadili chakula cha watu,hamjui kwamba mtu kawekeza pale
Mh. Bulaya simama mungu yu pamoja nawe,maadili ya vijana wenzako ndo haya peleka mswada bungeni ili viboko viendelee mashuleni. Napenda sana unavyoongea kwa data,kujiamini na unavyovaa kiasilia na usivyo mbaguzi hata kwa wabunge wa upinzani, wewe na January Makamba mtafika mbali msikate tamaa na wana JF kwani wengi hasira za maisha magumu tunazimalizia humu na si kingind.
 
Huna kazi, katafute kibarua, kwani wewe kutuletea huu ujinga unatafuta nini? Uonekane ili mradi umechangia JF. Waste of time

Sasa wewe mwenye kazi ya kufanya mbona tena umekuja kuchangia uzi huu wa mtu asiye na kazi?
 
Ritz acha kutumiwa na genge la wahuni wa lumumba kum-defence wa wasira,tunajua wasira ana hali mbaya sana bunda kisiasa na kwa taarifa yako bulaya vijana wengi wanamkubali tafauti na huyo mnaempenda hapo lumumba wasira

Toa takwimu ya kata na vijiji ili tukuaibishe.
Tafuta nafasi ongea na huyo dada anaweza kukwambia ukweli kuhusu Bunda. We acha dogo, achana na magazeti ndugu yangu Wasira ni habari nyingine.
 
kipindi nipo 6 mwaka 2008 nilikuwa napenda kusoma Think Big na Gifted Hands vya Ben Cassons,sasa huyu hajui author wa kitabu anachokisoma mara nyingi.Adrian njoo umtetee Muheshiwa

Ben nan? Ni kosa la jinai kukosea jina la mwandishi wa kitabu husika.
 
Esther Bulaya wala siyo kiongozi kama anavyojitanabaisha. Tena anajitahidi sana kukaa karibu na Halima Mdee ili amsaidie mambo ya kiuanaharakati, lakini wapi! Hawezi kuwa mwanaharakati hata chembe.
Ni kweli yuko karibu na Halima Mdee ili asaidiwe mambo ya harakati?

 
Alidhamiria kudanganya lakini mungu akampiga kikumbo , badala ya kusema anapenda kuangalia sinema za kanumba akataka kutupiga changa la macho , poor we dada esta !
Umeona eeh!! Esther Bulaya alitaka kujionyesha yeye wa kivile kumbe wapi.

Kwa tunaomjua vizuri Esther Bulaya mbali na siasa anapenda zaidi kwenda Disko kujirusha na muziki, kujichanganya na wanaume usiku kwenye kumbi za starehe na pia kushiriki michezo mbalimbali.

Msomi wa vitabu huwa hajifichi, kuanzia kuongea mpaka kuandika, lakini sio Esther Bulaya.
 
unakumbuka Mh.tyson alimpiga mkwara kwamba yeye si msemaji wa wananchi wa Bunda, kuhusu habari za fidia?
Msimpagawishe Esta jamani, hata yeye anajua kuwa akisimama kwenye uchaguzi hatakaa apite. Alipata ubunge wa viti maalum kwa jinsia yake tuu. Mara, mwanadada huyu hatakaa apate kwa kura.
 
Kweli watanzania sisi tunahali mbaya kama hii ndo hoja ya kujadili wakati yapo mengi ya kujadili.kamwe siwezi kushangaa madudu yanayofanya na viongozi wetu kwani hii inaonyesha kabisa jamii tulio nayo.Safari ndefu sana kwakua hata wale nilifikiri wanajitambua kumbe wana hali mbaya sana,yani inakua tatizo mtu kusahau jina la mwandishi?
Juzi kulikua na hoja ya matumizi mabaya ya ID ya Dr Slaa wale waliokua wanasema ni hoja ya kijinga na kunamengi ya kujadili ndo hao wanajadili Esther kusahau jina la mwandishi.
kazi kweli.
 
kiukweli mnapochagua wawakilishi wenu kuweni makini sana, kweli mbunge huyu katudharirisha sana watanzania maana hii runinga inaangaliwa africa mashariki kote. kweli hata hajui tofauti kati ya hobby na kazi? nilishangaa sana amekomaa anaendelea kusema pia anapendelea kupika pilau, alipoulizwa siyo ugali wa udaga akasema hiyo hajataja kwasababu ni kawaida tuu kwake. hivi kwa kusikiliza hotuba, kupika pilau na kusoma vitabu anaingiza bei gani? unategemea mbunge km huyu atakuwa na uwezo wa kutafta ufumbuzu wa tatizo la ajira kweli? inaudhi sana hivi mf. angekuwa ndo anahojiwa na bbc, cnn, rf, aljazra au dw si aibu kubwa duniani? inaonesha ni kiasi gani hayupo makini kwa vitu vidogo vyenye madhara makubwa. plz tuwasikilize tuwakosoe hakuna haja ya chuki hapa.
 
Pamoja na kuonekana amechemka ila nasikia ni kipenzi kikubwa kwa wananchi wa jimbo la Bunda, na kwa kiasi kikubwa anatishia maisha ya kisiasa ya Mzee Tyson, watu wa Jimbo la Bunda wanaweza kutupatia ukweli

Kipenzi cha watu wa bunda!!! Man usiongee vitu usivovijua, bunda yupo jembe la cdm papaa pius muulize huyo asiyemfaham mwandishi wa kitabu anachokipenda atakwambia
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom