Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 17,644
- 27,740
Esmail Qaani Yuko Hai Israel: Siri ya Usaliti Mkubwa Mashariki ya Kati
Ripoti za kijasusi zimeibua tetesi nzito zikidai kuwa Esmail Qaani, mkuu wa Kikosi cha Quds, yuko hai nchini Israel baada ya kutoroka Iran kwa siri. Inadaiwa Qaani alishiriki kikamilifu kutoa ramani na siri zilizopelekea kuuawa kwa Ismail Haniyeh kule Tehran, Hassan Nasrallah kule Lebanon, na viongozi wengine waandamizi wa Hezbollah.Habari hizo zinadai kuwa Qaani alipanga njama za ndani dhidi ya Ayatollah Khamenei kabla ya kutoroka kupitia mpaka wa siri. Inasemekana sasa anahifadhiwa na Mossad nchini Israel kama shahidi mkuu, huku akitoa siri za kijeshi za Iran baada ya kuona mfumo wa uongozi wa Tehran ukitetereka