ESCROW sio siri tena, mambo yote hadharani

ESCROW sio siri tena, mambo yote hadharani

ANaweza kuzuia tu haya yasitokee tena inatosha!Kufukua mambo ambayo hukuwa na maamuzi nayo sioni kama kuna umuhimu!Kila zama na kitabu chake
Hao watumishi hewa anaoshughulikia wameajiriwa ktk dhama zake? Mengi anayoyashughulikia yalifanyika awamu zilizopita, usimtetee na hilo linamuhusu aangaike nalo. Tofauti na hapo uchungu na nchi yake siuoni mkuu
 
huu mfupa unaweza ukamshinda
But if he goes after this, he leaves a legacy, kwamba kweli he walks the talk- kuhusu kupambana na ufisadi, and people might actually disregard his inaction on the lugumi scandal


Yes sasa afanye kwa vitendo yale anayoyahubiri kutwa kucha majukwaani.
 
Umeongea point kabisa

Upo umuhimu wa kuhoji...pesa halali hata siku moja haiwez kutumika hivyo...jins huyo ruge anaemtetea alivyotapanya mabilion kwa kina tibaijuka...chenge...ngeleja na hadi maaskofu eti kisha uje tuh useme kirahis rahis kuwa inawezekana?hiyo haingii akilin...

Wote wenye case ya kujibu wasiachwe katika hili
Nadhani unajaribu kumuondoa huyo unayemuita Ruge, lakini bado swali kubwa ni je, Ruge na hata huyo Singa walistahili kugawana pesa hizo? Hili ni muhimu kujibiwa. Kama hazikuwa pesa zao, basi wote ni wachafu bila kujali kama alitaka kuzulumiwa na nani.

Jinsi alivyozigawa kuna kitu hapo. Pesa ya halali haiwezi kugawanywa kiasi hicho. Hatuhitaji kuambiwa ni uamuzi wake, common sense hairuhusu jibu la aina hiyo. Je, hao ndo walimpa siri kwamba pesa imechotwa? Je, Nani ktk uongozi wa serikali iliyo timamu anaweza kuruhusu kiongozi kupewa pesa na mtu yeyote kiwango hicho na asiulizwe zimetoka wapi?

Tuwe wakweli wa maouvu. Hakuna haja ya kumtetea mtu muovu hata kama yuko kimya.
 
Hao watumishi hewa anaoshughulikia wameajiriwa ktk dhama zake? Mengi anayoyashughulikia yalifanyika awamu zilizopita, usimtetee na hilo linamuhusu aangaike nalo. Tofauti na hapo uchungu na nchi yake siuoni mkuu
unaelewa maana ya watumishi hewa??Bora hata ungesema vyeti feki
 
Kitu ninachokiamini kwasasa ni Kuwa Rais ajaye hatokuwA na matatzo ya kushughulikia ufisadi wa kipindi cha magufuli. Hili ni fanikio letu kubwa kwetu watanzania.

Magufuli atatumia muda wake mwingi kuhangaishwA na ufisadi kuanzia wa kipindi mwinyi kama mambo ya ngorongoro, kipindi cha mkapa kama mambo ya uuzwaji WA mali za umma kwa bei chee mpaka kipindi cha kikwete kama escrow na nk.

Naamini kipindi chake magufuli hatotengeneza ufisadi. Safi sana.
 
umesahau na serikali ya ccm kwenye hill kundi la wazi maana pesa zilikuwa za tanesco na kuhifadhiwa kwenye benki ya umma lakini raid wetu na mwenyekiti wa ccm akaikataa hadharani kuwa benki kuu si benki ya umma wa tanesco si shirika la umma na kwa maana hiyo hata hizo pesa tena madafu si za umma
Jibu sahii Ni hili soma ile hukumu Tena:
"
"SCB-HK understands that PAP used $75 million of the funds obtained from the escrow account to pay VIP Engineering and Marketing Limited (owned by Tanzanian businessman James Rugemalira) for its 30 per cent shareholding in IPTL," says part of the 100-page ruling.

"The funds held in the escrow account that should have been available to satisfy TANESCO's payment obligations to IPTL under the PPA (power purchase agreement) have therefore been paid to two Tanzanian parties - VIP and PAP - neither of whom made any financial contribution to the construction of the facility," it adds."

Hizo pesa zilikuwa mkopo Siyo zawadi hiyo pesa hawakuitolea jasho. Ruge Na PAP wote wezi.
 
Nywele zinakuwa nyeupe kuanzia kichwani mpaka kidevuni, sidhani kama ana lala masaa nane mkuu.

Ni ngumu sana kushughulikia ufisadi ambao Rais aliyekutangulia kuna harufu ya kuhusika. Hasa hasa kama mlikuwa chama kimoja na katiba inasema hawezi shtakiwa hata akitoka madarakan.
 
Ni ngumu sana kushughulikia ufisadi ambao Rais aliyekutangulia kuna harufu ya kuhusika. Hasa hasa kama mlikuwa chama kimoja na katiba inasema hawezi shtakiwa hata akitoka madarakan.
Ni kama mzinga wa nyuki, uguse kwa tahadhari.
 
Bila katiba mpya na chini ya utawala wa ccm tutabadirisha tu majina ya ufisadi toka EPA,Richmond, Escrow,huwezi kuutenganisha huu ufisadi mkubwa na ccm,wewe endelea kujidanganya.mark my word
Kitu ninachokiamini kwasasa ni Kuwa Rais ajaye hatokuwA na matatzo ya kushughulikia ufisadi wa kipindi cha magufuli. Hili ni fanikio letu kubwa kwetu watanzania.

Magufuli atatumia muda wake mwingi kuhangaishwA na ufisadi kuanzia wa kipindi mwinyi kama mambo ya ngorongoro, kipindi cha mkapa kama mambo ya uuzwaji WA mali za umma kwa bei chee mpaka kipindi cha kikwete kama escrow na nk.

Naamini kipindi chake magufuli hatotengeneza ufisadi. Safi sana.
 
Ndio maana white hair alikatwa akawekwa atakaye weza kuwalinda...
Tatizo huyu aliwekwa kuwalinda kuna muda anajisahau hadi anatoa siri zao...
 
Katika mradi huo sidhani Ruge alikuwa kachanga hata senti kununua ile mitambo na kuisimika,yeye katika ubia huo alikuwa katoa shamba lake la mihogo kama plot,
nadhaani malipo yalipotoka singer akaona uzito kugawana na ruge ambae hakuwa na mchango wa pesa katika mradi zaidi ya kiwanja na kuwa na connection serikalini.
Ni baada ya ruge kuona yeye kama mbia anaweza asiambulie kitu ndo kaenda mahakamani,na singer akaona isiwe tabu kama mradi ukiwa wake na akamudu kuzalisha megawat 500 atakula hela ndefu kuliko vile vijisenti,akaamua kununua zile asilimia 30 za hisa za Ruge kwa bilioni 75,akampay off,

Ruge ambaye alikuwa hajawahi kukamata kitita kama hicho akapagawa,akaanza kulipa fadhila,
sijui ile plot aliipataje,ruge akampa tibaijuka bilion moja,kumbuka kipindi hicho tibaijuka alikuwa waziri wa ardhi,nadhani ile haikuwa rushwa bali shukrani,akakumbuka pia maaskofu walikuwa wakimuombea na baraka zimefurika,akawapa mabilioni,akagawa makanisani na baadhi ya viongozi waliokuwa wakimnyooshea mambo yake,actually katika bilion 75 inawezekana alitumia bilion 5 tu kugawa takrima,bilioni 70 akatia kibindoni na kuachana na PAP.
SASA katika hela ya escrow ukitoa ile alilipwa ruge zinabaki ngapi vile?

Unafikiri Mr Waitu asingekuwa na mpunga mrefu si angekuwa bado analalamika, neema iliyopo inatosha mpaka wakuu na mwanae akishonea nguo mawaziri wa kike na wake wa mawaziri.
 
Atakuambia ni utawala wa sheria acha vyombo husika vifanye kazi yake kwakua tyr washanzisha mahakama hzo huku wakisema wanasubiri rufan iliyokatwa na tanesco kuzaa matunda..
Wanasheria wenyewe ni hawa wanaogalagazwa na Tundu au kuna wengine?
 
Wanasheria wenyewe ni hawa wanaogalagazwa na Tundu au kuna wengine?
Hawana wengine zaidi ya mkono

Saiv wanasema wanasheria wa tanesco wakate rufaa
Wakati nimefatlia tarifa ya zito ni kuwa hiyo ni mahakama ya mwisho sasa sjui rufani inakatwaje pia sielew daily news na habari leo yana milikiwa na nanii
 
Back
Top Bottom